WCB mfumo wa uongozi mikataba n.k

WCB mfumo wa uongozi mikataba n.k

Kabisa hii ingemuondolea Babu tale lawama kama anataka watu wake angewaweka kirahisi sana unasubiri mkataba ukiisha tu unakataa kurenew sasa hii mikataba ya muongo mmoja ni shida. Kampuni nyingi huwa zinaopt mkataba wa mwaka mmoja au miwili hapo kila mtu anakuwa na nidhamu maana ukizingua tu nasubiri kwenye kurenew mkataba.
Maana kuongoza watu kwenye tasnia ya burudani ni shida maana wengi hawajui ethics za kazi na ndio maana mtu akiondoka sehemu anaondoka na maneno mengi sijui kule hali ilikuwa vile wakati tasnia ya burudani ni ajira kama zilivyo ajira nyingine ambapo ukipigwa chini unaondoka kimya kimya tena ukiomba kazi sehemu nyingine wala huzungumzi mabaya ya mwajiri wako..kuepusha shari kuna watu kama kina Kifesi kwa nafasi zao unawapa mkataba wa miaka michache michache ili kama wakizingua unawabwaga
 
Sijawahi kuona wala kusikia mkataba wa miaka miwili let alone mwaka mmoja kwenye tasnia ya burudani! Mkataba mfupi kabisa utakaopata ni miaka 5.

Kwenye muziki; hiyo miaka 2 si ya kuandaa album moja tu hiyo!! Na kama wanamuziki wenyewe unawachukua chini kabisa (underground) kama ilivyokuwa akina Harmonize; hiyo miaka 2 ni ya kum-brand tu!!

Kwamba wakivunja mkataba wataishia kupelekana mahakamani; of course, ni very possible especially kama Msanii alifanikiwa sana au alipoteza sana!

Kwa wasanii underground; chukulia mtu kama Lavalava, anaweza kupata mkataba unaosema; ikiwa atauvunja ndani ya miaka 3; basi atailipa label, mathalani 20M kwa sababu unaamini ndani ya huo muda atakuwa hajatusua vya kutosha!

Lakini unaweza kukuta kwa mwaka wa kwanza ule ule anatusua kupita maelezo kiasi kwamba; hata 100M kwake ni pesa ya kawaida!

Wakati hata 100M kwake ni pesa ya kawaida; unakuta ndo anataka kuvunja mkataba kwa 20M wakati mnaamini hapo alipofika ni kwa ajili ya label huku pia mkiona potential kubwa iliyopo sentimita chache tu mbele yake!

Katika mazingira kama hayo, lazima zengwe litokee!

Na hiyo ndiyo sababu pia ni kwanini hawatoi (sio WCB tu) mikataba mifupi!

Mtu unaweza kumpa mkataba wa mwaka mmoja huku ukitarajia ata-renew! Lakini ndani ya mwaka huo huo anatusua vibaya mno huku akiwa na option ya ku-renew au kutofanya hivyo!!

Je, asipo-renew utakuwa uf.ala wa nani?!

NB: Duniani kote, mikataba kwenye tasnia ya burudani ni jipu, hasa kwa artists wasio na majina!
Haijawahi tokea kwa sababu hawataki kufanya hivyo na sababu ya kutokufanya hivyo nimeeleza pale juu kama nawewe ulivyoieleza ni hofu upande wa lebo kwamba watakimbiwa na msanii.

Lakini tukija kwa upande mwingine mikataba mifupi ina manufaa makubwa kwa msanii leave along hiyo miwili au mmoja itaonekana michache basi kwanini isiwe minne au mitatu kwani albamu haikamiliki kwa muda wa miaka mitatu?

Ila Mavoko ameingia mwaka 2016 leo unataka kutoka angekuwa na mkataba wa miaka mitatu ungekuwa unaisha mwakani ni rahisi kuvumilia
 
Haijawahi tokea kwa sababu hawataki kufanya hivyo na sababu ya kutokufanya hivyo nimeeleza pale juu kama nawewe ulivyoieleza ni hofu upande wa lebo kwamba watakimbiwa na msanii.

