Acha niwaachie wenye kitanda mtiririke maana mie sijui kiwango cha kunguni waliopo ila nilichosema mie huo ni mwanzo kuelekea huko kwenye degree maana watu huwa tunaponda taaluma za watu wakati tatizo sio lao ni la kimfumo kama ulivyosema hasa ukizingatia kwa muda mrefu tumekuwa na chuo kimoja cha udaktari zamani chuo kikuu kishiriki Muhimbili na ili uingie Muhimbili ulikuwa unahitaji upate ufaulu wa hali ya juu na waliokuwa wanabaki ndio walikuwa wanaingia kwenye hivi vyuo na kuwa AMO (kwa waliosoma miaka 90 wanajua kwamba ili mtu uingie chuo kama Muhimbili ulikuwa unahitaji maksi nzuri sana) (kama mtu hata kuandika jina ni issue hilo sasa ni lingine either limetokana na uchakachuaji wa udahil maana sifa za anaetakiwa kuchukua Diploma zinajulikana kama amemaliza form 6 maana yake O -level alifaulu na kupata credit na mara nyingi ili uchukuliwe lazima Chemistry na Biology uwe umepata kiwango cha C kwa O level hata huku chini tumeshuhudia watu wanaingia form 1 hawajui kusoma na kuandika), mie observation yangu ni hiyo maana nachojua kuna ambao ni RMO (Rural Medical Officer) hawa wengi wao hata mie nimewashuhudia kuna utata kuhusu ufaulu na wengi wao hupelekwa vijijini kabisa kwenye zahanati alafu hawa AMO wanakuwepo kwenye vituo vya afya na wengine wapo mpaka kwenye hospitali za wilaya na mikoa ila pia kuna hawa AMO wengi ninaowajua performance yao ilikuwa nzuri O level na wengi ni wale ambao kidato cha sita walifaulu kiwango cha kawaida ambacho hakikuwazesha kuingia university pia baada ya kufanya kazi kwa kutumia vyeti vyao hivyo hivyo huingia university za Tanzania na wengine mpaka Urusi wamekwenda