Waziri Wa Polisi Aibiwa Gari


Kamanda hapo chumvi umezidisha, Mkuu huyo CCM Maisara sio baraza
yake...
 
GARI la Naibu Waziri wa Usalama wa Raia MOHAMED ABOUD Mohamed, lenye alama, NW-UR,aina ya GX, limeibiwa na dereva wake aitwaye Tumaini Mbaga, ametoweka tokea Jumamosi iliyopita.

Hii imekaa kama tangazo vile? Kwa mwenye information kitita bei gani? Ihope there is that best part....zawadi NONO
 

Source: Kulikoni Na.234, JANUARI 23, 2008
 
Kamanda hapo chumvi umezidisha, Mkuu huyo CCM Maisara sio baraza
yake...


kaka inaeleweka kuwa ccm maisara si kijiwe cha mshkaji..ILA NIMESEMA KUWA NDIO KIJIWE CHA SIMU POA UNGUJA....UKIKOSA KOOTE NENDA PALE ..HATA ULE MWEZI...,NA HATA KAMA SI MASKANI YAKE ..HAKUNA AL WATTAN UNGUJA ASIYEFIKA PALE JAPO KUSABAHI....ILA KUNA WENYE KIJIWE HIKI ...SIMU POA NA "NDUGU ZETU WALE" WAKIWA MOJA YA WAGENI MAARUFU BARZA LILE....

YULE SERENGETI YAKE YA MOTOOO ..HUPENDELEA ..
 
ila kama wazanzibar wana jidanganya hawaongozwi au hawataongozwa na mlevi wanajidanganya [except for mzee mwinyi,jumbe and wakil..]

Hivi PhM unataka kuniambia Mhd Aboud atakua Rais wa SMZ? Maana niliwahi kusikia mahali kwamba anaandaliwa kwa kuwa yeye ni Mpemba na pia ana asili ya Kiarabu kwa hiyo rangi rangi yake atawamudu CUF katika uchaguzi mkuu ujao
 
hadi dereva apatikane ndio itajulikana kama katoweka nalo au katekwa, hawa polisi wababaishaji hawako competancy kwenye statement zao ndio maana wakikamata watu na bangi au madawa wanajua bei yake kivipiiiiiii!!!!
 
Hivi PhM unataka kuniambia Mhd Aboud atakua Rais wa SMZ? Maana niliwahi kusikia mahali kwamba anaandaliwa kwa kuwa yeye ni Mpemba na pia ana asili ya Kiarabu kwa hiyo rangi rangi yake atawamudu CUF katika uchaguzi mkuu ujao

kumekuwa na hisia ya jk kuwa na lengo la kumjenga SEIF SHARIFF mpya visiwani....anajaribu,...hii itasaidia kuondoa tension iwapo seif mpya atatoka ccm..na hii itawezekana pale tu ccm itakapokubali kumsimamisha mgombea urais zanzibar kutoka pemba[lazima atashinda]...hapo tention ya wapemba itapungua ...na upinzani utapungua ..demokrasia itastawi visiwani...

maana you know hata seif alitofautiana na wenzake baada ya kunyimwa fursa ya kugombea urais..pamoja na kujikomba kwa mwalimu na kumfunulia siri za wachafuzi wa hali ya hewa....

kinachofanyika zanzibar ni kama kenya ambako wakikuyu wanaamini rais bora lazima awe mkikuyu...
 
Duh!!! Hii ngoma bado nzito sasa . Inahama kwenye wizi wa gari inaenda kwenda kwenye kugombea? Aboud hana akili ya Urais nimemsikia akitoa speech zake pale Arusha ni mtupu sana .
 
hadi dereva apatikane ndio itajulikana kama katoweka nalo au katekwa, hawa polisi wababaishaji hawako competancy kwenye statement zao ndio maana wakikamata watu na bangi au madawa wanajua bei yake kivipiiiiiii!!!!

Ngomanzito karibu jamvini
 
Guys Check new development of this story tunaweza kuchangia. Hawa jamaa hawako serious na maisha ya watu !!!

Polisi wahusishwa mauaji ya dereva wa Naibu Waziri




na Happiness Katabazi



JESHI la Polisi nchini linawashikilia watu wanne wakiwemo askari polisi wawili kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa dereva wa Naibu Waziri wa iliyokuwa Wizara ya Usalama wa Raia, Tumaini Mbaga.
Vyanzo vya habari vya uhakika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi viliiambia Tanzania Daima kwa nyakati tofauti kuwa, wengine wanaoshikiliwa kuhusiana na tuhuma hizo ni raia wawili ambao hawakuweza kuthibitisha iwapo ni watumishi wa serikali ama la.

Habari hizo zinaeleza kuwa, watu hao walikamatwa mapema wiki hii na wanaendelea kushikiliwa na jeshi hilo kwa siri.