Lakini tukija kwa upande mwingine mikataba mifupi ina manufaa makubwa kwa msanii leave along hiyo miwili au mmoja itaonekana michache basi kwanini isiwe minne au mitatu kwani albamu haikamiliki kwa muda wa miaka mitatu?

Ila Mavoko ameingia mwaka 2016 leo unataka kutoka angekuwa na mkataba wa miaka mitatu ungekuwa unaisha mwakani ni rahisi kuvumilia
Tukitumia neno "wanahofu watakimbiwa na wasanii....!" nadhani hiyo phrase sio sahii sana kwa sababu it sounds too personal wakati ukweli ni kwamba, it's all about business... na hiyo no popote pale utakapoenda!

Na popote utakapoenda, mikataba yao ni ya muda mrefu unless kama Msanii ni mkubwa mno compared na Lebo! Leo hii Pozi kwa Pozi Entertainment inaweza kukubali kumsaini Diamond hata kwa miezi 6 kwa sababu PKP inamuhitaji zaidi Diamond kuliko Diamond anavyoihitaji PKP!

Anyway, nimeeleza mengi kwenye post ya kwanza, sioni sababu ya kurudia tena hapa labda niende moja kwa moja kwa issue ya Rich Mavoko!

Kama Rich Mavoko alisaini mkataba wa hovyo katu siwezi kuwalaumu WCB! Mavoko ni mkongwe kwenye game!! Mavoko anazifahamu fika fitina za tasnia ya burudani, au angalau tasnia ya muziki! Mavoko alishawahi kuwa hadi kwenye management ya nje ya nchi! Maelezo yote hayo yanathibitisha jambo moja tu: Rich Mavoko ni mzoefu wa haya mambo!

Sasa ikiwa pamoja na yote hayo, kwanini basi alisaini mkataba wa hovyo?
1. Labda ni mpumbavu!! Sio mjinga bali ni mpumbavu kwa sababu mjinga ni yule asiyejua! Kwanini alisaini mkataba wa hovyo wakati yeye ni mzoefu wa haya mambo? Alilazimishwa? Jibu HAPANA, so WHY? Because--

2. Huenda Mavoko alifahamu fika kwamba mkataba ni wa hovyo lakini alitaka kuitumia WCB kumrudisha kwenye game! Hata kama kuna baadhi ya watu wanaodai WCB ilikuwa inampoteza Mavoko lakini ukweli ni kwamba Mavoko alienda WCB wakati ameshaanza kupotea kwenye game!

Hivyo basi, inawezekana kabisa alifahamu mkataba haukuwa mzuri lakini akaamua tu kusaini huku akitegemea, akisharudi tu kwenye chati, basi anatafuta way out!!!

Smart, right?! Yes or no!

Atakuwa amecheza smart endapo tu wakati anasaini tayari alishaona loophole kwenye mkataba vinginevyo, it's nice try lakini kachemka! Kachemka kwa sababu BASATA hawawezi kumsaidia kwenye mkataba usio na kasoro! Hata kama alisaini miaka 50 huo mkataba huwezi kuita una kasoro UNLESS kama kuna sheria ya nchi inayosema mkataba kati ya msanii na lebo hautakiwi kuzidi miaka xyz!

Au, BASATA wanaweza kumsaidia Mavoko ikiwa WCB wamekiuka terms za mkataba na mkataba una kipengele cha "free way out" ikiwa lebo imekiuka terms fulani fulani!

But for what I know, napata shaka ikiwa WCB wanaweza kutoa mkataba wenye kasoro... those guys hawakwenda shule but wana smart people nyuma yao!!!!!

Lakini kwa upande mwingine, kwa umaarufu wa Mavoko, hata kama alishaanza kupotea bado alikuwa na uwezo wa ama ku-negotiate better terms au hata kukataa!!!

Lakini kwanini mambo kama haya yanatokea sana?!

Nishawahi kusema mara kadhaa hapa kwamba, Tanzania tuna Wanasheria lakini hatuna Wanasheria wa Burudani; yaani Entertainment Lawyers. Anyway, hilo la Entertainment Lawyers lipo juu ya uwezo wetu lakini angalau tungekuwa na Wanasheria wanaoifahamu vyema tasnia ya burudani!!! Narudia, kuifahamu tasnia ya muziki na sio kuufahamu muziki!

