sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,407
- 19,264
Kuna kitu kinaitwa CPI - Consumer Price Index; kuna udambwi dambwi mwingi sana wa kichumi lkn kwa lugha rahisi maana yake ni -> bidhaa na huduma zinazotumika zaidi kwa mwezi katika kundi fulani la watu. ripoti ya CPI ya Tanzania inaandaliwa kila mwezi na National Bureau of Statistics (Ofisi ya Taifa ya Takwimu)
Ukitaka kujua vipaumbele vya watanzania, tunazika hela zetu ktk bidhaa gani, vitu ambavyo watanzania hawajawahi kuvutiwa navyo - lazima upitie report kama hizi. Sio mjasiriamali unaona wamarekani Silicon Valley wanasuka Softwares na wewe upo Kimara Baruti unaanza kusuka App ambazo wabongo hawawezi kua na muda nazo. Dec 2019 Jumia *kampuni ya mauzo mtandaoni) walifunga kazi zao wakarudi walipotoka. Kama mjasiriamali lazima ujue wadau wanachoma hela zao kwenye bidhaa zipi, uende huko ukazikusanye hizo hela
Kuna jamaa zangu Software eng. waliunda mobile App kali sana ya wagonjwa kukutana na daktari. sasa hivi nawaona wamerudi kwenye vitu ambavyo waTZ wanavielewa kama ku-burn CD, kupiga window, kuInstall Anti virus, kuFormat flash na kuwadanlodia wakulangwa internet. Watanzania wana vitu vyao, na huwezi kuwabadili mtazamo kisa umesoma sijui Oxford. Takwimu inasema matumizi ya waTZ yapo hivi
1. Chakula na vinywaji baridi - 38.5%
2. Usafiri - 12.5%
3. Pango, umeme, maji & gesi - 11.6%
4. Pamba kali na viatu - 8.3%
5. Fenicha, vifaa & urembo wa ndani - 6.3%
6. Vifurushi vya mawasiliano - 5.6%
7. Misosi ya hoteli na bata - 4.2%
8. Pombe na sigara - 3.7%
9. Vitu baki km kuhonga, kuzurura usiku, bidhaa zisizo za msingi - 3.1%
Vitu vitatu vilivyoshika mkia kabisa, wabongo hawana muda navyo kabisa na huwaambii kitu ni
1. Huduma ya Afya - 2.9%
2. Elimu - 1.5%
3. Uwekezaji - 0.01%
Sasa ukiona mtu ana degree ya pharmacy na anapiga uwinga wa nguo na viatu hp IG na WhatsApp status, inabidi uelewe kua yupo sahihi, sababu kama mtanzania anapata mshahara mil 1 kwa mwezi, atatumia 83,000 kununua viatu na 29,000 kununua dawa. fuata mkondo wa pesa sio passion. Bishana na yeyote ila usibishane na namba. Usipoteze muda wako kufanya vitu vice versa. Utaliwa kichwa boss!
Credits: Sir_Jeff
Ukitaka kujua vipaumbele vya watanzania, tunazika hela zetu ktk bidhaa gani, vitu ambavyo watanzania hawajawahi kuvutiwa navyo - lazima upitie report kama hizi. Sio mjasiriamali unaona wamarekani Silicon Valley wanasuka Softwares na wewe upo Kimara Baruti unaanza kusuka App ambazo wabongo hawawezi kua na muda nazo. Dec 2019 Jumia *kampuni ya mauzo mtandaoni) walifunga kazi zao wakarudi walipotoka. Kama mjasiriamali lazima ujue wadau wanachoma hela zao kwenye bidhaa zipi, uende huko ukazikusanye hizo hela
Kuna jamaa zangu Software eng. waliunda mobile App kali sana ya wagonjwa kukutana na daktari. sasa hivi nawaona wamerudi kwenye vitu ambavyo waTZ wanavielewa kama ku-burn CD, kupiga window, kuInstall Anti virus, kuFormat flash na kuwadanlodia wakulangwa internet. Watanzania wana vitu vyao, na huwezi kuwabadili mtazamo kisa umesoma sijui Oxford. Takwimu inasema matumizi ya waTZ yapo hivi
1. Chakula na vinywaji baridi - 38.5%
2. Usafiri - 12.5%
3. Pango, umeme, maji & gesi - 11.6%
4. Pamba kali na viatu - 8.3%
5. Fenicha, vifaa & urembo wa ndani - 6.3%
6. Vifurushi vya mawasiliano - 5.6%
7. Misosi ya hoteli na bata - 4.2%
8. Pombe na sigara - 3.7%
9. Vitu baki km kuhonga, kuzurura usiku, bidhaa zisizo za msingi - 3.1%
Vitu vitatu vilivyoshika mkia kabisa, wabongo hawana muda navyo kabisa na huwaambii kitu ni
1. Huduma ya Afya - 2.9%
2. Elimu - 1.5%
3. Uwekezaji - 0.01%
Sasa ukiona mtu ana degree ya pharmacy na anapiga uwinga wa nguo na viatu hp IG na WhatsApp status, inabidi uelewe kua yupo sahihi, sababu kama mtanzania anapata mshahara mil 1 kwa mwezi, atatumia 83,000 kununua viatu na 29,000 kununua dawa. fuata mkondo wa pesa sio passion. Bishana na yeyote ila usibishane na namba. Usipoteze muda wako kufanya vitu vice versa. Utaliwa kichwa boss!
Credits: Sir_Jeff