Kwa kweli, ndio.
Watu tuliopata kufanya kazi katika private sector tumekuja kuzoea kupimwa/kijipima ufanisi wako.
Hatukuichukulia kama unyanyashaji bali kama njia mojawapo ya kujiendeleza kiufanisi. Haya mambo ya kuwa "ah, nitafanya kesho" yanaondoka.
Unajipangia ni kitu gani kifanyike kwa muda unaopanga (saa, siku, wiki, mwezi) halafu unajitathmini umefanikiwa kwa kiasi gani. Kama hukufanikiwa ni kwa nini, kama umefanikiwa je ungeweza kumaliza kwa muda mfupi zaidi?
Mtu unabidi uwe ( ujiwekee) log-book yako ya unachokifanya na muda unaouchukua kukifanya. Mwanzoni utaona ni usumbufu lakini ukishazoea hii nidhamu itakusaidia hata nje ya ajira.
Hii ni muhimu sana kama utaamua kujiajiri mwenyewe.