Hii tasnia (ya burudani) ingawaje watu wanaichukulia poa lakini ipo very complex!!

Leo hii unaweza kusaini mkataba kwa sababu tu umeangalia basic benefits bila kufahamu kuna benefits zingine kadhaa ambazo kwa level uliyokuwa nayo, huwezi kuziona kwa sababu zinaibuka kadri unavyozidi kuwa mkubwa!!

Kwa mfano, ikiwa mkataba kati ya Harmonize na WCB umeangalia tu mapato yanayotokana na shows, streaming, digital and cd sales na endorsement! Halafu leo hii, WCB wanaamua ku-print TShirt za KWANGWARU halafu zinauzika ile mbaya!

Now tell me, wewe Harmonize unaenda kudai share ya mauzo ya tshirts kwa kutumia grounds zipi ikiwa mkataba wako hausemi chochote kuhusu hilo, whether directly or indirectly? Mbaya zaidi (na mara nyingi inakuwa hivyo), unaweza kukuta nyimbo zako ni mali ya lebo... refer Saida Karoli vs FM Studio (Mzee Mutta)!!

Halafu hizi lebo hizi' we acha tu! Zina invisible costs kibao ambazo baadae zinageuka kuwa kitanzi kwa msanii!!! Na hizi costs lebo wanaziingiza makusudi ili "balance sheet" ya msanii always iegemee upande wa debit!!!

Hata hivyo, kwa Mavoko sitarajii kama hazifahamu janja janja kama hizi unless kama ni stupid!!!!
 
Ripoti: Mfumo wa uongozi WCB, mikataba ya wasanii pamoja na wanaomiliki hisa nyingi za kampuni


WCB ni moja kati ya label kubwa za muziki nchini Tanzania yenye mafanikio zaidi kutokana na ukubwa wa wasanii wake pamoja na uwekezaji walioufanya kwenye tasnia ya muziki wa BongoFleva.


Label hiyo inaongozwa na rais wa label hiyo ambaye pia ni msanii, Diamond Platnumz akishirikiana na Manangers,Sallam aka Mendez, Said Fella maarufu kama Mkubwa Fella pamoja na Hamisi Taletale aka Babu Tale.

Ukiachana na viongozi hao watatu pia kuna mameneja wengine wadogo wadogo ambao wana majukumu ya kuwasimamia wasanii waliosainiwa na label hiyo, ambao ni Ricardo Momo, Makame pamoja Sandra.

Label hiyo ina wasanii sita, Queen Darleen, Harmonize, Lava Lava, Mbosso, Diamond Platnumz pamoja Rich Mavoko ambaye amekua yupo kimya kwa muda mrefu huku akihusishwa na kutaka kuachana na label hiyo.

Diamond ni nani WCB na wanahisa wengine wa label hiyo.

Diamond Platnumz ndio kila kitu ndani ya WCB, ni Mkurugenzi Mkuu na ndio mwenye hisa nyingi ndani ya kampuni hiyo, hivyo basi ndio mwenye kauli ya mwisho katika maamuzi. Wakurungezi wengine wenye hisa ni pamoja na Sallam, Mkubwa Fella, Babu Tale pamoja na Mama Diamond ambao wanatambuliwa na memorandum ya kampuni hiyo.

Diamond Platnumz

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha uhakika kimedai, Mama Diamond yupo kwenye kampuni hiyo kama mkurugenzi huru ambaye ana jukumu la kuangalia kampuni inaendaje pamoja na kutoa ushauri katika baadhi ya mambo.

Kampuni ya WCB yenye makazi yake Mbezi jijini Dar es salaam, kwa sasa inamiliki Wasafi TV, Wasafi Redio,Wasafi.com, Wasafi Records Music Studio, Chibu Perfume pamoja na Diamond Karanga.

Mwaka mmoja uliopita wakati anatambulishwa Mbosso, Fella alitoa kauli ya kumtaka rais wa label hiyo Diamond Platnumz kuongeza kamisheni kwa mameneja hao kutokana na kazi kubwa wanazifanya.

