Wenye Magazeti anzisheni vyumba vya kusomea Mitaani

Wenye Magazeti anzisheni vyumba vya kusomea Mitaani

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Ni dhahiri kabisa kuwa kuja kwa teknolojia hakujaiacha salama sekta ya uchapishaji wa Magazeti, maana kwa sasa ni rahisi kwa mtu kupata taarifa papohapo tofauti na miaka ya nyuma.

Pamoja na changamoto hii yote lakini bado wapo watu wanaoamini na wanapenda kusoma Magazeti. Kama si Mgeni basi utakuwa unashuhudia Mkusanyiko wa Watu kwenye vibanda au meza za Magazeti, tena unakuta mtu ametulia akijaribu kupata chochote kilichoandikwa kwenye gazeti kwa taarifa iliyomvutia.

Nimeshuhudia mara kadhaa wenye Vibanda au Meza wakihangaika kuyalinda Magazeti yao yasichafuliwe au kushikwashikwa bila sababu kwa wengine kuweka Vioo juu ya Magazeti, na wengine huyapiga Magazeti pini (Stepler) kuyashikanisha ili Wasiohusika wasiyavuruge.

Nadhani ipo haja kwa Wenye Magazeti kukaa chini na kubuni namna bora zaidi ya kuandaa na kuuza Magazeti yao, haswa kwa kundi hili la Watu wa kipato kidogo ambao ni Wapenzi wa kusoma Magazeti. Wanaweza kuandaa vyumba au Vijiwe au Hema (tent) ambapo Mtu anayehitaji kusoma basi atalipa kiasi kidogo cha pesa, kwa mfano shilingi mia mbili ambapo atapata nafasi ya kupitia Magazeti Manne atakayoyachagua kwa muda maalumu mtakaokubaliana, kwa mfano nusu saa au dakika 40 n.k....na hapa kila Gazeti husika litapata mgao wa shilingi hamsini kutoka kwa Msomaji.

Bila shaka kuna uhusiano mzuri kati ya Wamiliki wa Magazeti na Wauzaji. Hivyo bado wanaweza kuwa Wawakilishi wazuri na Waaminifu.

Hii inaweza kufanyika kwa mfumo wa kopi ngumu (hard copy) au kopi laini (soft copy) ambapo kwenye banda kunaweza kuwekwa kifaa/tablet au smart TV ambapo Msomaji atakuwa ana 'touch' kupitia kurasa za Gazeti kwa muda aliolipia.

Bila shaka mtindo kama huu unaweza kupunguza hata gharama za kuchapisha kopi nyingi bila ya sababu na kwenda Mtaani kubahatisha Wateja...hapa zitaandaliwa kopi kadhaa kwa ajili ya Vituo maalum na kopi chache za kuuzia Watu wa maofisini, Majumbani n.k.

Mimi si Mdau wa uchapishaji wa Magazeti hivyo huu ni mtazamo wangu tu nikiamini Wahusika wao wanaweza kuwa na mawazo yao pia.
 
Umewaza vizuri napenda watu Kama nyie mnaoelewa haraka Nini maana ya ubunifu...ila kibiashara nadhani makampuni ya magazeti watakataa wataona unawakosesha pesa kwa kuwa nakala zinazouzwa zitakuwa chache
 
Kwanini tusiboreshe maktaba na hao wadau wapenda kuchungulia wakaenda huko (ila huenda hao ni watafuta story na vijiwe kuliko wasomaji) ingawa wazo lako wape wauza gahawa au zile kahawa na kashata mtu anunue magazeti yote na wateja wake wakija kunywa gahawa wasome bure...

Anyway magazeti profit ni through matangazo na matangazo mengi yanapelekwa kutegemea na circulation / wanunuzi kwahio gazeti moja likisomwa na watu mia moja ni vigumu mtoa matangazo kupata / kujua kwamba gazeti fulani linasomwa na watu wengi

Ingawa hao wapiga stapler waweka vioo wanaweza wakachukua wazo lako la kujiingizia kipato bila kuhusisha wamiliki... au kama vipi anzisha kibanda umiza cha wasoma magazeti
 
Kwanini tusiboreshe maktaba na hao wadau wapenda kuchungulia wakaenda huko (ila huenda hao ni watafuta story na vijiwe kuliko wasomaji) ingawa wazo lako wape wauza gahawa au zile kahawa na kashata mtu anunue magazeti yote na wateja wake wakija kunywa gahawa wasome bure...

Anyway magazeti profit ni through matangazo na matangazo mengi yanapelekwa kutegemea na circulation / wanunuzi kwahio gazeti moja likisomwa na watu mia moja ni vigumu mtoa matangazo kupata / kujua kwamba gazeti fulani linasomwa na watu wengi

Ingawa hao wapiga stapler waweka vioo wanaweza wakachukua wazo lako la kujiingizia kipato bila kuhusisha wamiliki... au kama vipi anzisha kibanda umiza cha wasoma magazeti
Maktaba zipo Moja kila Mji...Hapa nazungumzia chumba kidogo tu Mtaani ambapo ndipo Wasomaji wapo na ni kuwalenga Wasomaji wa Magazeti tu.

