Wenye "madingi" wakali tukutane hapa

Wenye "madingi" wakali tukutane hapa

nikisema nihadithie yote humu mtachoka.. mzee alikuwa mkoloni hatari... majirani wanamuita mjerumani ila wanamkubali kichizi... unakuta msiba wa jirani au sherehe ya jirani... wakiwa wanabishana bishana kufikia uamuzi wa pamoja... wanamuita mzee kwenye kikao awasaidie kufanya maamuzi.. kwanza cha kwanza anawaomba wanawake wote wanyamaze na wabaki wasikilizaji.. kisa anaongea na wanaume wenzake jinsi marehemu asafirishwe vipi au azikwe wapi.. na hapo marehemu sio ndugu yake.. ila majirani tu wamemualika.. mzee haaamini kabisa wanawake kama wana akili.. dada yangu alipata div 1.8 form 4 na point 5 pcm marian.. ila mzee hawezi mtuma kitu chochote serious anasema akili za wanawake rahisi kutapeliwa... huwa hawawazagi mambo kwa upana hata kama wamesoma sana
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji109]
 
Siku nimeiba chupa ya bia (Safari Lager) ya mshua nikauza nikaenda video...nilivorudi usiku nilitamani ardhi ipasuke nitumbukie...nilipata cosovo almanusura kulazwa....nikikumbuka huwa namwona dingi mkatili kinoma....
 
Enzi hizo nasoma form six nimerudi likizo! Kuna demu mmoja alikuwa anapenda kupita pita mitaa ya nyumbani ili aninase....basi kumbe jana yake kwenda kutazama mechi za eufa kumbe wadogo zangu nao walitoka pale nyumbani kukawa hakuna mtu wa kufungua geti! Basi mzee alivyorudi alipiga honi alivyoona hakuna response yoyote akaamua ashuke na kufungua geti mwenyewe! Basi bwana kesho yake si ndio akanifuma namaliza na yule demu ili niokoe mzigo. Duh kilichotokea pale siwezi kukisimulia ila ni zaidi ya fedheha.
 
Ngoja nami niandike mambo kadhaa ambayo yamenifanya niamini hakuna mzee kama mzee wangu.

1. Siku moja tumeenda kwenye ngoma masikini nikaongozana na dada zangu kwenda huko mzee alikuwa yupo safarini akarudi akakuta milango yote imefungwa na kuku wapo nje yaani full tafrani hapo nje, wazee wa ngoma tukaingia kwa mbwembwe shikamoo baba!!! Hahahha tukafungua
Duh!! Hii itakuwa kanda ya ziwa km ckosei
 
mzee wangu hakuwa mkali tatizo lilikua mimi, sidhani kama pamepata kutokea mtoto mtundu kama mimi ebufikiria nimefanya attempt mbili za kumuua dogo ikiwemo kumnywesha sumu ya kuoshea ng'ombe nikijua maziwa,nilinusurika kuchoma nyumba, though sikuanajua nlichokua nafanya sababu ya utoto lakini mzee alikua akininyoosha kisawasawa hakika nilichezea kipigo btw R.I.P Baba
We ni shida
 
true yaan wanavyopelekwesha hadi unajiuliza hivi ndo yule Dingi yangu bandidu ninayemjua mimi au
mana wanakuwa wa pole kupita viwango mbaya zaidi anafanyiwa vitu ambavyo wewe mwenyewe mwenye mtoto kimfanyia usingeweza wanawadekeza zaidi ya maraika
yaan utasikia tu acha nitakuchapa
kama kuna kiti chake cha uzee hakai mtu lkn huyo mjukuu wake anapanda na michanga tena wakati mwingne wanabanana hapo kukaa kiti kimoja
station ya tv anachagua yeye
wkt enzi nzake thubutuuuu uweke station unayotaka wewe wakati yeye yupo kwanza utaanzaje
True yani huwa najiuliza sana.. yeye alikua anajiita kiboko y a wajinga ila huyu dogo hapa anamnyoosha ipasavyo
 
Mzee alikua anasema kama unajiona upo vizuri njoo tuzipange.

Alikua hapendi mtu anyoe kipara, kaka yangu akawa mbishi siku hiyo karudi home na kipara. Mzee akamwambia kimbia ukiona upo mbali sema tayari.