“Kwa mara ya kwanza Diamond ameleta mapindunzi kwenye muziki kwa mameneja kulipwa. Wasanii wengine sisi ndio tunatoa hela, lakini huyu sisi anatulipa, Sallam analipwa japokuwa anauza magari, mimi diwani nalipwa na Diamond, Tale ana ishu zake nyingine lakini analipwa na huyu, na kuna deal nyingine inakuja tutakaa nusu kwa nusu,” alisema Mkubwa Fella

Fella aliwahi kunukuliwa na chombo kimoja cha habari nchini Tanzania akisema kwamba katika kila mapato ya Diamond ya mwezi mmoja, asilimia 30 inaenda kwa mameneja wake hao watatu. Yaani kama Diamond akiingiza milioni 100 kwa mwezi basi milioni 30 zinaenda kwa mameneja wake.

Fella ana jukumu gani WCB?.
Mkubwa Fella ni mmoja kati ya wakurugenzi wa WCB, lakini pia ana simama kama mmoja kati ya mameneja watatu wa Diamond Platnumz.

Mkubwa Fella

“Mimi ni mmoja kati ya wakurungezi wa WCB lakini pia ni meneja wa Diamond, na kama unavyojua kazi ya mkurungezi wa kampuni ni kuhakikisha kampuni inaenda mbele na inaendelea kukua. Pia kusimamia utendaji mzima wa WCB, kuwaangalia wasanii wetu pamoja na mameneja wao,” Fella aliiambia Bongo5.

Pia Fella ni mzee wa busara ndani ya label hiyo, na mara nyingi ndiye mtu ambaye ana zima moto kama kuna jambo limetokea ndani ya kampuni hiyo. Yeye hufanya hivyo hata nje ya kampuni kama kuna suala ambalo limeleta taharuki huwa anaweka mambo sawa kwani sio mtu wakupaniki na kukurupuka.

Sallam SK ana majukumu gani WCB?.
Sallam aka Mendez ni mmoja kati ya Wakurungezi wa WCB ambaye pia ni meneja wa Diamond wa Kimataifa. Meneja huyo amekuwa akionekana sana katika kumtafutia deals Diamond, shows za nje pamoja na kuingia mikataba na makampuni mbalimbali ya muziki duniani kwa ajili ya kuipeleka kimataifa brand ya WCB.

Sallam SK

Kifesi ambaye alikuwa mpiga picha wa Diamond na WCB, aliiambia Bongo5 kwamba Sallam ni kiongozi wa kampuni hiyo ambaye amechukua jukumu kubwa la kulinda brand pamoja na kuhakikisha kazi za kampuni hiyo zinaenda kama zilivyopangwa.

Babu Tale ana majukumu gani WCB?
Huyu ni Master in Street Management kama anavyojiita mwenyewe. Babu Tale ndiye mwenye kitengo cha lawama WCB lakini ni mlezi wa wasanii pamoja na WCB nzima. Mara nyingi amekuwa mtatuzi wa shida nyingi za wafanyakazi wake lakini ni mtu mwenye maamuzi ya hapo hapo akiona kuna tatizo au kuna mtu analeta shida ndio maana hata baadhi ya wafanyakazi wanaotoka WCB mara nyingi wanamtupia lawama.

Babu Tale

Tale ndiye aliyekabidhiwa kitengo cha lawama kama nilivyozungumza hapo awali, unakumbuka alivyojilipua kwa kauli yake ya kutaka ngoma zao zisipigwe katika vituo vya redio na TV, nani ungeweza kujilipua na kutamba kama alivyofanya Babu Tele?.

Wiki hii aliyekuwa mfanyakazi wa Social Media WCB, Almasi Zambele alidai alitimuliwa WCB na Tale kwa madai bosi huyo alikuwa anahitaji kuweka watu wake wapya. Kama nilivyosema hapo awali, Tale ni mkurugenzi, hawezi kubali mtu achafue brand ya WCB ndio maana hata wakati mwingine analaumiwa lakini kiukweli anatekeleza wajibu wake.

