Uchaguzi 2020 We need a President who will restore Law, Order and Constitutional Rights

Uchaguzi 2020 We need a President who will restore Law, Order and Constitutional Rights

Ni wazi tuko transitional period ya kuelekea chama kimmoja. Sioni kama miaka mitano ijayo serikali hii ya CCM kama itakuwa na muda wa law and order wala kufufua katiba ya Warioba.
Kwa sababu lengo lao ni njia ya kufanana na Russia ya Putin au kulingana na sera za Maduro wa Venezuela.
Pammoja na serikali kutoka njia kuu ya utawala tuliouzoea tokea Mzee Ruksa, Mkapa na Kikwete,kosa kubwa ni chama kutozingatia utu na upendo kwa wananchi wake.
Wanapochagua viongozi wao waache busara zitawale vichwa vyao.Siyo muda wa kupandisha mizuka kama Lugola au Kessy.
Wanaoweza kuifanya nchi ikawa ya chama kimoja ni China na Russia, nchi zenye nguvu za kiuchumi. Tanzania ikithubutu kufanya hivyo inageuka kuwa Zimbabwe ndani ya miezi mitatu.
 
Unawakilisha maoni ya wananchi walio wengi! Lakini hapo mwisho pia umeonyesha uoga wa wananchi walio wengi. Jambo ambalo siyo zuri hata kidogo kwenye Taifa huru lenye kufuata katiba na haki za wananchi wake.
Kuna moja tu hakuna binadamu atakaye kukufanyia mapenzi ya Magufuli kuna ubaya wake na ukweli wake.

Walahii naapa hakuna .
Naongea ukweli eti siongei uongoo.
 
Wanajamvi,

Mara zote mataifa ya wenzetu, hata yale wafadhili mfano wachina na wamarekani, huwa wanatafuta rais ambaye yuko vizuri kwenye hitaji lao kuu la Taifa ambalo wananchi walio wengi wanakubaliana na lengo hilo na hivyo kumtafuta, na kumpata kiongozi atakayewafikisha kwenye malengo yao hayo ya kitaifa.

Ni kweli tunahitaji sana viwanda ili tuweze kuwa na uchumi wa kati. Sera ambayo Rais aliyepo, ndugu Maghufuli, aliinadi kwa kupitia chama chake ccm. Hadi sasa hivi sioni tukielekea huko. Hata hivyo, lengo kama sikosei ni kuwa Taifa lenye uchumi wa kati ifikapo 2025! Miaka chini ya sita kutoka sasa! Kiuhalisia, sidhani hata kama tumeshaweka hata misingi ya kuelekea huko.

Kwa hali ilivyo ambapo ni vigumu kuhoji na hata kupata ripoti sahihi za wapi tumefikia kwenye agenda yetu hiyo, ukiuliza ama kuhoji, basi unaweza kuitwa msaliti au siyo mzalendo, unayeshirikiana na mebeberu nk.

Lakini wananchi walio wengi, malalamiko yaliyopo ni kuhusu ukiukwaji wa wazi wazi kabisa wa katiba na sheria za nchi pamoja na haki zinazowalinda wananchi!

Hakuna kipindi ambacho watanzania wamelilia utawala wa kisheria na mara nyingi katiba mpya kama ilivyo sasa! Sababu kubwa haswa ni kuminywa kwa uhuru wao, na pia kujichagulia viongozi wanaowataka...hata tume huru ya uchaguzi, ni kilio kinachoambatana na madai hayo ya wananchi walio wengi! Matamanio hayo, yanaweza kuwafanya wakataka kuwa na rais ambaye atarudisha utawala wa katiba, haki na sheria, kuwa nguzo kuu inapokuja kwenye uongozi wa Taifa letu pendwa!

...Kwamba anaweza kusimamia tukapata katiba ya kutoka kwa wananchi kwa ajili ya wananchi na siyo katiba ya mtu mmoja ambaye anakuwa hahojiwi lolote mahali popote na yoyote yule! Ni kama Mungu mtu kabisa!

Kiongozi ambaye atasikiliza vilio vya wananchi kuhusu utawala unaofuata sheria na katiba, pamoja na matamanio ya kupata tume huru ya uchaguzi.

Hata mikataba mingi tunaingia hovyo hovyo na kuivunja hovyo hovyo, imesababishwa na hayo! Hakuna mfumo wa accountability ama uwajibikaji! jambo ambalo limetusababishia hasara kubwa chini ya tawala za ccm haswa uongozi huu uliopo.

Kuiweka kando kwanza idea ya viwanda, si wazo la busara, tujipange, wenzetu ndivyo walivyofanya wenzetu, na si vurugu mechi!

Ni muhimu ili nchi inyooshwe inavyotakiwa, ili tuweze kupata viongozi ambao watawajibika kwa wananchi waliomchaguwa na si vinginevyo!

Kwa namna ambavyo ccm imetuingiza ama imeliingizia Taifa hasara kubwa na hivyo kuendelea kuwa masikini, ni wazi kwamba ufisadi mkubwa uliokubuhu, chanzo chake ni mazoea ya kutokuwa watu wenye kufuata sheria za nchi kwasababu ya katiba mbovu inayomlinda mwenyekiti wa chama cha mafisadi ambapo anatokea kuwa na majukumu ya kuongoza wananchi wake wote bila ubaguzi wowote hata ule wa vyama! Lakini hali iliyopo ni ya tofauti kabisa! Ubaguzi na upendeleo kwa baadhi ya wananchi kulingana na mitazamo ya kisiasa ni kinyume cha katiba ya nchi!

Endapo “law, order and constitutional rights”, itakuwa ndiyo one of the main agendas za Taifa na wananchi walio wengi kwenye uchaguzi ujao, basi honorary Lissu “is a good fit”


“In matters of truth and justice, there is no difference between large and small problems, for issues concerning the treatment of people are all the same”.

Albert Einstein
non but anyone from Opposition
 
Wanaoweza kuifanya nchi ikawa ya chama kimoja ni China na Russia, nchi zenye nguvu za kiuchumi. Tanzania ikithubutu kufanya hivyo inageuka kuwa Zimbabwe ndani ya miezi mitatu.
Already tupo practically one party,and theoretically multiparty kwa miaka 4 sasa.
Zamani tulikuwa hivyo zaidi miaka 20 ikiwa single socialist party.
 
Sijakuelewa.
Wewe hupendi chichim ndio maana huelewi .
Ukweli ni huu John Joseph Pombe Magufuli .
Ni mtu wa kipekee . Moyo wake ni wawatu kwanini kasaidia wanyonge.
Mtu maskini kanyimwa haki yake miaka 30 halafu magufuli akaja kumsaidia apate haki.
Sijawahi ona mtu anatatua shida ya mmoja mmoja .
Kuna mabaya yake na mazuri yake .
Na mabaya ni hataki kuzoewa vibaya basi.
 
Back
Top Bottom