Weka hapa tabia za ovyo za madereva wa bongo zilizojaa ushamba, ubabe, chuki na usela

Weka hapa tabia za ovyo za madereva wa bongo zilizojaa ushamba, ubabe, chuki na usela

  1. Dereva anataka kuingia barabarani toka barabara ndogo, au kukatisha barabara kuingia kulia, na wewe hutaki kumruhusu au kusimama ili aingie au kukatisha barabara.
  2. Unaruhusiwa kuingia barabarani au kukatisha na dereva mwingine, na wewe hutoi shukurani kwa ishara ya taa au hata kupunga mkono wa asante au thumbs up, umekaza uso tu kama vile barabara ni ya baba yako. Kukosa kuonyesha shukurani ni tabia ya kishenzi
  3. Mtu anataka kuku-overtake na wewe unaongeza spidi ili asiku-overtake, au asiingie mbele yako, japo ulikuwa unaenda taratabu
  4. Una-overtake kwenye jam, na upapoona kuna gari zinakuja mbele yako na kulazimisha kurudi kwenye line kwa ku-bully gari ndogo au za gharama kubwa bila hata kuomba kuingia
  5. Una-overtake kwenye Zebra crossing, au unaona kuna group la watu wanataka kuvuka barabara kwenye Zebra crossing, na wala hujali kuwapa nafasi.
  6. Kuna trafic jam, na sasa upande wa jam wanatengeneza lane mbili na kuwaachia upande wa pili nafasi kidogo ili wapite. Wewe unaamua kutengeneza lane yako ya tatu na ku-block magari yanayokuja, japo tayari tumelazimisha kuwa na lane mbili na kuwaachia nafasi kidogo. Huu ni ushenzi, wewe unataka wao wapite wapi?
  7. Kutoa ishara za matusi unapofanyiwa kitu kibaya na dereva mwingine - kwani wewe hujawahi fanya hivyo?
Namba 4,5 na 6, zinakera na wengi hufikiri ukifanya hivi ndo ujanja
 
NAMBA MBILI KWANGU NI BIG NOO MIMI NIKIWA NA CHOMBO CHA MOTO HATA KAMA UNAKATIZA NA NIMEKUSUBIRI UKATIZE HUJANI SHUKURU AU KUPIGA HONI YA FRESH KWANGU SIO ISHU KABISA WALA SIJARI

BARABARANI MAMBO NI MENGI WENGINE WANA STRESS SASA UKITAKA KILA SEHEMU UPEWE SHUKURANI KUTOKANA NA UDEREVA WAKO WENYE UBORA SASA ITAKUWA NI MCHEZO

MIMI HATA UKISIPO NIPA SHUKURANI AU KUPIGA HONI FRESH TU NINACHOCHUKUA NI KWAMBA SASA NIMEKOMAA KATIKA UDEREVA BASI
 
Unampa lift mtu anaanza kukuelekeza ongeza au punguza speed, volume ya muziki, overtake yule, mpigie honi huyu, simama nimpungie mkono huyo
Kuna jamangu, nikibembeba atakuonyesha taa ya mkanda, punguza mwendo si unajua mbele kuna kona, tunakaribia kona washa indiketa, inaiona hiyo mbele kule anataka kuingia barabarani.
 
Kupiga honi hovyo!

Hivi honi inaandikwa Piiiiii...! ama Poooo....! 😆😆😆😆😆😆
Wacha nikupigie honi tena Piiiiii.....!!! Poooooo....!!! 😂😂😂😂😂😂😂😂.

Nguo yako ya Oktomba 30 ntamwambia fundi akuwekee honi mgongoni ukikaa inalia Pooooo.....!!! 🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Au akuwekee honi kwenye mokasini yako ukitembea vilie Piiiiiii Poooooo....
😆😆😆😆😆😆😆 aahahahahaa my ribs looh!!
 
Dereva anataka kuingia barabarani toka barabara ndogo, au kukatisha barabara kuingia kulia, na wewe hutaki kumruhusu au kusimama ili aingie au kukatisha barabara.
Sio lazima kumruhusu aingie kila atakapo. Tabia mbaya ni dereva anaetoka njia ndogo kulazimisha kuingia njia kubwa bila kuwa na subira. Au anataka akate kulia anawasha taa tu na kuingia kama yuko chooni kwake. Hio ndio tabia ya kishenzi. Unataka kuingia barabara kubwa au kuingia kulia kaa kwa kutulia magari yapungua au wapo wastaarabu watakupisha uingie.
 
8. Mtu ana overtake anaona kuna gari mbele linakuja analiwashia taa full limpishe hii tabia wanayo sana madereva wa serikali
Huwa wanashangaza hao watu, inamaana mimi niko kwenye lane yangu ndio ananipa warning nimpishe wakati yeye ndio katanua.
 
Hii ya kuongeza speed ukitaka kumu overtake huwa inanishangaza sana
Huwa najiuliza inamaana hutaki upitwe au kupenda ligi au roho mbaya tu
 
Back
Top Bottom