Mikataba ya Wasanii wa WCB

Kama unavyojua WCB ni label kubwa nchini Tanzania, Afrika Mashariki pamoja na Afrika kwa sasa, kwa uchunguzi tulioufanya tumegundua wasanii wengi wana mikataba ya muda mrefu tena yenye vipengele ambavyo ukitaka kusaliti kambi lazima ujiulize mara mbili mbili. Lakini wachache wanadaiwa hawana mikataba akiwemo Queen Darleen ambaye ni dada wa Diamond Platnumz.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya WCB, Harmonize na Rich Mavoko wanadaiwa kuwa na mkataba wa miaka 10 na WCB na mtu ambaye atataka kuvunja mkataba atatakiwa kulipa fidia isiyo chini ya tsh milioni 10. Lakini mikataba yao inaweza kubadilika muda wowote kutokana na mafanikio ya wasanii hao. Mikataba ya wasanii wengine imekuwa ni siri kubwa lakini nadhani umepata picha kwamba WCB ni label ya namna gani mpaka sasa.

Wasanii hao wanaingiza pesa kupitia shows na ishu za matangazo, ambapo kampuni huchukua asilimia kadhaa na pesa nyingine huwenda kwa msanii. Pia ishu za production zimebaki kwa WCB, kuanzia video mpaka audio.

Diamond aliwahi kunukuliwa na vyombo vya habari kwamba kuna baadhi ya wasanii kama Harmonize alitumia zaidi ya tsh milioni 100 kwaajili ya kuandaa kazi zake pamoja na kutengeza brand yake.

Hii imetupa picha kwamba WCB sio label ya kawaida, ni lavel za kimatifa, wasanii na wadau wa sanaa wanatakiwa kuanza kutengeza mazingira ya brand za wasanii kama walivyofanya WCB.

Bongo5 tunawapongeza sana WCB kwa mambo makubwa wanayoyafanya, uwekezaji walioufanya kwenye muziki pamoja na kutengeneza sura mpya ndani ya industry ya burudani na muziki wa BongoFleva Tanzania, Afrika Mashariki pamoja na Afrika.

Toa maon yako

Naona babu tale n kama hua anafkiria
Kwa kutumia makalio huyu mzee

Sources bongo 5:
Hata kama ukitudanganya sisi tutajuaje?
By the way, si hadithi tamu
 
Huyu jamaa ninachomshauri akomae mwenyewe, tunaweza tukawalaumu WCB, wakati yy mwenyewe mavoko ana matatizo, kwa nini nasema hivyo?

Jamaa kaanza kuwa managed na Papaa Misifa, mpaka Papaa akampeleka mahakamani kwa kukiuka mkataba na akataka alipwe mil 50, sijui walimalizana vipi. Baadaye kakimbilia Kenya kwenye label ya King Kaka ya Rabbit wakazinguana na King kaka akavunja mkataba now ni WCB nao kazinguana nao, japo hatujauona mkataba lkn mavoko bado namuona ana matatizo.

Alafu maswala haya ya mara nyingi mikataba yake ni ya muda mrefu, Kanye kazinguana na Jay Z lkn bado yupo chini ya Roc Nation, Lil Wayne pamoja na kazinguana na birdman bado yupo chini ya Cash money na hawa wote wapo ktk label zao zaidi ya miaka 10, njoo kwa nick minaj na Drake wana miaka zaidi ya 9 ktk label ya young money, njoo kwa kendrick lamar, yupo chini ya Dr dree zaidi ya miaka 5.

Wanafanya hivi sababu label wanawekeza hela ndefu sana na ndio maana wanafanya mikataba ya mda mrefu ili hela yao irudi.Ila kwa wenzetu ulaya mkataba unabainisha kama labda label itasimamia distribution ya nyimbo online, kwenye maredio pamoja na promotion, ring tones nk au vyote kwa pamoja lkn msanii kama akiwa na ishu zake kama yy mwenyewe kuwa na label au kuwa na biashara yake ambayo haikubainishwa ktk mkataba basi hela yote ni ya msanii sasa sijajua mkataba wa mavoko unasemaje.

