Wazo la Biashara ya Kuuza zawadi

Wazo la Biashara ya Kuuza zawadi

sumu-ya-panya

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2016
Posts
632
Reaction score
572
Dunia inabadilika kila siku,binadamu amekua kiumbe hatari zaidi ingawa wenye upendo wapo na wabaya pia wapo.

Ulimwengu huu ni wa usawa na haki hivyo kila mmoja wetu anahaki ya kupata sawa sawa na wengine kulingana na nafasi alio nayo.

imekua rahisi kuonesha upendo kwa uwapendao kwa kuwatumia zawadi michango n.k
lakini imekua ngumu kumuoneaha wazi wazi adunia yako chuki uliyo nayo juu yake ,hakuna sababu ya kushindwa mpa zawadi aduni yako mpe zawadi utayoona inamfaa.

Kampuni mpya niliyoianzisha PANYABUKU inayofanya biashara kwa njia ya mtandao tumekuja na huduma ya kutuma zawadi kwa maadui zako pasipo kuonesha imetoka kwa nani au ukipenda unaweza wekwa pia mtoaji.

katika mtandao wetu tunauza Mahirizi feki, cheni zilizokatika,matambara misalaba,mashada ya makaburini , mizoga,takataka za jalalani, mavi yaliokauka, na mabicho mayai viza yalipasuka au mazima. mafuvu ya wanyama,condom zilizotumika,v itu vilivyoexpire n.k
yote ni kumfanya adui yako asiwe na furaha kabisa, apate presha na ajue anachukiwa , pia tutaweka option ya alietumiwa kifurushi basi anaweza kureply kwa kununua zawadi mbaya zaidi katika mtandao wetu na kututaka tumtumie aliekutumia.

vifurushi vya mizoga na taka zinazotoa harufu zitafungwa kwa njia mbali mbali za kumfanya mpokeaji awe na furaha lakini akifungua apambane na mshtuko ataopata, ndani ya parcel ndiko tutaweka detail za campuni na alietuma kwa code maalumu.


Vifirushi vya mzoga na venye harufu kazi mbaya vitafungwa kiwango ambacho harufu haiwezi toka kamwe.


hivyo natafuta maagent ya biashara hii ikipatikana deal ya percel anatumiwa agent na kupeleka kwa mteja
 
kumbeee, ndio maana mungu kila mtu alimpa akili zake, nilikuwa najiuliza Kama sote ni watoto wake, kwanini agawe akili tofauti, Leo ndio nimepata jibu. thanks GOD
 
Daaah ama kwa hakika binadamu ni kiumbe chenye akili za tofaut sana. Njoo inbox mkuu tulonge kidogo jambo.
 
Back
Top Bottom