Elections 2010 Wengi hawajui Nguvu ya Maaskofu

Status
Not open for further replies.
Mdondoaji said:
Vile vile ungeliongezea kuwa viongozi wa dini wangelijiepusha kuonyesha wanakubaliana na viongozi wa chama fulani au itikadi ya chama fulani, kwani waumini wao ni wafuasi wa vyama vyote Tanzania. Hivyo basi lingejenga mazingira ya kuaminiana zaidi.

Mdondoaji,

..true .. true.

..labda kuwa specific ni kwamba wasimuunge mkono mgombea wa chama fulani kwasababu tu ni muumini wa dini yao.

..katika uchaguzi uliopita kulikuwa na wagombea watatu wa Uraisi ambao ama wanajulikana kwa uzinzi, au ndoa zao zilikuwa na mgogoro. tatizo ni kwamba viongozi wa dini moja wakaamua kumshambulia mgombea asiye wa dini yao na "kuwamezea" wale wengine.
 
Mtazamo wangu ni kuwa katika suala la kutokuaminiana viongozi wa dini wana dhambi ya kuchochea na kutofanya juhudi za kutosha kuondoa hali hiyo.

Mzizi wa hali hii ni jamii zetu kuanzia ngazi za familia. Wengi wetu tunakuzwa katika hali ya kuaminishwa kuwa dini zetu ni nzuri na za kweli sio kwa mafanikio yake bali kwa kulinganisha na "ubaya" wa dini zingine. Hali hii hutoka katika familia hadi katika mfumo mzima wa kijamii ukiwemo mfumo wa elimu yetu. Na hata tunapokuwa wakubwa hali hii tunakutana nayo mitaani na vijiweni. Inapofika katika ngazi ya makazini na nafasi za kiuchumi na kisiasa ndio hali inakuwa mbaya zaidi. Tatizo linakuwa zaidi pale viongozi wetu wa kidini wanapoamua kuchagua makundi ya kisiasa kama nyenzo za kulinda, kutetea ama kuhakisha maslahi yao binafsi na pia makundi yao.

Sasa unapokuta tunakuwa mfumo hovyo wa kisiasa unaohodhiwa na wanasiasa wajanjawajanja na wenye tamaa isiyo na kifani, ndipo mchanyato huo unapokuwa mkubwa na kupelekea hali hii ya kutukuaminiana kugeuka kuwa hali ya kuchukiana kama ambavyo inajijenga sasa.
 
maaskofu hawana mamlaka ya kumkataa meya aliyechaguliwa na wananchi(waislam+wakristo+wasio na dini),kufanaya hivyo ina maaana wanataka awe nani?:

 
Maovu anayosema chatanda kwa akili yake finyu ni kibaka kukwapua simu basi!! lakini Dowans,IPTL,KAGODA,WIZI WA KURA kwake yeye hayo sio maovu!!
 
Hao wasiojua nguvu ya maaskofu nadhani wamekuja Tanzania jana au juzi,lakini kwa mtanzania halisi awe mkristo au mwislamu na hata mpagani kwa sehemu fulani maisha yake ya kila siku yanaguswa na mchnago wa maaskofu na madhehebu yao katika kutoa huduma za jamii kama Shule,Afya,Maji n.k. Kama serikali inatambua mchango huo na kuupoke,basi yanapotokea matatizo yeyote katika jamii vingozi hawa wa kidini wanayo nafasi ya kukemea na kutoa maoni yao.
 

Hili ni tatizo, la watu wengi ambo badala ya kujadili hoja, wanaingiza mambo ya kidini ambayo kimsingi hayawezi kuleta suluhisho la hoja iliyo mezani.
 
Mimi na ungana na wadau wanaopinga kujadili mambo kwa hisia za udini
 
wapemba 27 walivyouwa mwaka 2001 na mzee mkapa hawa maaskofu walikuwa hawajazaliwa au walikuwa bado hawajahitimu mafunzo ya uaskofu? maana hawakutoa kauli yoyote!

Walitoa tamko na hapa jf kuna mtu alipost lile tamko litakuwepo some where search.
 
Mashirika ya dini hapa Tanzania ambao mengi yake yuko chini ya Maaskofu yana mchango mkubwa katika nchi hii. Hivyo Maaskofu ni wadau wakubwa katika jamii. Pia maaskofu wanasimamia makanisa ambayo wanaumini wake ni wananchi wale wale ambao ndio wapiga kura na wanategemewa na viongozi wa siasa kuendesha nchi. Sasa unakuwaje pale maaskofu wanapoona haki ya waumini wao inapotea na kuamua kukemea wanaonakana wanafanya mambo yasiyowahusu? Hao wanapinga viongozi wa dini kukemea mambo mabaya ndio wana matatizo kwani kama kusingekuwa na ubaya maaskofu hawangekuwa na cha kusema. Pia wao sio wa kwanza kusema bali wanaungana tu na wanajamii wengine kukemea mambo maovu baada ya kusikia kilio cha jamii.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…