Jamaa akakimbia mzee anaona mdau anasogea tu hasemi tayari, akamuungia. Dakika kadhaa mbele tunaona kaka anarudishwa kabebwa begani.
Kufika home akaambiwa tuzipange, ghafla jamaa kapiga magoti analia anaomba msamaha.

Mzee akamwambia adhabu yako utakua unapaka kiwi kichwa hadi nywele ziote.
hahahahahahahahhahaha mzee wangu fair sana nakumbuka baada ya kutairiwa ananiambia unaona icho kichwa ndio kinachomtoa chozi mwanamke kwa utamu huko kwingine hakuna ishu kabisaaa ndio maana nimekutairi.....mengine baadae nitaandika hapa
 
Mkuu baba yako alipofariki (RIP) Baba angu ndo alishika ukanda wote wa maziwa..Kig, mwnz, Tbr, Sh, Kagr.

Huyu jamaa unaweza sema sio baba yako hana lugha rafiki hata kidogo..

Alijaliwa mimacho makibwa akikuangalia tu unakua mdogo..

Huyu jamaa aliniwekea watu wa kunichunga nisiongee wala kusimama na msichana.

Tushawah changia dem na hili jamaa, Siku nyingine tukakutana gest mm naingia yy anatoka..

Kanishinda 22yrs
Haaaaa haaaaa....JF duuuh
 
utawaonea hadi huruma maana akijipindua kafinywa akikaa vibaya kakojolewa basi full lawama tu...utamsikia yani huyu hana tofauti na baba ake
Hahaha,

Nimerudi likizo nimekuta madogo wanajiachia mpaka nikashangaa.

Wakati enzi zake shua mkisikiagari getini tu, hata kama kuna kikaratasikidogokikochini inabidi kiokotwekitupwe kwenye jaa, ama sivyo kinaweza kuzua kesi kubwa sana.

Mpaka juzi nikoofisini, kukawana kikaratasi kidogo kwenye carpet, sikuweza kuvumilia nikakiokota na kukitupa kwenye bin.

Discipline ya mshua hiyo.

Lakini kama ulivyosema, ukimkuta sasa utamhurumia.
 
nyinyi nyote trella... dingi yangu maarufu sana maeneo ya yombo kila mtu hadi majirani wanamuongelea enzi zake.. kuwa alikuwa hatari...

enzi hizo dar bado wenyeji wengi mitaa ya uswahilini kuna ngoma za wamakonde na wazaramo kibao....

kuna siku wazaramo walipita na kigodoro chao mchana nje ya ukuta dingi alikuwa anapalilia majani... wazaramo kibao kama 200 hivi.. dingi akawasimamisha.. na kuwauliza hivi kila kabila hapa likisema lipige ngoma yake si itakuwa balaa.. akawaambia ngoma za wazaramo kwa mchaga, mkurya, mnyakyusa, mhehe etc ni usumbufu.. kama wanataka ngoma wakapigie kwao msanga huko ambapo hakuna makabila mengine... wazaramo wakacharuka si unajua wanaongea sana wakaanza msuta dingi... mzee akajifanya amezidiwa.. akawaambia amependa hoja zao wamsubiri awaletee zawadi ya mwali wao...

wale wazaramo walivyo wajinga wakamsubiri kweli... dingi kazama ndani.. chumbani kwake kachukua gobole lake... kilichotokea ilikuwa story yombo mzima hakuna ambaye haijui..... dingi alivyotoka tu nje na gobole wakaanza kimbia na wapiga ngoma wakaacha ngoma zao.. dingi akazigeuza zile ngoma ni mafunzo ya kulenga shabaha... zile ngoma kubwa akazitia risasi zote.. na gobole lina kelele balaaaaa... mtaa mzima ndanii.. yeye anazitia shaba tu.

hawakurudi tena na ngoma zote zikawa zinapita mtaa wa pili.. hazipiti njia ya kwetu wanaogopa mwanajeshi mstaafu

dingi alikuwa anatubondaaa hadi mama analia yeye...

anakwambia ndani ya nyumba rafiki yake mke wake tu.. ana gari lake land rovee ukiingia humo huruhusiwi kukaa kiti cha mbele ni cha mke wake tu mama yetu.... na hata ukikaa siti ya nyuma ukipigwa wimbo mzuri huruhusiwi kutikisa kichwa anakushusha... enzi hizo watoto wake alikuwa anatushusha kwenda kanisani eti tunatikisa kichwa kwenye gari lake tukisikia mziki mzuri.. so kanisani inabidi twende kwa mguu.. yeye na mama ndio kwenye gari
hhahahahahahahahahahahahahaha leo mmenichekesha sana kwa kweli hahahahahahaha
 
