Wenye Nyumba kaeni kitaalamu: Kama mpangaji wako atakutwa na dawa za kulevya nyumba yako itataifishwa!

Hawa wapuuzi kuna wakati wanalewa madaraka na kuropoka ovyo kama watu waliokula madawa ya kulevya. Huyo aliyetamka hayo maneno inawezekana naye amelewa madawa ya kulevya. Akamatwe apimwi madawa mwilini mwake.
Kabla hajapanda kwenye podium lazima ashtue Embassy km 3/4 hivi na akisema Embassy nazo ni dawa za kulevya basi yeye atakua wa kwanza kukamatwa na kuwekwa ndani

Daktari anakataza watu wasivute Sigara ila kwenye mfuko wa Shati ana paketi la Sigari au anakataza watu wasinywe pombe ila kwenye draw kahifadhi Kisichana (bapa ndogo)
 
Nyumba zangu za kupangisha Kuna kupengele Mali ya mpangaji ni yake haisiani na mwenye nyumba hata ulinzi WA Mali zake ni juu ya mpangaji mwenyewe,Sheria ya Lyimo inakinzana na masharti ya wapangaji wangu
Kwanza kitendo cha kupokea kodi tu kutoka kwa mpangaji, hiyo nyumba si mali yako tena hadi pale kodi itakapo kwisha,ndiyo nyumba inarudi kwa himaya yako na unaweza hata kuingia ndani saa yoyote ukitaka!!
 
Biashara ya nyumba za kupanga, ni changamoto kwa baadhi ya maeneo na kwa baadhi ya wapangaji wasio waaminifu coz anaweza fanya tukio huko au nyumba yako ikahifadhiwa vitu vibaya kama hilo angalizo.
Kila sehemu kuna watu waaminifu, na wengine siyo waaminifu, halkadhalika wapangaji! na hadi huko serekalini wapo pia!!
 
Huyo kamishina hapo atasababisha watu wadhulumiwe nyumba zao na pia ametengeneza mianya ya rushuwa

Watu wenye elimu iliyokamilika hawawezi kutunga Sheria kama hiyo
 
Kijana yupi mkuu?
 
Kwamba ukiweka hicho "kipengele" kwenye mkataba halafu mpangaji akakutwa na bangi au heroine ndani ya hiyo nyumba wataacha kuitaifisha?

Hapo dawa ni kuipinga hiyo sheria ya hovyo ifutwe (kama tayari ipo), ila wakiipitisha huwezi kuzuia utekelezaji kwa kigezo cha Mkataba.

Watawala walishagundua kuwa raia ni wapole, watawaonea sana hadi watakapozinduka
 
Yes, atleast hapo unaweza kupata som sort of proof kwamba mwenye nyimba alikuwa anajua, lakini, nado nayo ni rahisi kukana, maana atasema yeye huwa haingii kukagua vyumba vya wapangaji..
 
Mpangaji endapo amekutwa na Madawa anabidi kuwajibika kupitia Makosa yake yeye mwenyewe.

Sasa ikiwa nchi imekosa watu wenye uwezo mzuri wa kufikiri Kwa kina inatia mashaka Sana .

Wanachukulia mambo kiuwepesi Sana kiukweli.
 
Kuna baadhi ya Sheria, kabla hazijapitishwa huwa wanakusanya maoni ya Wadau

Nafikiri kwenye hii Sheria, hawakufanya hivyo

Nafikiri kuna haja tuombe amendment.

Kwasababu halitamgusa mtu mmoja, bali wote

Maana hata Wabunge wanazo nyumba za kupangisha
 
Tz, roho mbaya, daima kutunga sheria za kukandamiza na kuumiza WaTz! Madawa yamekutwa ndani ya Tz, je nchi itaifishwe, maana kama mamlaka mmeshindwa kuyadhibiti, mna kwenda kukomoa Mtz asiyehusika na madawa! Serikali mmeshindwa kazi!
 
kwa mwendo huu polisi ccm watamiliki nyumba za kisasa kabisa
 
Ukishaikamata nyumba, jaribu kutafuta uhusiano wa mwenye nyumba na hiyo biashara,KAMA HAKUNA UHUSIANO MRUDISHIE MWENYEWE NYUMBA YAKE.

Mtu kakupangisha anakwambia ni muajiriwa taasisi fulani na umethibitisha hilo au mfanyabiashara Kariakoo na umethibitisha hilo suala la yeye kuuza madawa ni la siri na NI mamlaka za usalama tu zinazoweza kugundua.
Nina office apartments na mtu kaja kapanga kwa kazi fulani na ana leseni nayo na analipa Kodi, mamlaka zimemkamata kwa biashara yake ya gizani, Mimi nahusikaje?
 
KWa huu mwendo itabidi tutaifishe nchi yenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…