"Wengi Wape"...Uamuzi Mzito

umuhimu wa kwanza ni...


  • Total voters
    40
Mbu tatizo ni kwamba una ngazi mbili, usipokua makini moja inaweza kuporomoka na kusababisha inayobaki nayo ikose nguvu ya kukuweka juu. Kwahiyo vyovyote utakavyofanya hakikisha wewe uliyeko katikati umejibalance vizuri,that's all.
 
Reactions: Mbu
Hapa wachangiaji wengi mmejielekeza kukieleza kipato ni fedha tu ! . Wakati mimi naamini hata ukijielekeza Shambani ukivuna na kutokuuza ukala mwenyewe mavuno yako pia ni kipato.
 
Reactions: Mbu
Soulmate
Samahani sikuwa nimeiona hii post mapema. Ila ninapenda kuchangia nami kidogo. Kwa mtazamo wa haraka familia ni muhimu kuliko kipato. Ukilinganisha umuhimu wa kuwa karibu na familia yako na ule wa kukaa mbali kutafuta maisha uzito unaangukia kwenye kukaa na familia lakini Soulmate, critically thinking itakufaa kipi kukaa na familia pasipo kuimudu? unakaa na kuangalia jinsi wapendwa wako wanavyopata shida kwa kukosa mahitaji muhimu? uwepo wako pekee pasipo kuwa na uwezo wa kutimiza majukumu yako kama mzazi hakulipi (ni kwa mtazamo wangu mie) ni bora kipato kwani ninaelewa kuwa angalau katika kuhangaika kwako kutafuta kipato, unapata muda japo wiki mbeli au mwezi kukaa na familia yako. Use effectively, utilize effectively huo muda mfupi kwa kuwa na familia so that unakuwa na stable kipato at the same tome short but quality time ya kuenjoy na familia yako (kwa kutumia kipato ulichokipata) otherwise hata ukiwa unashinda na familia yako 24/7 kama kipato ni mgogoro kwanza hata wao hawatasettle nawe kuenjoy hiyo wanayoita quality time, watakaa nawe kipindio kifupi kisha kila mtu achanje mbuga kuhangaikia tumbo na mahitaji mengine..... na kama ndo una mke ndo kwanza anaweza akaanza kukudespise kuwa u mume ambaye hayuko responsible kwa kuitunza familia yake.

nadhani ndio maana wazazi wengine wanachukuaga maamuzi magumu ya kwenda machimboni huko mbali na familia kutafuta maisha. Otherwise life would be so easy Soulmate.
 

Kwa mara ya kwanza umenivuruga vuruga kabisa??

Kura umepiga upande gani??....Kipato au familia???

Babu DC!!
 
Mimi hili nalitazama kwa jicho la tatu zaidi kwa maana ya Ukosefu wa Miundombinu ya kisasa huku kwetu ndio chanzo cha haya yoote ya kukaa mbali na familia. Chukulia mfano umbali wa kutoka Dsm hadi Morogoro, familia ipo Dsm, mimi nipo kikazi Moro, kama kungekuwa na Miundo mbinu ya kisasa mfano Treni ya Umeme, hapa ni mwendo wa kwenda kibaruani na jioni upo home na familia.
BUT, kwangu mimi upendo kwa familia kwanza, kipato kinafuata. Nikiugua familia ndo itakuja itaniuguza, Nikifa ndo itanizika regard less nipo wapi
 
Kwa mara ya kwanza umenivuruga vuruga kabisa??

Kura umepiga upande gani??....Kipato au familia???

Babu DC!!
Babu jibu langu halipo kwenye poll yake.............. si familia wala si kipato bali ni familia unayoweza kuimudu (kwa maana ya kuwa na kipato cha kuiendeshea) na si familia mkono mtupu na wala si kipato bila familia. Sijuibado nimekuchanganya??

Nisamehe bure Mjukuu wako nimeuanza mwaka kivingine!
 
Familia kwanza kipato baadaye,ukiwa na ushirikiano na familia then kipato kitakuja,na isitoshe kuwa karibu na
familia inaongeza ushirikiano
 

Nimeangalia tena kuona kama hili swali lina chembe yoyote ya utata,

...[h=2]umuhimu wa kwanza ni...[/h]

Kweli katika hayo mawili umeshindwa kupata kipi ni nambari one na kipi kinafuatia??

Mie ninavyoamini, familia ni nambari one, tena pia ni nambari mbili, tatu na hata nne!!

Kwa sababu mleta mada hajatuelza kama tuchague kuwa na kimoja peke yake, kwa hiyo unaweza kuwa na wingi wa kimoja na hilo jingine likawa kidogo. Hivyo, nikiwa na familia yangu iko stable, sitashindwa kutafuta kidogo kidogo cha kutuweka mjini!!

