Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Katiba Mpya ndiyo suluhisho la Changamoto zote hizi.
 
Hakuna ndugu yako yeyote aliyeahiriki uandikishaji wa wagombea wa serikali ya mitaa na kijiji uwaulize walichokua wanakifanya na maagizo waliyopewa?.

AU unataka kuchosha watu? au wewe unadhani nchi ni ya ccm au wananchi?
 
Too low..

Point no 5 ulitaka CHADEMA wawe na mbinu ya kuwapata wasimamizi kama ikitokea hawawakuti maofisini wakati wanarudisha forms, kwani huo ndio utaratibu watu watafutane au utaratibu ni wasimamizi wawepo ofisini kusubiri wagombea wakati wakirudisha forms??
 
Kuna upumbavu mwingi unaendelea kwenye nchi yetu alafu kuna watu wanajitoa fahamu kulaumu upinzani na kushabikia upuuzi huo.

Kabla ya kushabikia haya yanayofanyika hebu tuwawazie hawa Wasimamizi Wasaidizi (Watendaji) hivi watendewa wa dhuluma hizo wakiamua kupanga ovu lolote dhidi yao watakwepea Wapi?

Wagombea wa CCM walisaidiwa ujazaji na hao hao wasimamizi, na walipewa fomu Mara nyingi iwezekavyo kila ilipotokea wamekosea walibadilishiwa fomu, wakati Wagombea wa Upinzani walipewa copy moja Mara moja tu tena bila maelekezo yoyote ukikosea inakula kwako.


Tuache ushabiki wakipuuzi puuzi hatuna nchi mbadala zaidi ya hii tuliyopo.
 
2202094_Screenshot_2019-11-03-12-57-23.png


Katika hali kama hii hata wangerudisha fomu mwezi mmoja kabla nani angepokea ? unafahamu kwamba watendaji walifunga ofisi muda wote huku wagombea wa ccm fomu zao zikikusanywa gizani lakini bado unaleta uzushi huu ! Hakika Mwanakijiji umepauka vibaya sana ! Tatizo nini , ukabila au njaa , au vyote pamoja ?
 
Yaani Tanzania nzima unataka utueleze leo mfano Dar pekee mitaa zaidi ya mia tano 28 tu ndiyo wameweza kujaza form vizuri. Yaani Chadema tu ndiyo hawajui kujaza form!! tumefika mbali sana hata wale niliowahi kuheshimu nakala zao ni pumba tu
 
Pendekezo Moja: CDM ije na sera ya wazi na maelekezo ya wazi kuwa wagombea wake wote wahakikishe wanarudisha fomu siku tano kabla ya mwisho wa siku iliyowekwa. Mtashangaa tofauti itakuwa nini hapa.
Viongozi wa juu wapo bize kutafuna ruzuku
Niliwahi kuchangia humu,nikauliza john mrema ,mkurugenzi wa halmashauri na bunge amejikita tu ufipa kusubiri apige ruzuku,huku wagombea hata kujaza fomu hawajui
 
Ccm ambayo inaongoza kwa mbumbumbu imeweza kujaza form halafu vyama vingine vyote wameshindwa ayo maneno uliyoandika waambie wapumbavu tu ndio watakuelewa.
Mkuu hapo kwenye maandishi yaliyokolezwa ni mtazamo au hisia zako tu, unaweza usiwe sahihi.
Una kipimo gani cha kusema hivyo?
Ushahidi unaonesha CCM maeneo mengi wameweka watu wenye elimu kubwa au elimu ya juu wakati upinzani wameweka vijana wenye elimu ndogo ila ni maarufu.

Unakuta huyo wa CCM ameshashika nyadhifa kubwa hata mkuu wa chuo cha elimu ya juu lakini bado CCM wamempa mafunzo juu ya ujazazi fomu za wagombea na namna ya kuendesha kampeni.
Huyo msomi wa CCM unakuta amezowea kujaza nyaraka za serikali n.k.
Mfano huku kwetu Ubungo Msewe mgombea wa CDM ni form 6, ana uzoefu wa kazi za ulinzi, wakati CCM wamemuweka Mzee aliyewahi kuwa mkuu wa chuo cha Takwimu Changanyikeni. Nadhani hapo unaona tofauti kubwa.

Mnakumbuka jambo dogo tu la kujaza fomu ya mchezaji bora wa FIFA ilimuharibia sana Mohamed Salah pale uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Misri walivyojaza kwa herufi kubwa sahihi zao kwenye fomu za kupigia kura. Herufi kubwa au ndogo inaweza kukunyima ushindi kwa kukiuka mashariti.

Dharau na dhana kama zako ndio husababisha viongozi wa upinzani hasa CDM kutokuchukua hatua za makusudi kutoa elimu na mikakati kwa wagombea wao jinsi ya kujaza fomu, kujilinda wasikosee kitu ktk kampeni na kutenguliwa ushindi wao. Hii kujiamini sana bila mipango na mikakati ni kosa la kiufundi.

Mwisho ningependa kuwatetea upinzani hasa CHADEMA kwenye suala la kukatazwa hata mikutano ya ndani kunaweza kuwa kumechangia sana wao kushindwa kutoa mafunzo kwa wagombea wao na wasimamizi kwa gharama nafuu kwa kuwakusanya pamoja badala ya kuzunguka nyumba hadi nyumba au kila kitongoji.

Kwahili la kuzuwia mikutano hadi ya ndani ya wapinzani huku wao wakifanya ni aibu na fedhea kwa serikali na CCM, hamuwezi kujivua lawama za uvurugaji demokrasia. Kwa hili nawaambia historia itawahukumu wote mliohusika hata siku mkitangulia mbele za haki, huku nyuma mtaacha maandishi mengi ya kuwaandika ubaya juu ya jambo hili. Mngeacha tu mikutano ya ndani hakuna baya lingetokea kwa taifa, lakini haya mliyofanya yanapika hatari kubwa ya chuki na uhasi kama wa jirani zetu nchi zilizotuzunguka.
 
Back
Top Bottom