Sokoro waito
JF-Expert Member
- Nov 21, 2014
- 2,201
- 2,599
Basi nilikuwa nimekuelewa vingine. Maana aya ya Kwanzaa ulivyosema sio rahisi halafu ukaunganisha BOT Nikadhani unamaanisha BOT ni kikwazo.Mkubwa unelewa maana ya kulalamika? Makada wa chama wanatoka wapi kwenye bandiko langu?
Nimegusia kuhusu usimamizi wa BoT kwa microfinance zote.
Ninaeleza kwamba mifuko ya pension inaanzishwa na kusimamiwa kisheria, ndio maana bila kujali mwajiri wako ni serikali au sekta binafsi, lazima uwe kwenye mpango wa kujiwekea akiba ya uzeeni.
Nikamalizia umuhimu wa watu kuwa na utaratibu wa kujiwekea akiba.
Sijaona mahali nikilalamika wala kutaja chama.
Basi nilikuwa nimekuelewa vingine. Maana aya ya Kwanzaa ulivyosema sio rahisi halafu ukaunganisha BOT Nikadhani unamaanisha BOT ni kikwazo.
True.Hapana mkuu, pia nakushukuru kwa ustaarabu wako. Ningoga matusi yanivurugie Jumapili kama usingekua mtulivu na mjenga hoja makini.
Zamani hata makampuni ya simu yanayotoa huduma za kifedha hazikua zikisimamiwa na BoT, siku hizi wametoa mwongozo na sera za usimamizi.
Umuhimu wa kurasimisha hii mifumo una manufaa sana. Kwanza kuhakikisha pesa iliyopo kwenye hiyo mizunguko inakuwa na usimamizi pia kuzuia utakatishaji wa pesa haramu. Kuna watu wamewekeza mabilioni ya pesa kwenye biashara za kukopeshana hauwezi kuwahusianisha nazo kirahisi.
Kingine serikali inapoteza mapato kutokana na kodi kwa hizo taasisi kutokurasimishwa.
Wakifanikiwa vizuri zoezi la usimamizi, ni rahisi kupanua wigo wa huduma kwa wanachama/ wateja kutumia akiba zao kwenye fursa zingine zilizo rasmi.
Mwisho kabisa, licha ya wengi wetu kutokuupenda huu utaratibu, pension lengo lake ni kumsaidia mwanachama anapostaafu au kupata ulemavu wa kudumu unaomzuia kufanya kazi. Huo ndio ukweli mchungu.
Wazo jema, jinsi ya kutekeleza sasa, hata kama unao huo mtaji.Wazo la kuwa na kampuni ya private pension, wanachama wanapata malipo yao mara baada ya kustaafu.
Kushawish waajiriwa na wafanyabiashara kujiunga. Hata wale wenye pension kwenye mifuko mengine wanaweza kujiunga. Kwakuwa hii kampuni mpya pesa unapata mara tu ikiwa kulisha maombi, wakati unasubiri NSSF unakamata milioni zako kadhaa.
Katika nchi kama kenya, ghana n.k mifuko hii ya private ipo kisheria na inasajiliwa uchangiaji ni wa hiari lakini imeleta faida sana kwa nchi na wananchi. Hizo private fund zinatumia michango kuwekeza kwenye miradi yenye tija na yenye faida na wanachama wanapata faida wakati wa kuchukua mafao yao ambayo wanaweza kuchukua wakati wowote. Nchi hizi kiwango cha kuchangia mifuko ya lazima haizidi 10% hiyo inampa mtu nafasi ya kichangia private sasa hapa kwetu ukishachangishwa 20% utaweza kuchangia tena private fund?Wazo la kuwa na kampuni ya private pension, wanachama wanapata malipo yao mara baada ya kustaafu.
Kushawish waajiriwa na wafanyabiashara kujiunga. Hata wale wenye pension kwenye mifuko mengine wanaweza kujiunga. Kwakuwa hii kampuni mpya pesa unapata mara tu ikiwa kulisha maombi, wakati unasubiri NSSF unakamata milioni zako kadhaa.
Nchi nyingine pesa hizi hukopeshwa tena serikali kujengea hospitali shule na miradi mikubwa ya maji. Inschangia kuleta maendeleo haraka kwa wananchiKatika nchi kama kenya, ghana n.k mifuko hii ya private ipo kisheria na inasajiliwa uchangiaji ni wa hiari lakini imeleta faida sana kwa nchi na wananchi. Hizo private fund zinatumia michango kuwekeza kwenye miradi yenye tija na yenye faida na wanachama wanapata faida wakati wa kuchukua mafao yao ambayo wanaweza kuchukua wakati wowote. Nchi hizi kiwango cha kuchangia mifuko ya lazima haizidi 10% hiyo inampa mtu nafasi ya kichangia private sasa hapa kwetu ukishachangishwa 20% utaweza kuchangia tena private fund?
Faida kubwa zaidi ni kuwepo mitaji kwenye hizi private fund inayotumika kwa tija sio hapa yanajemgwa magorofa marefu yaliyotupu miaka nenda miaka rudi.