Kama ni kipato cha kunipa mafweza ya kumwaga (kama yale ya EPA) at the expense of my family..please hicho kipato niko tayari kukikosa!!


Babu DC!!
 


...Sijui ni kipato kikubwa kiasi gani hicho Mbu ambacho kitakufanya uamue uishi mbali na familia yako. Fikiria raha ya kuona mwanao anazaliwa na kumshika mikononi mwako kwa mara ya kwanza, anakaa chini kwa mara ya kwanza na anakaa kiajabu ajabu 🙂🙂akichoka anaanguka lakini uko nyuma yake kuhakikisha unamdaka kabla hajafika sakafuni/ardhini, kumuona anaanza kutambaa kwa mara ya kwanza wengine hutambaa kiajabu ajabu 🙂🙂 mpaka ile tambaa yake inakuvunja mbavu kupita kiasi 🙂🙂 anapoanza kusimama kwa mara ya kwanza na huku wewe na mwenzio mkijaribu kumpa motisha asimame kwa muda mrefu zaidi huku mkimuimbia simama dede sima dede 🙂🙂 anapoanza kunyanyua mguu mmoja katika kujaribu kuanza kutembea na mambo mengine chungu nzima.

Mhhhhh labda kuwaona kila baada ya miezi miwili lakini miezi sita hadi nane kwa maoni yangu ni mingi saaaaana, sijui ila mimi naona hili ni gumu sana Mkuu. Unaweza kutuwekea hicho kipato kikubwa kinachozungumziwa hapa kiko katika range ipi labda $200,000 to $300,000, $300,000 to $400,000, $400,000 to $500,000 etc. Ukishajibu hili swali langu nitarudi na kisa nilichokiona kwa Oprah cha Mume ambaye almanusura apoteze ndoa yake.

 
Asikudanganye mtu... WE KAA MBALI TUKUMEGEE... You need to go back to your basic question.... WHY DID YOU GET MARRIED.. Majibu ya swali hili yatakusaidia kuamua
 

...kaka thx, ...ni kipato cha kawaida tu mkuu...matumizi tu ndiyo yanatofautiana, ila naweza
kusema, kipato (net!) ni mara tatu ya kipato (gross!) ambacho ningekuwa napokea 'nyumbani'...
:juggle:...
 

...ubarikiwe mkuu, hapo penye wekundu umenigusa lile neno la wahenga "kujifunza kukinai" japo kujishusha gharama!
 

dahhhh,....thx bana japo "ngumu kumesa!"

Post yako imenifanya nijiulize, hivi haya majukumu ninayojitwisha ni kwa manufaa ya nani?
Extended families nazo zina high expectations nikiwa huku 'mgodini' labda nitaporudi mjini
kidogo huruma itawaingia.

Naanza kuji question iwapo haya ndiyo majaaliwa yangu,


....
"...do I live to work, or work to live?"
 

...dahhh, hiyo ya riziki ni popote kisha ukamalizia na mvumilivu hula mbivu ndio umenipoteza kabisaaa...


Mbu & The Boss,

Naomba mnisaidie kidogo....Which of the two is more romantic??

Babu DC!!!

...mnh, labda ungeuliza which is more enjoyable...

kila ninapoondoka na kuwaacha, mwezi mzima nakuwa na homesickness,
tena ile ya kujifunika gubi gubi kutotaka kuongea na yeyote...

...muda ukipita najipa moyo, this is for the last time...!" ila pesa nayo mwanaharamu bana....
"work like a donkey to live like a king!
"
 



That is intelligent of you Mbu.... Wajua wazi ukiweka zoote, wooote watachagua zote... Hapa sina jinsi ombi langu limekataliwa inabidi ni vote family.....

Alafu Mbu do you know wengi ambao husema Money is not everything they have loads of it? lol ever wondered hilo?
 
Mi masikini mkosefu... money does not make happiness, but it can contribute largely on buying it. 🙂
 
Life is all about calculated risks. Nakumbuka baba yangu used to leave home 5am kila siku, akiita kusalimia kila mlango kabla hajaondoka. Lakini alirudi 7 pm kila siku, na dinner wa a family affair. Hata kama unaumwa utakuja kukaa na uji wako wa limao, ili uzungumze na familia. I mean calculate ur risks mbu but don't overdo. Ya leo sio ya jana, unawezajikuta una mahela, by the time umerudi home mwenza is a total stranger na wanao huwezi kuconnect nao. Washakuwa wakuubwa, you don't even know their hobbies unarudi hapa kuomba ushauri wa besdei na xmas gifts! Just don't OVERDO. Sijui kura yangu hata inaangukia wapi, manake na wewe na poll yako kama uchaguzi wa chama kimoja,kha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…