Mtoto wa Shule
JF-Expert Member
- Nov 16, 2014
- 15,133
- 11,914
Usishangae hilo. Shangaa chama cha Chadema kinachofikiria kushika dola na kuwaletea maendeleo Watanzania huku chama chenyewe hakina hata ofisi!Alafu tunajengea marais wastaafu mahekalu huku mamilioni ya wanaanchi wa kawaida wanaishi katika lundo la umasikini.
..au tunatumia billion 495 kununua ndege tusizozihitaji.
..fedha hizo zingeweza kujenga vyuo 49 vya ufundi na kubakisha chenji.
Nilikuwa nimeajiri watu 12 kwenye duka la kubadilishia hela. Nikaporwa na biashara kufa.Yaah! Nimefurahi kusikia hivyo ili niendelee kupambana zaidi ili kuitoa nchi yangu kwenye hiyo list.
Naamini Jitihada zangu ndo zitafanya maisha yangu kuwa mazuri au mabaya hayo mengine yaliyobaki Niya watu wazembe na watu wa kulia lia.
Usitake kupinga mtazamo Wangu kwa kuleta hoja za propaganda hapa.Nilikuwa nimeajiri watu 12 kwenye duka la kubadilishia hela. Nikaporwa na biashara kufa.
Kule kusini,kwenye korosho,niliajiri Watanzania 177. Biashara imekufa kwa kuingiliwa na watu waishio Dodoma wasiojua "a" wala "b" ya korosho.
Uwakala wangu wa vinywaji uliajiri watu 32. Leo hii kutokana na nguvu ya manunuzi ya Watanzania kupungua sana,nimebakisha wafanyajazi 14 tu.
TADB wameninyima mkopo ambao ungeajiri Watanzania 262 kwenye hekari 1800.
Hapo bado unaamini bila serikali kukuwekea mazingira mazuri,jitihada zako pekee zitafanya "utoboe"!?
Usifikiri kila mtu anafanya ufanyacho jamaa.Usitake kupinga mtazamo Wangu kwa kuleta hoja za propaganda hapa.
Hapo 99% ulichoandika ni propaganda tu.
Jamani nyie mnaotmebeq huku na kule,,givi maisha ya kawaida ya Mtanzania ukilinganisha na ya Mganda,Rwanda,Zambia, Malawi, Msumbiji..wapi kunaunafuu wa umasikini?
Maono ya mzee Mkapa binafsi nimeyaheshimu sana. Kila ukisoma reforms alizozifanya na malengo yake unagundua alikuwa na maana bora sana kwa nchi.Hii hutasikia Akina Polepole wanasema. Unfortunately hata waandishi wetu wa Habari hawatauliza... Ila kwenye mideal income kelele zake haziishi. Hawajui hata Zambia na Zimbabwe waliingia huko Siku nyingi. Ndiyo maana Mkapa (RIP) alitaka $3000.