AahaaaaaHoja imeungwa Mkono, bango lipandishwe kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro.
Wanajifanya wamesahau walivyo tusumbu wa na kibegi chao kilichojaa malonyalonya ya Kichina, sasa na bado mpaka waseme.
Tulimkamua mtu, na bado hatukuanzisha mbwembwe kama walizonazo wale washamba wa pale Mafurikoni.
Mlitufunga 5 ipi nyingine kabla ya hii ya juzi? Mdomo mreefu uhalisia 0.Mmesahau tuliwakanda 5 ndani ya dj 45 mkatoa timu uwanjani? Mngekula 10 sikuile.
Hauna rekodi nyingine ya kuifunga Simba magoli 5 zaidi ya hii ya juzi juzi.Kumbe hata historia huijui? Hujui kuwa uliwahi kukimbiza timu uwanjani baada ya kichapo? Bila shaka wewe ni mtoto wa miaka ya 80-90 hapo.
Pia wapeleke Kwenye njia za kutokea miji mikubwa yote TANZANIAJambo hili lisiishe hivi hivi, ni lazima watalii wajue kilicho tokea. Bango la 5G lipelekwe kwenye kilele cha mlima mrefu kuliko yote Africa, pia bango liwekwe kwenye malango yote ya hifadhi za taifa na mbuga za wanyama.
Ni muhimu pia kuweka kwenye international airports, bandari (Boss la DP World atusaidie kupata space) na kwenye stesheni ya treni mwendo kasi.
Hili jambo sio siri, viongozi wa Yanga msitubanie, wekeni mambo hadharani.
Rekodi kutoka kijiwe cha kahawa pro-Max. Hizo huwezi kuzikuta mahala popote.Juni 1 mwaka 1968 mlikula khamsa pale shamba la bibi mkafukuza karibu timu nzima, kabla ya hapo mlikula 5 mkakimbiza timu uwanjani.
Na nyie tengenezeni bango
Rekodi kutoka kijiwe cha kahawa pro-Max. Hizo huwezi kuzikuta mahala popote.
Bado hujasema.........mpaka useme !Tunaziona athari za supu ya vibudu.