Ila WCB naona kama wamemfanyia favor kwani Baraka da prince, kiss Daniel, wizkid hawa walinyang'anywa mpaka acc zao za YouTube baada ya kuvunja mkataba na label zao. Ila naona muda umefika kwa wasanii kuwa na wanasheria wao na wao wenyewe waiheshimu mikataba ila nimesikia mkataba umepelekwa wizara ya michezo kwa kuangaliwa zaidi, sasa ngoja tusubiri.
 
Tukitumia neno "wanahofu watakimbiwa na wasanii....!" nadhani hiyo phrase sio sahii sana kwa sababu it sounds too personal wakati ukweli ni kwamba, it's all about business... na hiyo no popote pale utakapoenda!

Na popote utakapoenda, mikataba yao ni ya muda mrefu unless kama Msanii ni mkubwa mno compared na Lebo! Leo hii Pozi kwa Pozi Entertainment inaweza kukubali kumsaini Diamond hata kwa miezi 6 kwa sababu PKP inamuhitaji zaidi Diamond kuliko Diamond anavyoihitaji PKP!

Anyway, nimeeleza mengi kwenye post ya kwanza, sioni sababu ya kurudia tena hapa labda niende moja kwa moja kwa issue ya Rich Mavoko!

Kama Rich Mavoko alisaini mkataba wa hovyo katu siwezi kuwalaumu WCB! Mavoko ni mkongwe kwenye game!! Mavoko anazifahamu fika fitina za tasnia ya burudani, au angalau tasnia ya muziki! Mavoko alishawahi kuwa hadi kwenye management ya nje ya nchi! Maelezo yote hayo yanathibitisha jambo moja tu: Rich Mavoko ni mzoefu wa haya mambo!

Sasa ikiwa pamoja na yote hayo, kwanini basi alisaini mkataba wa hovyo?
1. Labda ni mpumbavu!! Sio mjinga bali ni mpumbavu kwa sababu mjinga ni yule asiyejua! Kwanini alisaini mkataba wa hovyo wakati yeye ni mzoefu wa haya mambo? Alilazimishwa? Jibu HAPANA, so WHY? Because--

2. Huenda Mavoko alifahamu fika kwamba mkataba ni wa hovyo lakini alitaka kuitumia WCB kumrudisha kwenye game! Hata kama kuna baadhi ya watu wanaodai WCB ilikuwa inampoteza Mavoko lakini ukweli ni kwamba Mavoko alienda WCB wakati ameshaanza kupotea kwenye game!

Hivyo basi, inawezekana kabisa alifahamu mkataba haukuwa mzuri lakini akaamua tu kusaini huku akitegemea, akisharudi tu kwenye chati, basi anatafuta way out!!!

Smart, right?! Yes or no!

Atakuwa amecheza smart endapo tu wakati anasaini tayari alishaona loophole kwenye mkataba vinginevyo, it's nice try lakini kachemka! Kachemka kwa sababu BASATA hawawezi kumsaidia kwenye mkataba usio na kasoro! Hata kama alisaini miaka 50 huo mkataba huwezi kuita una kasoro UNLESS kama kuna sheria ya nchi inayosema mkataba kati ya msanii na lebo hautakiwi kuzidi miaka xyz!

Au, BASATA wanaweza kumsaidia Mavoko ikiwa WCB wamekiuka terms za mkataba na mkataba una kipengele cha "free way out" ikiwa lebo imekiuka terms fulani fulani!

But for what I know, napata shaka ikiwa WCB wanaweza kutoa mkataba wenye kasoro... those guys hawakwenda shule but wana smart people nyuma yao!!!!!

Lakini kwa upande mwingine, kwa umaarufu wa Mavoko, hata kama alishaanza kupotea bado alikuwa na uwezo wa ama ku-negotiate better terms au hata kukataa!!!

Lakini kwanini mambo kama haya yanatokea sana?!

Nishawahi kusema mara kadhaa hapa kwamba, Tanzania tuna Wanasheria lakini hatuna Wanasheria wa Burudani; yaani Entertainment Lawyers. Anyway, hilo la Entertainment Lawyers lipo juu ya uwezo wetu lakini angalau tungekuwa na Wanasheria wanaoifahamu vyema tasnia ya burudani!!! Narudia, kuifahamu tasnia ya muziki na sio kuufahamu muziki!

