Wazo 34

Wazo 34

OGOPASANA

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2009
Posts
262
Reaction score
144
Habari GTs,
lifuatalo ni miongoni mwa mawazo kadhaa ninayoyafikiriaga mara kwa mara, hivyo nikawiwa kushare na wanajukwaa nikitumaini pengine kuna watakaoweza kunufaika nalo.
- chukulia ukanunua kiwanja cha kutosha kujenga ukumbi wa kuhudumia watu 500 hasa ktk mikoa ama wilaya zenye pilika pilika, ktk huduma za shughuli mbalimbali kama vile harusi, kitchen party, send off, kipaimara, birthday party, ubatizo, gratuation, engagement, sherehe za pongezi na kadhalika. Hakikisha eneo husika liwe na facilities muhimu kama parking, washrooms za kutosha nk.
- jaribu kuwa na wengine kwa kufanya gharama zako kuwa ktk bei mmoja kiujumla yenye mahitaji yote. Mfano TSHS 30,000 kwa mtu mmoja ambayo itakuwa ni gharama yenye kujumuisha chakula, vinywaji, mapambo, still pictures, video recording, overhead projector, cake na kadi za mialiko. (Huduma hizi zote zitolewe kwako kwa gharama hiyo utakayoipanga). Mtera aje Na MC wake tu.
- Kwa makadirio ya chini fanya kwa wiki upate biashara 3 kwa watu wasiopungua 300, hivyo:
Kwa siku = TSHS 30,000 X watu 300 = TSHS 9,000,000
Kwa wiki = TSHS 9,000,000 X 3 = TSHS 27,000,000
KWA mwezi = TSHS 27,000,000X 4 = TSHS 108,000,000
Kwa mwaka = TSHS 1,296,000,000

- bottom line kwa mawazo yangu, inanekana ni biashara yenye kuingiza kipato kizuri na kuwa na matumizi na rasilimali watu kidogo. WAZO hili unalionaje???

nawasilisha.
 
Duh mkuu mi sijakusoma freshi japokuwa nimerudiarudia kuisoma hii thread .,ngoja nikae kimya kuwapisha watakaoelewa vizuri hii thread.
 
Duh mkuu mi sijakusoma freshi japokuwa nimerudiarudia kuisoma hii thread .,ngoja nikae kimya kuwapisha watakaoelewa vizuri hii thread.

Wapi hujaelewa Mkuu nijaribu kukuelewesha?
 
Wazo zuri, ila unahitaji kuweka uhalisia.
 
Back
Top Bottom