Wenye mitaji hii fursa inasomeka

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Wazo la kuwa na kampuni ya private pension, wanachama wanapata malipo yao mara baada ya kustaafu.

Kushawish waajiriwa na wafanyabiashara kujiunga. Hata wale wenye pension kwenye mifuko mengine wanaweza kujiunga. Kwakuwa hii kampuni mpya pesa unapata mara tu ikiwa kulisha maombi, wakati unasubiri NSSF unakamata milioni zako kadhaa.
 
Wazo zuri lakini Bashite atakubali kweli watu binafsi waanzishe kampuni za pensions?
 
Na watakuwekea mikwara mingi wakati wanatafuta wawekezaji. Nime Ona katika nchi za magharibi watu waliochangia state pension na private pension baada ya kustaafu wanaishi vizuri.
Na hapo ndipo penye shida. Huku nje waweza ona mambo mengi tu ambayo ukiyaleta hom yanaweza kukuza uchumi na kuondoa umaskini kwa kasi kabisa na kuleta unafuu kwa watu. Shida ni kwamba sheria zetu zipo "too restrictive" na haziko "supportive" hata kidogo.

Kimsingi, kilichofanywa na kinachoendelea kufanywa na nchi zilizoendelea ni tofauti kabisa na tunachofanya. Sasa utajiuliza kama tunafanya tofauti tutafikiaje hayo maendeleo tunayoyahubiri? Bado tupo kwenye era za kubania bania kama wakoloni walivyokuwa wanatufanya.
 
Mkuu,
Haya Mashirika huanzishwa kwa sheria ya Bunge. Wale wabunge waliopitisha mstaafu kulipwa only 25% kwanza wakati wao Wabunge hubeba 100% at per sijui kama wataipitisha hii kitu ikifika kwao.

Wamekua muhuri wa kupitisha yasiyowapendeza Wananchi kisa tu Chama kimeamua, Ubinafsi ulioje sababu tu wao hawaguswi.
 
Inaweza kupitishwa kama mtamuahidi mkubwa mmoja hisa kwenye kampuni. Afrika mimi kwanza iko kila mahali. Kama wabunge wa kijani waliweza kupitisha sheria ya mitandao ya kijamii kwa milioni 10.
 
Social Security USA huitoi mpaka uwe above 64yrs.
Private (401k) ndiyo unaweza kukopa, ukakatwa kwenye mshahara kidogokidogo, kwa mwaka au 2yrs halafu ukalipa na kuendelea na maisha.

Pia, waajiri wengi huchangia dollar to dollar hadi 6%, wengine mpaka 4% ya income yako. Minimum wengi ni 3% ya income yako.
Ukikatwa 100$, muajiri anakuchangia 100$ sema huwezi kuzitoa au kuwa nazo mpaka uwe vested.

Kuwa vested inategemea, labda uwe umefanya 5,10 or 15yrs depending na mwajiri. pia unapewa option ya shares za kampuni kwa sababu 401k ni mchango wako Wall street.

Yaani hiyo fedha ya pensheni binafsi inakuwa invested Wall Street na wanakuonyesha spread yako every 3 months.

Najua watanzania wengi wanalalamika Social Security, ila hiyo huwa huchukui mpaka uwe mzee au kilema cha maisha.
 
Wazo zuri lakini halitekelezeki kirahisi.
Kumbuka sasa hivi wanataka BoT wasimamie vyama vyote vya kuweka na kukopa.

Hivi karibuni wameamua kuunganisha mifuko ya jamii ya mafao, sifikirii wataruhusu watu binafsi kufungua mifuko mipya.

Hata hivyo watanzania wengi hatuna utaratibu wa kujiwekea akiba. Ukikuta mtu amejiunga na saccos, analenga kukopa na sio kuweka akiba.
 
Wazo zuri lakini kwa bahati mbaya watawala hawawezi kuruhusu hilo litokee.

Kama wasivyoruhusu wanunuzi binafsi kununua,

- Korosho

- Kahawa

- Ufuta

Lengo ni mtu AFE MASIKINI wafurahi.
 
