Weka dirisha la dharura kwenye nyumba yako, nyumba siyo gereza

Weka dirisha la dharura kwenye nyumba yako, nyumba siyo gereza

robbyr

Senior Member
Joined
Apr 8, 2017
Posts
129
Reaction score
221
e60283b2174d20e737ee0809bb5c9f06.jpg

Image source: Pinterest

Nyumba si gereza. Kutokana na mfumo wa ujenzi wa sasa ambapo tunaweka chuma kila dirisha na baadae tunavisha madirisha ya vioo (Aliminium) ni mihumu kuweka dirisha la dharura ambalo halitakuwa na chuma au likiwa na chuma ziwe ni slide pia.

Naandika andiko hili baada ya kupitia miezi kadhaa nikishuhudia nyumba ikiungua moto na ndani kulikuwa na mtu.

Mungu ni mwema kwani alikimbia chooni na waungwana walijitahidi kuvunja dirisha ambapo mmoja aliingia na kumtoa ingalia alikuwa amesharizai.

Naamini wewe ni shahidi wa habari hizi. Nahisi kuwepo kwa existing window tofauti na mlango kwenye baadhi ya vyumba au chooni kunaweza kusaidia katika uokoaji wakati wa janga la moto.

Narudia nyumba si gereza lazima tahadhari za usalama zizingatiwe.

Pia, wale wenzangu ambao jiko lipo ndani ni muhimu kuweka mtungi wa kuzimia moto kwa usalama zaidi. Nadhani wengi tunahisi mitungi ni kwa ajili ya kampuni na ofisi ila hata katika makazi yetu ni muhimu.

Na kabla ya kuwasha jiko hakikisha umekagua mfumo wa gesi ili kuhakikisha usalama.

Mwisho, kama unapika na upo mbali na jiko, weka moto kidogo ili chukula kiendelee kuiva taratibu kwani moto mwingi unaweza kukausha maji na baadae chakula na hata kusababisha mlipuko wa moto. Hili lilinitokea bahati nzuri ni moshi ulijaa ndani tu.

Asante sana kwa usikivu wako
 
You are right.

Emergency exit route ni MUHIMU SANA KUZINGATIWA wakati wa ujenzi wa nyumba.
Watu waweke madirisha ya magrill yanayoweza kufunguka Kama milango yenye bawaba. Aidha, Watu wafundishwe na kusisitizwa kuhusu matumizi sahihi ya majiko ya Gesi huko majumbani mwao. Jiko la Gesi ni bomu ambalo linaweza kulipuka muda wowote ule, hivyo matumizi yake yanahitaji uangalifu Sana hususani kwenye Nyumba zenye madirisha ya vioo ya aluminum.
 
Wazo zuri ila kwenye hiyo nyumba ukiamka asubuhi alafu ukaskia watu wanajadiliana wanasema

"Alafu huyu aliefanya hivi siyo mtu wa mbali anaijua vizuri hii nyumba , kwa mgeni asingejua kuwa hapa kuna dirisha la dharua na akaja kupitia hapahapa"

Ujue tayari watu wameshalizwa.
 
Wazo zuri ila kwenye hiyo nyumba ukiamka asubuhi alafu ukaskia watu wanajadiliana wanasema

"Alafu huyu aliefanya hivi siyo mtu wa mbali anaijua vizuri hii nyumba , kwa mgeni asingejua kuwa hapa kuna dirisha la dharua na akaja kupitia hapahapa"

Ujue tayari watu wameshalizwa.
Huwa wanaanza na TV kwanza😂😂😂
 
Bora nife na mali zangu ndani kuliko uzungu wa kuweka dirisha lelemama waniibie mali zangu, huko wenzetu wazungu wanaweza kujenga madirisha ya dharura ya kutokea kwa sababu hakuna wizi sasa we unaishi Tandale kwa Tumbo halafu uweke dirisha lisilo imara unategemea nini
 
You are right.

Emergency exit route ni MUHIMU SANA KUZINGATIWA wakati wa ujenzi wa nyumba.
Watu waweke madirisha ya magrill yanayoweza kufunguka Kama milango yenye bawaba. Aidha, Watu wafundishwe na kusisitizwa kuhusu matumizi sahihi ya majiko ya Gesi huko majumbani mwao. Jiko la Gesi ni bomu ambalo linaweza kulipuka muda wowote ule, hivyo matumizi yake yanahitaji uangalifu Sana hususani kwenye Nyumba zenye madirisha ya vioo ya aluminum.
Asante kwa mkazo huu. Nimeona nyumba ina chumba kama gereza wala hamna existing window
 
Wazo zuri ila kwenye hiyo nyumba ukiamka asubuhi alafu ukaskia watu wanajadiliana wanasema

"Alafu huyu aliefanya hivi siyo mtu wa mbali anaijua vizuri hii nyumba , kwa mgeni asingejua kuwa hapa kuna dirisha la dharua na akaja kupitia hapahapa"

Ujue tayari watu wameshalizwa.
Ha ha ha nahisi kwa nyumba yako hutokosana namna ya kuweka privacy😁😁
 
Bora nife na mali zangu ndani kuliko uzungu wa kuweka dirisha lelemama waniibie mali zangu, huko wenzetu wazungu wanaweza kujenga madirisha ya dharura ya kutokea kwa sababu hakuna wizi sasa we unaishi Tandale kwa Tumbo halafu uweke dirisha lisilo imara unategemea nini
Ha ha ha ha😁🤣🤣
 
Uko sahihi mimi nimeweka mlango wa dharura naufungia kwa ndani tu ukiwa nje huwezi kuufunga wala kufungua,kuna nyumba iliungua buguruni,familia inaungua inajona wakawa wanaagana kabisa na majirani,haya baba nanii wasalimie huko mbingumi
 
Upo sahihi - pia nimeona kuna mitungi mizuri inazima moto automatic that is good .

So I think we need to think out of box about our security and safety.
 
Uko sahihi mimi nimeweka mlango wa dharura naufungia kwa ndani tu ukiwa nje huwezi kuufunga wala kufungua,kuna nyumba iliungua buguruni,familia inaungua inajona wakawa wanaagana kabisa na majirani,haya baba nanii wasalimie huko mbingumi
Dah!!!🥲
 
Retractable security grills nafikiri inaweza kuwa salama zaidi incase kukitokea tatizo la moto. Binafsi hizi grills madirishani zilishanishinda sijaweka na madirisha yangu ni makubwa full sliding windows - floor to ceiling (3m by 2.4m) niliongeza ukubwa wa madirisha kidogo kutoka mita 2 mpaka mita 3 nikifungua napata uwazi wa 1.5m.
 
Back
Top Bottom