Habari wana JF wenzangu hopeful mpo poa!
Jana usiku nlikuwa natazama kipindi cha THE MBONI SHOW katika kituo cha runinga namba 1kwa vijana Tanzania EATV chini utangazaji wa mwanadada MBONI MASIMBA ambapo katika kipindi huwa ana walika wegeni tofauti tofauti kuzungumza mada mbalimbali za kijamii,kiutamaduni,kimapenzi nk.
Kwa show ya jana alikuwa na bongo moves star Wema Isack Abraham Sepetu wakijadili mada ya Uwazi katika Mapenzi ambapo mwanadada Wema bila kupepesa macho wala kutafuna maneno alitiririka kinagaubauga kuhusu maisha yake ya kimahusiano ya mapenzi,ambapo aliwataja wanaume wote ambao kwa nyakati tofauti amedate nao.
Wanaume wao ni pamoja na Marehemu Stephen Kanumba,Jumbe,TID,Mr Blue,Chalz Baba na hivi karibuni Dimond Platinum"sukari ya warembo"Kwanza niseme nlikuwa sifahamu kama Wema ni Binti wa kiislam!ila ni katika show hiyo ya jana nlifahamu kutokana na Wema mwenyewe kujiita mtoto wa kiislam pale alipokuwa anajitetea au kujibu maswali aliyokuwa akibanwa na aidha wanaalikwa kwenye show au host wa kipindi Mboni Masimba.
Lengo la thread hii siyo kuutazama na kujaji uislamu wa Wema ila kilichonisikitisha ni jinsi Wema alikuwa anajificha katika kivuli cha mwamvuli wa dini ya kiislam kwa mambo mbalimbali aliyokuwa akiulizwa!Ni ukweli usiopingika kuwa matendo anayofanya Wema ni kinyume kabisa na mafundisho ya dini ya kiislamu au jinsi binti wa kiislamu anatakiwa aishi,mojawapo ikiwa ni hilo la kukiri kufanya zinaa na wanaume zaidi ya watano kabla ya ndoa tena hadharani.
Ni aibu kubwa Wema Kujivunia uislamu wake wakati matendo yake yapo kinyume kabisa na mafundisho ya dini hiyo!
Wito wangu kwa dada Wema na mastar wengine ambao wana majina ya kiislam waache haka katibia cha kujiita mtoto wa kiislam wakati dhahiri shahiri metendo,tabia na maadili yao haviendani na mafundisho ya dini ya kiislamu kwani wanaidhalilisha uislam na waislamu ni vyema wakakaa kimya tu wasifiche uchafu wao kwa kujiita watoto wakiislamu!Uislam kama dini ni mfumo mzima wa maisha wenye maadili sheria na taratibu zake ambazo Wema anatakiwa kuzifuata kabla ya kujinadi kuwa yeye ni mtoto wa kiislam!
Mwisho napenda kumsihi dada yangu Wema kumrejea Muumba Wake kama ilivyoamrishwa ktk kitabu chao kitakatifu cha Quran!