Fighter23
Member
- Sep 22, 2019
- 41
- 131
Kwa wale wenye mitazamo na ndoto za kufanya biashara ya kuuza vyakula hasa waliopo kwenye miji ya mikubwa ya kibiashara, unaweza pitia wazo hili pengine linaweza kukufaa.
Ni kwamba kwenye miji mikubwa yenye watu wengi, Ni sehemu chache sana ambapo kuna migahawa ambayo mtu anaweza kupata vyakula asilia kama alivyozoea kula kijijini kwao. Kuna watu hutumia muda mrefu kuishi na kukaa kwenye miji hii bila kurudi makwao kutokana na shughuli wanazozofanya hivyo kwa namna moja au nyingine huwa wanakosa sehemu nzuri na nadhifu pa kuweza kupata vyakula vya asili yao vilivyopikwa kama vile wanavyokula wakiwa kwao.
Unaweza kutumia fursa hii kufungua Mgahawa hasa sehemu yenye Garden ukawa na walau nafasi ya kukaa meza 10 au zaidi Kisha ukawa unauza vyakula vyenye asili ya makabila yaliyopo nchini kwetu Tanzania na nchi za jirani. Nakuhakikishia watu wengi wanatamani sana kitu hiki na sehemu nyingi hakuna migahawa wanauza vyakula hivi.
Nawasilisha wazo.
Ni kwamba kwenye miji mikubwa yenye watu wengi, Ni sehemu chache sana ambapo kuna migahawa ambayo mtu anaweza kupata vyakula asilia kama alivyozoea kula kijijini kwao. Kuna watu hutumia muda mrefu kuishi na kukaa kwenye miji hii bila kurudi makwao kutokana na shughuli wanazozofanya hivyo kwa namna moja au nyingine huwa wanakosa sehemu nzuri na nadhifu pa kuweza kupata vyakula vya asili yao vilivyopikwa kama vile wanavyokula wakiwa kwao.
Unaweza kutumia fursa hii kufungua Mgahawa hasa sehemu yenye Garden ukawa na walau nafasi ya kukaa meza 10 au zaidi Kisha ukawa unauza vyakula vyenye asili ya makabila yaliyopo nchini kwetu Tanzania na nchi za jirani. Nakuhakikishia watu wengi wanatamani sana kitu hiki na sehemu nyingi hakuna migahawa wanauza vyakula hivi.
Nawasilisha wazo.