real G
JF-Expert Member
- Feb 7, 2013
- 5,227
- 5,299
Mahakama Kuu nchini Kenya, imewapiga faini ya shilingi za Kenya 200,000, waziri wa mambo ya ndani Fred Matinag'i (mbele kushoto) na Inspekta jenerali Mkuu wa Polisi Joseph Boinnet (hayupo pichani) kwa kosa la kudharau mahakama. Jaji George Odunga aliwaamuru maafisa hao waandamizi wa serikali kufika mahakamani siku ya Jumatano, kwa ajili ya kuhukumiwa, baada ya kutiwa hatiani kwa kudharau mahakama walipokataa kumuachia mwanasiasa wa upinzani Miguna Miguna. Odunga ameagiza pesa hizo zikatwe kwenye mishahara yao.
Chanzo: DW
Chanzo: DW