Wazo la kufungua Computer learning center

Kila la kheri na ngoja waje kukupa muongozo...
 
Kila la HERI mkubwa ukifika wakati ukihitaji computer niona, nina mzigo wa computer dell AIO,nzuri sana kwa darasa, bado uko majini ziko zaidi ya 14. inbox if you are seriously guy
Unauza kwa moja moja pia mkuu ??
 
Napenda kufungua center itakayokuwa inatoa mafunzo ya computer kwa wanafunzi wanaohitimu elimu ya kidato Cha nne pamoja na wadau wengine

Naomba mwongozo wenu juu ya wazo hili au anaejua changamoto Zake anijuze tafadhari

Nakaribisha mawazo
Kuna center moja niliwahi hudhuria kabla You tube wasap hazijagunduliwa ilikuwa haina watu na mwishowe ilifungwa.Jaribu na wewe labda itauza
 
Mimi nilihudhuria kozi za office 10 - years ago yaani darasa lilikuwa halina wanafunzi na cession zilikuwa tatu au unavyojisikua mwenyewe. ICT sio chaguo la wabongo tangu iingie mpaka leo.
Wengi wanaofanya pc maintainance hawajasoma shule bali mtaani hata hivyo kupata wateja ni mbinu na mkakati hasa kipindi hiki cha ushindani, ajipange.
 
Nenda Kijijini Sehemu ambazo Utapata Wateja Wengi wasiojua Kabisa. Kuliko Kukaa Mijini ambapo Mtu akiwa na Laki 3 anaweza nunua Computer akaweka Ndani watoto wakajifunza
 
Natafuta mfanyakazi wa stationary
Vigezo
Awe binti hajaolewa staki mwanaume
Awe mwaminifu na mchapakazi loss na wizi statain.
Awe tayari kukaa ofisin mpaka saa 3 usiku.
Awe mcha MUNGU
Mshahara wa kuanzia
80,000/=
Kama uko tayari njoo whasp 0689880309
Staki usumbufu Kama huna sifa hata usihangaike
 
Naona wachangiaji wengi Mnamkatisha Tamaa mtoa mada! Mnaongea kitu msichokijua kabisaa! Ushauri wangu kwa Mtoa mada : Wazo lako ni zuri tena fundisha Computer Application yani fundisha Word, excel, powerpoint, Access, Publisher nakuhakikishia utapata Wateja! Mimi nipo Mjini kabisa Naona Center zipo kibao watu wapo hapa hapa Mjini wanafundisha kuanzia mwanzo kabisa kuwasha Computer na kuzima na wanapiga Hela sana tu! Asikutishe Mtu eti watu wanajua kutumia Computer, wengi wanajua tu kuwasha na kuplay movie ila watu wengi Hata Microsoft word inawasumbua sana vitu kama kuandaa Table of contents, kuweka page number, yani hiyo Word tu itakujazia wateja! Sasa ukiongeza na excel ndo kabisaa yani wewe fundisha program za microsoft tu utakuja kuniambia!

Eti watu wanasoma Online nyooo! Wabongo waache kuingia insta aende youtube kusoma Excel? Mtoa mada usitishike! Achana na Graphics na maintanance anza kwanza na akina Microsoft utakuja kunishukuru

Sent from my SM-G531H using JamiiForums mobile app
 
Bro umeshauri vizuri watu hawajui haya mambo wanajiongelea tu
Nashauri uzi uishie hapa maana umemaliza
 
Hiyo ndiyo akili ya mitanganyika iliyomingi. Haijui kitu kwa undani wake lakini inajifanya ni master wa kila jambo. Ukiyataiti kidogo tu yanasepa. MZEE WE ENDELEA NA MIPANGO YAKO CHA MSINGI UWE MBUNIFU KWA HIYO CENTRE YAKO. UNAWEZA KUFUNDISHA PROGRAM MBALIMBALI UTAKAZOONA ZINAFAA KULINGANA NA ENEO ULILOPO NA WAKATI HUO HUO UKAANZISHA WORKSHOP YA KUTENGENEZA PC, PHONES NA ELECTRONI DEVICES NYINGINE, PIA UKAWEKA NA KASTATIONERY N.K CHA MSINGI KULIKO VYOTE IPENDE KAZI UNAYOIFANYA NA KUWA MWAMINIFU HUTOJUTA MAISHANI.
 
Umetisha broooo....ila ww cyo mbongo....maana umenyoosha ukweli
 
Asante brother
 
Hakikisha unapata computer za kibabe siyo utopolo

RAM
PROCESSOR NA
HARD DISK

Viwe vya kibabe siyo utopolo

Kuwa mbunifu
 
Lakini computer ina matumizi yake sahihi. Mimi nilishuhudia chuo kuna watu wana laptop ila hajui kutumia MS office hata kidogo anakwenda stationary kuandikiwa kazi zake.

Computer anaitumia kwa entertainment tu kama kucheki movie na kucheza games.

Kuna umuhimu wa watu kufundishwa matumizi natural ya computer katika shughuli mbali mbali za kibiashara na kijamii.

So usichukulie kuwa anachosema mdau hapo si sahihi. Actually yupo very sahihi sababu anazungumzia kutoa huduma ya kusaidia jamii kupata elimu sahihi ya natumizi ya computer.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…