Hii tasnia (ya burudani) ingawaje watu wanaichukulia poa lakini ipo very complex!!

Leo hii unaweza kusaini mkataba kwa sababu tu umeangalia basic benefits bila kufahamu kuna benefits zingine kadhaa ambazo kwa level uliyokuwa nayo, huwezi kuziona kwa sababu zinaibuka kadri unavyozidi kuwa mkubwa!!

Kwa mfano, ikiwa mkataba kati ya Harmonize na WCB umeangalia tu mapato yanayotokana na shows, streaming, digital and cd sales na endorsement! Halafu leo hii, WCB wanaamua ku-print TShirt za KWANGWARU halafu zinauzika ile mbaya!

Now tell me, wewe Harmonize unaenda kudai share ya mauzo ya tshirts kwa kutumia grounds zipi ikiwa mkataba wako hausemi chochote kuhusu hilo, whether directly or indirectly? Mbaya zaidi (na mara nyingi inakuwa hivyo), unaweza kukuta nyimbo zako ni mali ya lebo... refer Saida Karoli vs FM Studio (Mzee Mutta)!!

Halafu hizi lebo hizi' we acha tu! Zina invisible costs kibao ambazo baadae zinageuka kuwa kitanzi kwa msanii!!! Na hizi costs lebo wanaziingiza makusudi ili "balance sheet" ya msanii always iegemee upande wa debit!!!

Hata hivyo, kwa Mavoko sitarajii kama hazifahamu janja janja kama hizi unless kama ni stupid!!!!
Mkuu mimi sitofautiani na wewe naona Mavoko hakuwa makini kusaini mkataba wa aina hiyo. Kwa sababu sioni sababu ya msanii ambaye alikuwa ameshatoka kama Mavoko kuingia mkataba wa muda mrefu hivyo. Angalau basi ingekuwa miaka miwili, mitatu au minne hiyo inatosha kwa msanii ambaye hahitaji nguvu nyingi kumtoa.

Kwa harmonize kwa kuwa alikuwa hajatoka kimuziki nadhani kwake mkataba wa miaka mitano au Sita ungetosha sana. Lakini mkataba miaka 10 kama leseni ya kitalu cha madini siyo reasonable kwa dunia ya sasa aisee! Muongo mzima?

Pia ameenda serikalini sijui BASATA nadhani anaogopa kwenda mahakamani maana utakuta hata cause of action hana. Wanasheria watakuwa wamekaa naye wakaona njia ya kumsaidia ndiyo hiyo. Huwezi ukaenda mahakamani eti ukadai mkataba halali uliofuata sheria na utaratibu zote eti "ni wa kinyonyaji"? How?

Kwenye sheria za mikataba tunasema consideration need not to be adequate but sufficient. Haijalishi hata kama gari la milioni 100 ukaliuza kwa milioni 10 kwa kuwa umekubali kwa hiyari yako hiyo anaitwa sufficient consideration japokuwa siyo adequate na hiyo haifanyi makubaliano yenu kuwa batili unless sasa kuna vitiating factors zingine zimekufanya uaccept terms hizo.

Kama ni mahakamani atatakiwa awe na cause of action ya kueleweka na siyo eti " wa kinyonyaji" hizo ni hoja za kisiasa. Kama nawaona wazee wa matamko hapo hata Mr Kangi atatamani atie neno ili mradi tu matamko.
 
Hili ni tatizo kubwa tulilonalo wa africa wengi, tukiajiriwa tunashindwa kuweka nidhamu katika kazi badala yake tunatamani kuwa wale waliotuajiri, mfano umeajiriwa na kampuni ya ujenzi kama foreman, badala ya kuweka nguvu yako kwenye kazi wewe unawaza kuwa kama mmiliki wa kampuni, Mfano Mavoco kabla ya kuingia WCB hakuwa na wazo kama anaweza kuwa kama Diamond, kaingia huko anataka awe kama Diamond, na akishamalizana na WCB akawa na kazi zake mtaona kama atakua na mafanikio yoyote
 
Back
Top Bottom