Waziri wa nishati, Umeme huu wa Nkasi vipi?

Waziri wa nishati, Umeme huu wa Nkasi vipi?

VYEMELO

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2020
Posts
349
Reaction score
464
Ndugu Waziri wa Nishati, mheshimiwa Januari Makamba, ninakuandikia kwa masikitiko makubwa juu ya KERO YA UMEME wilayani Nkasi. Umeme unakatika mara kwa mara isivyo kawaida. Ni kero. Biashara za watu zinazotumia Nishati hii muhimu zimedorora na nyingine zimefungwa kabisa. Vifaa vingi vya umeme vinaungua majumbani mwa watu kila siku. Wananchi tunajiuliza, Tatizo lipo wapi? Tatizo lisiloisha! Umeme unawashwa dakika kumi unazimwa. Hivyo hivyo!

Je, ni Tatizo linalosababishwa na uchakavu wa vifaa? Upungufu mkubwa wa mafuta? Au ujuzi mdogo wa wahandisi na mafundi sanifu wa umeme?

Tunashauri: TANESCO walitafutie ufumbuzi wa kudumu Tatizo hili. Iwapo wamebaini Tatizo linalosababisha umeme kukatika-katika hovyo, Si wakae na kutengeneza kabisa hata kama itachukuwa miezi sita, na kadhalika, ili watakapowasha mitambo, Iwe moja kwa moja. Hii "danganya toto" haifai hata kidogo. Serikali inajivunjia heshima.

Mheshimiwa Makamba tunakuomba fuatilia shida hii Nkasi, Isije ikawa baadhi ya Watumishi wachache wa TANESCO wasio waaminifu wanahujumu juhudi za Serikali za kuhakikisha Nchi inatoka gizani. Wanakuharibia mheshimiwa. Ni mengi yasiyopendeza yameanza kusemwa juu ya kadhia hii; Si unajua hii ndiyo Wilaya pekee Nchini ina Jimbo linaongozwa kisiasa na Chama cha Upinzani? Wananchi wameanza na Kumkumbuka mbunge mstaafu Ally Mohamed Keissy; Inawezekana angekuwepo Bungeni haya yasingetokea.Tafadhali tusaidie Waziri. Wananchi Tunateseka.
 
Ndugu Waziri wa Nishati, mheshimiwa Januari Makamba, ninakuandikia kwa masikitiko makubwa juu ya KERO YA UMEME wilayani Nkasi. Umeme unakatika mara kwa mara isivyo kawaida. Ni kero. Biashara za watu zinazotumia Nishati hii muhimu zimedorora na nyingine zimefungwa kabisa. Vifaa vingi vya umeme vinaungua majumbani mwa watu kila siku. Wananchi tunajiuliza, Tatizo lipo wapi? Tatizo lisiloisha! Umeme unawashwa dakika kumi
Tumepokea taarifa kwa ufatiliaji na hatua zaidi

Huduma kwa wateja

MAKAO MAKUU
 
Ndugu Waziri wa Nishati, mheshimiwa Januari Makamba, ninakuandikia kwa masikitiko makubwa juu ya KERO YA UMEME wilayani Nkasi. Umeme unakatika mara kwa mara isivyo kawaida. Ni kero. Biashara za watu zinazotumia Nishati hii muhimu zimedorora na nyingine zimefungwa kabisa. Vifaa vingi vya umeme vinaungua majumbani mwa watu kila siku. Wananchi tunajiuliza, Tatizo lipo wapi? Tatizo lisiloisha! Umeme unawashwa dakika kumi
Kwani huko nkasi hamna mbunge? Wakuwasemea
 
Nasikia TANZANIA wamesema watapunguza makali ya mgao was umeme labda ndo wameamua wawe wanawasha wanazima..😂
 
Ndugu Waziri wa Nishati, mheshimiwa Januari Makamba, ninakuandikia kwa masikitiko makubwa juu ya KERO YA UMEME wilayani Nkasi. Umeme unakatika mara kwa mara isivyo kawaida. Ni kero. Biashara za watu zinazotumia Nishati hii muhimu zimedorora na nyingine zimefungwa kabisa. Vifaa
Ndugu Mteja wetu!

