Wema nimemtengeneza, hawatamuweza tena - Mama Wema

Wema nimemtengeneza, hawatamuweza tena - Mama Wema

ngoshwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2009
Posts
4,131
Reaction score
937
Mama yake Wema Sepetu, Bi Mariam Sepetu afunguka kwa ghadhabu akiwatakia wale wote ambao wamekuwa wakifuatilia maisha ya mwanae hasa waandishi wa habari za Udaku waache mara moja vinginevyo atakula nao sahani moja.

Akieleza kwenye Kipindi cha "Take One" kinachorushwa na Clouds TV, amejigamba kuwa mwanae alikuwa na "tabia nzuri" lakini baadhi ya marafiki wamemharibu japo bado anakubalika na watanzania wote.

Amesema wengi wa marafiki walifikia hata kumpeleka kwa waganga wa Kienyeji, na kuna wengine amefikia kuwafukuza kabisa wasikanyage nyumbani kwake kutokana na tabia zao.

Akifunguka kwa maneno tata mama huyo amesema kuwa ana mchukia sana Diamond kutokana na "kumtumia mwanae" kwa ajili ya mafanikio yake ya kimuziki (hakufafanua kimtumia mwanae kivipi?) ila alisema kuwa ameyajua hayo baada ya kuzunguka.

Alieleza pia kuwa amehangaika sana kumrudisha Wema hapa alipofikia sasa. Aalisema kuwa amegundua mengi sana ambayo marafiki zake walikuwa wakimfanyia (hakuwataja zaidi ya Jackline Whopper) ambae anasema aliwahi kumtusi mwanae wakati fulani kuhusu maangaiko yake na kusema hana pa kuishi.. "Huyo Whopper aelewe Wema hapa ndio nyumbani kwao alipozaliwa" aling'aka mama huyo.

Kuhusu mahusiano ya Wema na Diamond alisema, alimchukia sana Diamond tokea walipoanza mahusiano na Wema kwani Diamond alilenga kumtumia tu mwanane kufika pale alipo lakini atashuka muda si mrefu. "Diamond hana adabu hata kidogo, kijana huwezi kumchukua binti wa watu ukaenda kumvisha pete ukumbini hata wazazi wake hawajui wala hujaenda kujitambulisha kwa wazazi wake...hii ni dharau kubwa sana aliyoifanya na mimi nilisema, kamwe asingeweweza kuishi na mwanagu kama mimi mzazi wake sijapenda".

Alionya kuwa kwa sasa mwanae WEMA amemtengeneza na hakuna atakaweza tena kumvuruga kama mwanzo.... Hata hivyo, Mzazi huyu aliyeonekana akiongea kwa machungu hakuweza kufafanua mwanae amemtengeneza namna gani....

Pata Majigambo mazima ya mama huyo hapa:


 
Last edited by a moderator:
Diamond anaonekana mshirikina sana huyo dogo,
 
Like Mom Like Daughter..huyu mama hana busara na hata shule nina mashaka nayo..mswahili na mshirikina sana anaonekana..yani una ropoka kumtengeneza kwa mganga binti..what a shame..? ngoja aje zamaradi mketema na ID yake ya Mrembo By Nature aanze kumwaga mitusi!
 
lol! some moms are amazing! kutetea upumbavu, eti marafiki walimharibu, kwani walimfunga kamba kumvuta na kumharibu! pathetic eish!
 
Anamchukia diamond kisa? Au alitaka apewe ile pete yeye? Maana kwa ile tabia yake anaweza kuwa anataka dogodogo! Hata kama wanasema mama is the best, then kwa mama wa aina ile nimegundua ina ukweli. Malezi ya mama saa nyingine bana, angalia lulu, wema, diamond hewa kabisa.
 
Anamchukia diamond kisa? Au alitaka apewe ile pete yeye? Maana kwa ile tabia yake anaweza kuwa anataka dogodogo! Hata kama wanasema mama is the best, then kwa mama wa aina ile nimegundua ina ukweli. Malezi ya mama saa nyingine bana, angalia lulu, wema, diamond hewa kabisa.

Pengine akina mama ndio wanaoharibu watoto kwa kile wanacho dhani ni mapenzi ya dhati..hakuna mama ambae anapenda mwanae aonekane kakosea, akina mama wanapenda zaidi watoto wao kuliko watoto wa wanawake wenzao..kwa kuona kuwa wao ndio walioumia kuzaa mtoto pengine wanapoteza mwelekeo na kusababisha watoto wasimheshimu wengine hata Baba zao...Tuangalie malezi ya watoto wetu, tutawaharibu!!
 
huyu mama analaumu magazeti ya udaku wakati akina wema wanalipa pesa ili waandikwe.!
 
Wema si anapeleka habari zake mwenyewe kwenye magazeti. Na kipindi cha Jumbe huyu Diamond alikuwepo? amuache mtoto wa watu, mtoto wake amechafuka kitambo.
 
hii familia ni washirikina hata kwa jumbe walidai hivihivi ptyuu!
 
mama Wemal anaonekana ni Mshirikina kabisa, sasa huyo Wemma anarogwa na kuchezewa nani? Wakati tabia zake ndio zinazo mfanya aonekane kama Mwehu fulani? Kwanini sio Nancy Sumari? Awe yeye? Mama na mwanae wote washirikina tu...
 
Duh mama ake ni mchawi sana na mswahili mno,ptuuuuuu naisi hata la saba hakufika yule mama kaishia chekechea maneno gani yale ya kuongea mbela ya camera
 
Duh mama ake ni mchawi sana na mswahili mno,ptuuuuuu naisi hata la saba hakufika yule mama kaishia chekechea maneno gani yale ya kuongea mbela ya camera

wote washirikina hao mama na mwana
 
Asiyefunzwa na ***** hufunzwa na ulimwengu.Huyu mama anaonekana hamjui mwanae vizuri, ataaibika.
 
"Nani kama mama? wahenga nao hawakufafanua mama wa aina gani maana kama mama anajigamba kumtengeneza mwanae hapo kuna nini tena!
 
Jamani kumtukana Wema inatosha,mama yake mngemwacha tu hata kama yukoje ni mtu mzima
ni sawa na mama yako.

Halafu hii dhana ya kila mtu akikosea kusema Elimu,Elimu,Elimu...sio kweli, hakuna watu waliokua na hekima, busara na wastaarabu kama bibi na babu zetu huko nyuma na hawakusoma hata darasa moja.
Ila muafrika akiwa tu na degree, kila kitu mtu akikosea utasikia ni kwa vile hana elimu
yaani anakua Limbukeni kupitiliza.
 
Back
Top Bottom