Wazo 35

Wazo 35

OGOPASANA

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2009
Posts
262
Reaction score
144
Habarini,
Hili ni Wazo ninaloona laweza kuwafaa vijana wengi hasa wahitimu wanaosubiri kupata ajira na hasa wenye uelewe na ICT na uwezo wa kuongea na watu vizuri.
- tengeneza business cards zenye jina lako na mawasiliano yako.
- nunua External hard Disk yenye uwezo mkubwa. Eg TB 1
- ijaze external hiyo na softwares, programs na applications zote muhimu zinazohusiana na matumizi ya computer ktk maofisi, stationeries, na majumbani.
- sasa anza biashara kwa kuwatembelea wenye viofisi vidogo vyenye computer na stationeries mtaa kwa mtaa na kujitangaza kuwa unatoa huduma ya kutoka virus kwenye computers, kurudisha mafia ili yaliyopotea, kuwekea antivirus mpya (yenye lifetime keys), kuinstall programs muhimu kama Microsoft office, adobe, operating systems nk kwa gharama nafuu ya TSHS 10,000 kwa huduma zote hizo.
- Nina hakika kama upo serious, sidhani kama utakosa wateja 3 wenye kuhitaji huduma hiyo. Je kiwangu hicho cha mapato kwa siku hakitoshi kufanya jambo la maana baada ya muda Fulani?

nawasilisha.
 
Ahsante sana kaka, wazo zuri sana hili. Pia jamani tujitahidi na kuongeza ubunifu ili kuwa na competition ndogo. Pamoja na wazo la hapo juu, unaweza kuongezea kwa kuburn na kuuza CD za program au applications ukapiga pesa. Maisha ya sasa magumu jamani, na kupata kazi ndo ngumu kabisaaaa... Cha msingi hata kama umehitimu degree ya kumi usidharau wala kubagua shughuli ya kufanya, as long as inakuzalishia na kukupa starter ya kuweza kufanya shughuli zako ambazo unazipenda. Otherwise sio lazima kufanya kazi ya kitu ulichosomea, jali pesa na maisha yaendelee
 
Back
Top Bottom