Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Mkuu Mwanakijiji umeongea vizuri sana, lakini wana Chadema wanaojiona wana akili kuliko wengine wataishia kukutukana badala ya kujibu hoja.
 
Maswali haya naona yanahusu hata ACT Wazalendo... ni katika kuelewa masuala ya upinzani hasa kwenye mazingira ambayo wanajua kabisa hawawezi kutendewa kwa haki.

Nilichokigundua kwako ni muandishi mzuri uliyejaa nadharia na hujui lolote kwenye uhalisia. Yaani kwa akili yako tu umeshindwa kuona nia ovu hata ya kutoa tu hizo fomu? Hayo unayoshauri kuwa cdm wasimame vijana mpaka fomu zao zichukuliwe, unajua hata kanuni tu hazitaki kuwa na wapambe wakati wa urejeshaji fomu? Isitoshe hilo unaloshauri la vijana kusimama mpaka fomu zao zichukuliwe huitwa uvunjifu wa amani. Hilo unaloshauri ndio cdm waliwahi kulitumia mpaka leo akina Mbowe & co Wana kesi mahakamani.

Naomba nikuulize ili ujue ww unapungukiwa na busara hata kama una mtiririko mzuri wa uandishi. Lengo lilikuwa ni uchaguzi na sio umahiri wa kujaza fomu. Hizo techniqualities ziko upande wa upinzani tu? Hizo fomu za safari hii ndio ulikuwa uchaguzi au uchaguzi ni jambo jingine? Mbona hizo fomu zimezidi hata huo uchaguzi wenyewe? Hizo figisu zote kwa wapinzani kupata fomu mpaka kuzirejesha hukuzisikia huko ulipokuwa, au macho na masikio yako yamesikia tu hiyo Hadaa ya kujaza fomu?

Ni hivi mzee naomba nikusaidie kitu, aliye nyuma ya hii hujuma ya kitoto kwenye huu uchaguzi ni rais, hilo wala halina mjadala. Anaamini kuwa yeye na ccm wanakubalika hivyo wana uhalali wa kushinda. Lakini kitendo cha watu wengi kususia kujiandikisha kimemtisha yeye na chama chake, ndio maana akaamua ufanyike uhuni huu unaoendelea kwani uhakika wa kushinda haupo. Na isitoshe voters turnout pia haiwapi raha, maana hawawezi kutamba kuwa wanakubalika wakati watu hawajitokezi kupiga kura, hivyo namna pekee ni kuhujumu wapinzani ili ccm ipite bila kupingwa, na aibu ya idadi ndogo ya wapiga kura isiwepo.
 
Wakikuelewa najinyonga kweupeee hadharani
 
Namba 5:

Baadhi ya wagombea wa CDM walikuwa wabishi wakishinda Ofisi za watendaji walikamatwa na polisi na kubambikiwa tuhuma mbalimbali.

Nilitegemea uje na makala ukihoji kwanini Watendaji walipotea ofisini wakati wa zoezi la urejeshaji wa fomu n.k
 
Maswali haya naona yanahusu hata ACT Wazalendo... ni katika kuelewa masuala ya upinzani hasa kwenye mazingira ambayo wanajua kabisa hawawezi kutendewa kwa haki.
Wewe ulishaamua kumuunga mkono Magufuli na mambo yake yote. Tuache tafadhali na yatakayotokea kwa hao watendaji uje hapa kutoa uzi wa kuwalaumu!
 
Jamii Forum is dead.., hoja hujibiwa na hoja sio personal attacks.., hata kama huyu mleja uzi ameeka vibaya, ni kibaraka..,. hana akili, hajui kinachoendelea, ni mpuuzi n.k. Je mpuuzi na asiyejua hastahili kujibiwa kile alichouliza.., sababu kumkumbusha kwamba hajui sio kujibu swali lake bali ni matumizi mabaya ya post na ujazaji wa server...
 
Miaka haigandi; kwani kabla ya 2014 watu walikuwa hawaenguliwi? au 2014 wagombea wote wa upinzani walipitishwa? Au mmeshasahau?
We jamaa unatafuta matusi ya vijana bila sababu.. bora ukae kimya kwa Muda.. pengine ikqtunza heshima yako kidogo iliyo baki. ..
Muda ni mwalimu mzuri sana.... hiyo CCM yako italazimishwa kukubali demokrasia hata kwa gharama kubwa namna gani
 
Hii ndio aina ya watu wenye ndoto za kuitoa ccm madarakani, SILIONI HILO LIKITOKEA ANGALAU KWA MIAKA HII YA KARIBUNI.

KWANINI
Malalamiko sio hoja. Hoja unatakiwa kujibiwa je? Mlijipanga vipi na mliwapanga vipi wagombea wenu, kuhusu taratimu na hoja za kifundi zinazoweza kuwaondoa wagombea wenu?.