Tatizo huwa mnageuka na kutapeli watu na ni vipi utaaminiwa?
Kwanza sirikale haitakupa kibali
 
😱😱😱😱😱 Mtaji wake si wa mchezo mchezo
 
Financial Services Tanzania bado zipo kiholela sana kiasi kwamba inakuwa vigumu kwa watu binafsi kuwekeza kwenye financing. Technology bado hazipo up to date kivile, bado tupo nyuma sana almost Africa nzima bado technologies za financing hazipo well distributed kutuwezesha kuwa kwenye financing bussiness.

Finance inatawaliwa sana na sheria za kimataifa na sheria za nchi zilizoendelea. hela nying zinazotembea Africa hasa nchi zetu, siyo hela rasmi. Zipo kimchezomchezo.

Sasa kama Micro-finance ilivyokuwa shaghalabaghala , kweli mlitaka BOT isi-control microfinance?

Micro-financing ikirasimishwa itaongeza mpaka GDP yetu kwa wingi sana (lazima tuta rebase in a little while) kwa sababu sekta hii haikuwa rasmi kihvyo na ilikuwa inawanyonya wananchi na pesa nyingi zilizokuwa zinatembea zilikuwa chafu.

Ili tuwe included in Global Finance, lazima cha kwanza kabisa ni kurasimisha mzunguko wetu wa fedha. lazima tuwe na records.

Vitu vingine ni technocrats ndiyo huvianzisha. Siyo makada wa CCM. Vitu vingine tuwe tunavifanyia utafiti kabla ya kulalamika.
 
Wazo zuri katika mazingira yasio rafiki, mi nataka kuanzisha kampuni ya betting vipi utaratibu ukoje maana naona ndio fursa iliopewa kipaumbele awamu hii! Kampuni ikichanganya tunachanganyia na style ya biko ile ya kuchezesha draw kila week! Tukumbuke tu kuwa Jackpot Bingo ilianzishwa katika utawala wa Mkapa, hii inaashiria katika vipindi vigumu vya utawala ndipo hizi biashara za kamari huchipuka kama uyoga!
 
Wazo lako ni zuri mama, ila usisahau kuwa hizi kampuni zipo kwa mujibu wa sheria na kanuni ambazo unazitaka kufuata utaratibu wa aina moja......


Najua umeamua kubuni huo utaratibu kulingana na uhitaji uliopo kwa sasa.......ila ukweli ni kwamba haitawezekana maana sheria zilizopo hazitakuruhusua kuthubutu kufanya hivyo, maana nadhani unajua ikitokea hivyo tafasiri yke ni kuwa nchi nzima wafanya kazi watahamia kwenye huo mfuko na kuacha iliyopo ambayo inaendeshwa kwa utaratibu wa sasa unaokizana na unachosema......
 
Hivi Magufuli,watumishi wa umma walimkosea nini? Ikumbukwe yeye pia aliwahi kuwa mtumishi wa umma
Mpaka sasa bado ni mtumishi wa Umma,ni kiburi tu cha madaraka.
Dhuluma kubwa sana hii.
 
Mifuko ya Pensheni za serikali ni lazima. Nchi zote duniani.
Pensheni binafsi kwa sasa hivi zinawezekana kama sheria hii mpya ya Microfinancing itatengenezewa regulations nzuri. Itabidi mtu ununue pensheni binafsi kutoka Benki au hata SACCOS.
Hii imerruhusiwa (kama sikosei kwenye microfinance act).

 


Mkubwa unelewa maana ya kulalamika? Makada wa chama wanatoka wapi kwenye bandiko langu?

Nimegusia kuhusu usimamizi wa BoT kwa microfinance zote.
Ninaeleza kwamba mifuko ya pension inaanzishwa na kusimamiwa kisheria, ndio maana bila kujali mwajiri wako ni serikali au sekta binafsi, lazima uwe kwenye mpango wa kujiwekea akiba ya uzeeni.
Nikamalizia umuhimu wa watu kuwa na utaratibu wa kujiwekea akiba.

Sijaona mahali nikilalamika wala kutaja chama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…