Hata kama kuna faida kupitia Matangazo vipi kama Gazeti litalipiwa na Watu wengi zaidi si ndio itapatikana pesa zaidi labda zaidi ya hiyo ya matangazo?. kila Mtu anapenda kupata zaidi...na kama ripoti itaonesha Gazeti fulani linapata Wasomaji wengi bado ni kipimo tosha kuvutia Matangazo.

Kuwahusisha Wamiliki ni ili wapate udhibiti na wanufaike na Kazi yao, na wao ndio wana nafasi ya kuwa na mtaji tofauti na Muuza Magazeti. Na hilo wazo la kuweka kahawa na kashata si wazo baya yaweza kuongezwa pia.
 
Wanasoma habari za michezo wanaangalia vichwa vya habari za michezo wapate cha kuongea vijiweni. Mtu anashindwa kununua chai ndo ataweza kununua gazeti
 
Wanasoma habari za michezo wanaangalia vichwa vya habari za michezo wapate cha kuongea vijiweni. Mtu anashindwa kununua chai ndo ataweza kununua gazeti
Sawa lakini Mimi nimeshajiridhisha kuwa kun Watu ni kama wapo addicted na Magazeti...na wakikosa hiyo access ya kusoma vichwa vya bure watatafuta mia mbili wakajinafasi zaidi...waweza usiwapate wote lakini walau nusu utawapata.
 
Wanasoma habari za michezo wanaangalia vichwa vya habari za michezo wapate cha kuongea vijiweni. Mtu anashindwa kununua chai ndo ataweza kununua gazeti
Watu wakisogezewa huduma na kurahisishiwa watashiriki tu.

Kumbuka hata wanaohitaji taarifa kwa njia ya simu bando zinapanda bei kila kukicha...hakuna bando chini ya sh 500 na kuendelea...sasa huoni hiyo 200 ni nafuu sana?.

Pia kumbuka hii itakuwa nafuu pia kwa hao Wachapishaji maana watapunguza idadi ya kopi ngumu za kusambaza.
 
Ni dhahiri kabisa kuwa kuja kwa teknolojia hakujaiacha salama sekta ya uchapishaji wa Magazeti, maana kwa sasa ni rahisi kwa mtu kupata taarifa papohapo tofauti na miaka ya nyuma.

Pamoja na changamoto hii yote lakini bado wapo watu wanaoamini na wanapenda kusoma Magazeti. Kama si Mgeni basi utakuwa unashuhudia Mkusanyiko wa Watu kwenye vibanda au meza za Magazeti, tena unakuta mtu ametulia akijaribu kupata chochote kilichoandikwa kwenye gazeti kwa taarifa iliyomvutia.

Nimeshuhudia mara kadhaa wenye Vibanda au Meza wakihangaika kuyalinda Magazeti yao yasichafuliwe au kushikwashikwa bila sababu kwa wengine kuweka Vioo juu ya Magazeti, na wengine huyapiga Magazeti pini (Stepler) kuyashikanisha ili Wasiohusika wasiyavuruge.

Nadhani ipo haja kwa Wenye Magazeti kukaa chini na kubuni namna bora zaidi ya kuandaa na kuuza Magazeti yao, haswa kwa kundi hili la Watu wa kipato kidogo ambao ni Wapenzi wa kusoma Magazeti. Wanaweza kuandaa vyumba au Vijiwe au Hema (tent) ambapo Mtu anayehitaji kusoma basi atalipa kiasi kidogo cha pesa, kwa mfano shilingi mia mbili ambapo atapata nafasi ya kupitia Magazeti Manne atakayoyachagua kwa muda maalumu mtakaokubaliana, kwa mfano nusu saa au dakika 40 n.k....na hapa kila Gazeti husika litapata mgao wa shilingi hamsini kutoka kwa Msomaji.

Bila shaka kuna uhusiano mzuri kati ya Wamiliki wa Magazeti na Wauzaji. Hivyo bado wanaweza kuwa Wawakilishi wazuri na Waaminifu.

Hii inaweza kufanyika kwa mfumo wa kopi ngumu (hard copy) au kopi laini (soft copy) ambapo kwenye banda kunaweza kuwekwa kifaa/tablet au smart TV ambapo Msomaji atakuwa ana 'touch' kupitia kurasa za Gazeti kwa muda aliolipia.

Bila shaka mtindo kama huu unaweza kupunguza hata gharama za kuchapisha kopi nyingi bila ya sababu na kwenda Mtaani kubahatisha Wateja...hapa zitaandaliwa kopi kadhaa kwa ajili ya Vituo maalum na kopi chache za kuuzia Watu wa maofisini, Majumbani n.k.

Mimi si Mdau wa uchapishaji wa Magazeti hivyo huu ni mtazamo wangu tu nikiamini Wahusika wao wanaweza kuwa na mawazo yao pia.
In Tanzania we need critical thinker like you it's a good idea
 
Watu tunatoka na taulo na mswaki asubuhi kwenda kusoma vichwa vya habari Mkwajuni kino alafu tunarudi kulala
 
Back
Top Bottom