Wazo la biashara Morogoro mjini

Wazo la biashara Morogoro mjini

mkuu fanya biashara ya samaki wabichi unatoa mtera unapeleka kweny mabucha hapo mawenzi utanishukulu
 
Hivi zile mbogamboga za majani zinazo ingia Dar es Salaam kule soko la Ilala kila siku kutokea Morogoro huwa zinalimwa wapi? Yaani ni vijijini gani kwa huko Morogoro
Ndio aende vijiji vya kilombero huko kuna fursa nyingi. mfano tuliani, mngeta, mlimba, Chitamlela, mang'ula n.k akiwa na mil 3 inatosha kwa kuanzia.

Baada ya miaka miwili aje hapa kutupa mrejesho.
 
Kwa huo mtaji kama unataka kuishi nao mjini basi kodi kibanda cha machinga kingalu sokoni, weka bidhaa tofauti tofauti, weka kipaza sauti... Hukosi ya kula na kuendeleza mtaji mpaka kuja kumiliki fremu
Hii unamaanisha kuwauzia machinga au
 
..unataka shughuli ya kukuingizia kipato kila uchwao au una utayari iwe inakuingizia baada ya muda Fulani ..
Kama ni ya kila uchwao ( biashara asubuhi jioni mahesabu ) jaribu biashara zifuatazo
1. Bodaboda - comes with highest risk
2. a) Goli la chips/ndizi/mishikaki/kuku - mwanzoni kulingana na eneo utakalojiset itakuwa ngumu mpaka pakishazoeleka
2. b) Goli la chapati/maharage/supu ya ng'ombe ...bado kwa Moro mjini na viunga vyake vijiwe hivi havijasambaa sana

Kama unataka ya msimu nunua nafaka kipindi cha mavuno weka store then uza baadae, hii inataka umakini wa quality checking unaponunua, nafaka kama mpunga, mahindi, maharage , mtama (mweupe au mwekundu) n.k
Biashara nyingine kwa mtaji wako nenda minadani nunua mbuzi safirisha kupeleka Dar, (Anza na mbuzi wachache) ila kwanza pata taarifa na maarifa namna ya kuwafikisha, vibali, n.k
Nimeipenda hii
 
Back
Top Bottom