Nimesoma comments zote hakuna anayemfikia mshua wangu kwa ukali hadi sasa hivi bado ni kimeo tuu
 
hao wazee wote mnaiwataja hapa hamna kitu asee nakumbuka mwaka 84 ilikua jumamosi mzee akatuagiza majani ya kuku tulikua na kuku wengi sana yeye akaenda kazini ..tulivyoenda tulikaa mpaka saa nane au tisa hivi ndo tukarudi na mizigo yetu ya majani ya kuku watu wa arusha wanayafahamu majani ya sungura..bwana kumbe mzee alikua amesharudi na ameenda kutafuta chakula cha kuku mwenyewe....

Kwakuanzia tuliambiwa kila mtu ale mzigo wake coz tuna njaa na kuku wameshakula hamna pa kuyapeleka...kwa jinsi alivyokua tukaanza kupiga mdogo mdogo tulikua watatu...kaka yangu akaleta ukorofi mzee alimtia kwenye gunia la kuhifadhia kahawa akalifunga kwa juu asee alimtia fimbo zisizo na idadi ..akamtoa kwenye gunia akamtia fimbo kavu kavu mpaka vijiti vikamwingia kama miba then akamfingia kwenye mti wa mlimao kwa minyororo kwa siku 3 day and 9t tulikua tunampelekea msosi kwa siri usiku na alivyotoka hapo ni kumuuguza na kumtoa vijiti mwilini......

pia nakumbua dada yetu mkubwa aliwahi kumpiga mdogo wake mama akamsemea mzee alimpiga then akampeleka kwe ng'ombe zizini akamwambia akae huko siku saba kwasababu anatabia za ng'ombe...kuna matukio mengi sana mfano akikupangia kazi usipifanya mfano ya shamba akirudi hata kama ni saa nne usiku utaenda kulima ...alikua anaogopwa mpaka na mabosi wake
 
[emoji1][emoji1][emoji23][emoji23][emoji23]mkuu huyu mzee bado yupo hai kwelii

amefariki mwaka jana akiwa na miaka 79.. ila mpaka uzee wake hadi wajukuu walikuwa wanamuogopa.. anacheza nao ila akiamua anawatia viboko..

kuna mjukuu aliua kuku wa nyama... mama anafuga kuku sasa kuna siku wanawapa kuku dawa kuna mjukuu akaenda kumkamata kuku wa nyama bahati mbaya akamnyonga mzee alikuwepo jirani akaenda mtia fimbo mjukuu hadi mama yake mke wa kaka akataka kulia... bro akamwabia kama unataka kulia kalilie chumbani maana mzee akikuona unalia hapa anaweza anzisha ugomvi mzito na usikanyage tena hapa
 
Mshua alinichapaga viboko mbele ya demu wangu alikuja kusuka.
Dingi amekuja mchana kula chakula akakuta hakuna maji hata ya kunawa mikono, kubabake alinichapa sticki hizo.
Demu wangu alikua nje anasukwa na dada yangu, dingi ananichapia sebuleni.
Kwa kuwa nilikua sitaki demu wangu ajue kama nachapwa, nikawa najikaza sipigi kelele.
Dingi akajua viboko havini umizi, akaanza kunipiga na mavibao, kubabake nilivimbaga mikononi.
Mara Paaaap nikatoka na mindoo kwenda kuchota maji, mialama ya viboko kwenye matako, mgongoni, mikononi.
2001 hiyo Kiloleni Tabora
Haaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
mzee wangu ukimtibua aisee anakua mkali kinoma

kwanza sitosahau tuko madogo tulikua na tabia ya kuzurura kitumbo waz bila ndala aisee halafu mzee alikua na cheo tu dah alikua anamind tunamzalilisha
siku hio akatuona live na mdogo wangu kama kawaida kitumbo wazi kufika home tunashangaa milango inafungwa tukajua leo kiama chetu kimefika akajikagua akaona hajavaa mkanda akaona hakijaharibika kitu aisee alituchapa ngumi na mikanda na mdogo wangu tangia siku hio mm ni tawiree tu
 
Back
Top Bottom