Tunakujulisha kuwa tumekuwa na changamoto kwenye moja ya mashine umba yetu iliyosababisha kuwa ya upunguza wa umeme hivyo kuathiri baadhi ya maeneo ya Mkoa wetu wa Rukwa.

Hatua tulizochukua

Zoezi la ufungaji wa mashine umba kubwa mpya yenye uwezo wa 15MVA lipo katika hatua za mwisho na tunategemea kukamilika zoezi hili mwishoni mwa mwezi wapili 2022,

Shirika limekuwa likitoa taarifa kupitia njia mbalimbali ikiwemo kutumia Radio Nkasi, Magroup ya WhatsApp na matangazo ya moja kwa moja.

Uongozi wa TANESCO unawaomba wananchi wote wa Mkoa wa Rukwa kuwa na matumaini ya hali ya umeme kuwa nzuri zaidi mara baada ya kumamilisha ukarabati wa mashine mpya

TANESCO HUDUMA KWA WATEJA

Makao Makuu
 
Ndugu Mteja wetu!

Tunakujulisha kuwa tumekuwa na changamoto kwenye moja ya mashine umba yetu iliyosababisha kuwa ya upunguza wa umeme hivyo kuathiri baadhi ya maeneo ya Mkoa wetu wa Rukwa.

Hatua tulizochukua

Zoezi la ufungaji wa mashine umba kubwa mpya yenye uwezo wa 15MVA lipo katika hatua za mwisho na tunategemea kukamilika zoezi hili mwishoni mwa mwezi wapili 2022,

Shirika limekuwa likitoa taarifa kupitia njia mbalimbali ikiwemo kutumia Radio Nkasi, Magroup ya WhatsApp na matangazo ya moja kwa moja.

Uongozi wa TANESCO unawaomba wananchi wote wa Mkoa wa Rukwa kuwa na matumaini ya hali ya umeme kuwa nzuri zaidi mara baada ya kumamilisha ukarabati wa mashine mpya

TANESCO HUDUMA KWA WATEJA

Makao Makuu
@TANESCO Tatizo la umeme nkasi ni shida ya mda nazani toka mwezi wa 12/ 2021 na tuliambiwa tatizo litaisha mwezi wa kwanza kati kati cha kushangaza hadi saiv shida kama inaizidi na hili tatizo linasababisha hasara kwa wafanya biashara wengi kwani uku kuna uvuvi sana wa samaki,
Kuna kipindi tulitembelewa na waziri wa maji, ila wananchi wakawa wanamlalamikia sana shida ya umeme kukatika ovyo
Fanyeni marekebisho ili watu waendelee kununua umeme na nyie mjiongezee makusanyo yakuondesha shirika lenu vizuri
 
@TANESCO Tatizo la umeme nkasi ni shida ya mda nazani toka mwezi wa 12/ 2021 na tuliambiwa tatizo litaisha mwezi wa kwanza kati kati cha kushangaza hadi saiv shida kama inaizidi na hili tatizo linasababisha hasara kwa wafanya biashara wengi kwani uku kuna uvuvi sana wa samaki,
Kuna kipindi tulitembelewa na waziri wa maji, ila wananchi wakawa wanamlalamikia sana shida ya umeme kukatika ovyo
Fanyeni marekebisho ili watu waendelee kununua umeme na nyie mjiongezee makusanyo yakuondesha shirika lenu vizuri
Ni kweli limeanza kipindi cha Decemba 2021 ambapo mashina ziliharibika na kazi ya kuweka mashine mpya inaendelwa na inahitaji muda
 
Back
Top Bottom