Hivi wewe ungekua mwalimu umemwambia mtahiniwa kuandika kuandika sentensi ya kiswahili alafu akaandika NAOMBA KUGOMBEA SERIKALI ZA MITAA ungelimpa vema?

Je! Ungeenda kituo cha polisi au mahakamani ukaulizwa unafanya kazi gani ungemjibu hakimu kwamba wewe Ni MPAMBANAJI?

Ifike wakati tujifunze kuheshimu taratibu kwakua muhusika anahiari ya kukuonyesha huruma au kukuchinjilia mbali na usipate pa kwenda kushitaki.

Mzee Mwanakijiji, hawa watoto na wazee wenzio pia watakukashifu, watakutusi na mbali ya yote watasema unatumika.

Na kama utakua unatumika kweli utakua unaitumikia akili na Muumba wako na si chengine.
 
Inasikitisha sana wale tunaowaamini wanatuangusha...
Yaani nchi nzima kweli wagombea wa vyama vya upinzani tu ndio hawajui kusoma au hawajui kujaza fomu....CHADEMA AMBAYO WANACHAMA WAKE WENGI NI WASOMI IZIDIWE KUJAZA FORM NA MWANACHAMA WA CCM ngazi za chini wasiojua kusoma na kuandika....yaani kuna sehemu hata kiswahili hawajui ...kuandika ndio kabisa....Mwanakijiji unaenda unapoteza heshima yako uliyojijengea.
 
Katiba Mpya ndiyo suluhisho la Changamoto zote hizi.
Kenya wanakatiba nzuri na kila wakifanya uchaguzi lazima wachapane, kwako mwalim Kashasha unalizungumziaje hili?

Kenya wanakatiba nzuri na wanaongoza kwa ufisadi. Kwako Sudi mkumba.

Kenya wanampaka mashine ya kupima kama unasema urongo au la na wanaongoza kwa uongo, kwako kiungo mkata shombo Mwanaid Suleiman.
 
Mzee Mwanakijiji, Nadhani kama ningelikuwa mkuu wa kaya yetu pendwa, Leo leo ningelimfukuza kazi huyo waziri wa tamisemi na kumfungulia makosa ya uhujumu uchumi. Halafu ningeliufuta huu uchafuzi aliouweka niamuru fomu mpya, zisizo na mitego niweke hadharani kabisa mwezi mzima kabla fomu hazijatoka. Watu wazisome, wazijadili, wakazijaze. Ili kuwe na uchaguzi sio uteuzi. Mtu kuenguliwa ili mwingine apite bila kupingwa huo ni utoto.
Sisi tumeyaona yoote aliyoyafanya mkuu na tumeyakubali kwani yanajieleza yenyewe. Kuna shida gani kumpenda aendelee kuongoza?? Tusiseme kuwa tuna hofu kushindwa uchaguzi. Hata zuzu tu atamchagua kwa kishindo. Ila mafindofindo kama haya, yanamharibia sifa sana
 
Maswali haya naona yanahusu hata ACT Wazalendo... ni katika kuelewa masuala ya upinzani hasa kwenye mazingira ambayo wanajua kabisa hawawezi kutendewa kwa haki.
Hivi lengo la wasimamizi wa uchaguzi ni nini? Ni kuwezesha wagombea waweze kushiriki uchaguzi? Ktk hali ya kawaida, wangetakiwa kuwa-facilitate wagombea na kuhakikisha wanajaza fomu kwa usahihi kuliko walichofanya; kutafuta kasoro za kuwaengua na kuhakikisha fomu zao hazipokelewi kwa kukimbia ofisi?

Vv
 
Maswali yako ni fikirishi kama tu Tanzania kungelikuwa na demokrasia ya magharibi...
 
Mapendekezo ya wagombea ni suala la wananchi husika ku propose kiongozi wanayemtaka.

Hizo technicalities lazima ziwe rafiki kwa uchaguzi, kwa mfano kama mtu ni jambazi na ana record hiyo ni automatic rejection.

Lakini kuongeza vipengele utafikiri mtihani wa form IV , hiyo ni kuua demokrasia.

Mimi CCM damudamu lakini nisingependa kushindana na ombwe.
 
Hata kama Chadema wangekubali kushiriki uchaguzi, Mimi nisinge nyanyua mguu wangu kwenda kupiga kura.

Maneno ya huyu mzee yana ukakasi sana na yeye yupo behind na yale wanayofanyiwa wapinzani.

Sijui kwanini CCM mlimpitisha huyu firauni na hatimaye amekuja kuwa rais .
 
Siamini kuwa Mwanakijiji amepungukiwa ufahamu ila huenda anautamani ujinga, na ili kuufikia anafanya kila jitihada kujitoa ufahamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…