"Jeshi limewakamata watu hao mapema wiki hii na linaendelea kuwashikilia kwa mahojiano zaidi, lakini hata hivyo baadhi ya maofisa waandamizi wa jeshi letu wanajitahidi kuendesha jambo hili kwa siri," kilisema chanzo chetu cha habari.

Habari hizo zilieleza kuwa chanzo cha mauaji ya dereva huyo ni wivu wa baadhi ya polisi ambao inadaiwa walikuwa wakichukizwa na aliyekuwa Naibu Waziri wa wizara hiyo, Mohamed Aboud, kuendeshwa na dereva ambaye si polisi.

"Inasemekana baadhi ya madereva wa polisi walikuwa wakikerwa na dereva raia kumwendesha naibu waziri wakati madereva wa Jeshi la Polisi wapo," kilieleza chanzo hicho.

Taarifa za kukamatwa kwa watu hao zililifikia gazeti hili mwanzoni mwa wiki hii na tayari habari zimeanza kuenea mitaani.

Chanzo hicho cha habari kilieleza watuhumiwa hao ambao awali walikuwa wakihifadhiwa katika mahabusu ya jeshi hilo iliyopo eneo la Stakishali - Ukonga, lakini sasa wamehamishwa na haijafahamika wako mahabusu gani.

"Mpaka jana watuhumiwa hao walikwishahamishwa kutoka mahabusu hiyo, lakini hatujui ni wapi wamehamishiwa. Wamekuwa wakihojiwa na kikosi maalumu kilicho chini ya Ofisi ya Rais (Task Force), kikosi hiki kinaundwa na vyombo vya ulinzi na usalama kutoka JWTZ, Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa," kilieleza chanzo hicho.

Habari zaidi zinaeleza kuwa askari wanaotuhumiwa katika tukio hilo ni watatu, lakini mmoja alifanikiwa kutoroka baada ya kupata taarifa ya kufichuka kwa siri hiyo.

Miongoni mwa askari waliokamatwa, mmoja anatoka Kituo cha Polisi Msimbazi na mwingine anatoka kitengo cha Upelelezi, Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Mbali na askari hao, pia wapo raia wawili, mmoja wao ni mwanamke ambaye ni raia kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), anayeishi Yombo, jijini Dar es Salaam.

Jana gazeti hili lilifanya juhudi za kuzungumza na Mkuu wa Jeshi hilo, IGP Said Mwema, ili kupata ufafanuzi, lakini halikuweza kuzungumza naye, baada ya simu yake ya kiganjani kupokewa na msaidizi wake, ambaye alieleza kuwa IGP alikuwa kwenye majukumu mengine ya kitaifa nje ya Dar es Salaam.

Aidha, gazeti hili lilifanya jitihada za kuzungumza na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, ambaye baada ya kupatikana hakuwa tayari kuthibitisha au kukataa, zaidi ya kulitaka gazeti hili kuwasiliana na Kamishna wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Alfred Tibaigana kwa ajili ya kupata taarifa za tukio hilo.

Hata hivyo, Kamanda Tibaigana hakuweza kupatikana baada ya simu yake ya mkononi kupokewa na mlinzi wake ambaye aliieleza Tanzania Daima kuwa kamanda huyo alikuwa kwenye kikao ambacho hakufahamu kitamalizika muda gani.

Mwishoni mwa Januari mwaka huu, polisi waliokota mwili wa dereva huyo ukiwa umetenganishwa na kichwa, eneo la Kwembe, ukiwa umeharibika vibaya, ikiwa ni takriban wiki mbili tangu alipotoweka.
 
Our security departments have clearly become sourec of our insecurity. Kweli hii ni hatari, i wonder kama watu watakuwa wanawaamini polisi! Kama kweli hii ilikuwa hivi inakumbusha jinsi askari wa Nduli wa Uganda walivyokuwa wakifanya.
 
Our security departments have clearly become sourec of our insecurity. Kweli hii ni hatari, i wonder kama watu watakuwa wanawaamini polisi! Kama kweli hii ilikuwa hivi inakumbusha jinsi askari wa Nduli wa Uganda walivyokuwa wakifanya.

Jeshi la polisi linapaswa kujisafisha au kusafishwa, matukio ya hivi karibuni yanaonyesha wazi uozo wa polisi tulionao. Angalia kisa cha kuuawa kwa wafanya biashara kutoka Mahenge (ambapo mkuu wa Zombe alihusika), kupigwa hadi kuchomwa visu viongozi wa CHADEMA huko Karatu, kuua dereva wa bossi wao nk. Ni dhahiri kwamba polisi wamepoteza dira, endapo hawawezi kujisafisha (IGP kuchukua hatua za makusudi) basi wasafishwe (Rais achukue hatua stahili, ikiwezekana kupangua ma RPC, ofisi ya DCI, wapelelezi, kitengo cha madawa ya kulevia nk.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…