Wenye Nyumba kaeni kitaalamu: Kama mpangaji wako atakutwa na dawa za kulevya nyumba yako itataifishwa!

Kuna sheria na Mwana sheria tutakutana mahakaman

Kuna sheria gan inampa kibari mwenye nyumba kuwa anaenda kukagua kila sku kwa mpangaji wake
Ni sheria gan inaniruhusu kuingia nyumban kwa mpangaji wangu na kuingia vumbani kwake kumkagua km anatunza madawa

Kwa ujinga huu tutakutana mahakaman na uyo mkurugenzi wa madawa
 

Tanzania nchi yahovyo sana kuishi ukiwa raia wa kawaida, ila kwa watawala ni nchi poa sana maana unanyonya kwa mrija tuu.
 
Na kuna sheria nyingine ya wizi tuu. Inahusu wanaochimba visima vya maji. Yaani wewe umejenga sehemu ambayo huduma ya maji haipo unajikoki unaona si vyema familia iteseke, unaingia gharama kuchimba maji kwa mamilioni mengi sana kupata underground water. Umefanikiwa kupata maji mita 100 chini ya ardhi. Unatakiwa kulipia drilling permit (hiyo sikatai). Ila sasa umeanza kutumia maji unaambiwa kila mwaka uwe unalipia kodi/ushuru. huu ni wizi kama wizi mwingine. Serikali inashindwa kufikisha huduma ya maji kwa wananchi, anatokea mwananchi anaingia gharama kubwa (ambayo serikali ilipaswa kubeba). badala ya mwananchi huyu kusaidiwa ndo anakandamizwa. Mtu anatumia milioni 15 hadi 20 kwa ajili ya maji tuu, pesa ambazo zingemkwamua huyu mwananchi from other problems lakini badala ya kusaidiwa anakandwa zaidi
 
Hii inafanana na ile ya gar yako ikishikwa imebeba madawa inataifishwa
Sasa mm nimebeba misokoto yangu 10 ya bangi naenda kuenjoy polisi kakushika kakuta bangi kwa gar unataka utaifishe gar yangu ya million53 kwa bangi za elf10 huu ujinga nani atakubari
 
Gari sawa ila kwa nyumba nadhani hii sheria wangeiangalia upya. Mfano mimi nina nyumba masaki na ninaishi njiro arusha. Nyumba ya masaki nimempangisha mtu, je ni jukumu langu tena kuwa naenda kumkagua huyo mpangaji kila siku kuona ni nini kiko ndani ya nyumba? Vipi kuhusu sheria ya faragha na haki binafsi za huyu mpangaji?
 
Kuna sheria na kuna maneno ya jukwaani

Ata jiwe alisema wamachinga waweke biashara zao popote pale ila akuwawekea sheria ya kuwarinda bali aliongea stejini km mwana siasa tu
 
Mahakama gani hiyo?
Labda ingekuwa Mahakama za nchi nyingine zonazotenda haki. Ukileta ubishi utabambikiziwa kesi ya uongo tu kuwa na wewe umekutwa na madawa ukatulizwe ndani huko
 
Ujaelewa mchezo uliopo apa ,shida sio kazi aliyonayo mpangaji shida ni kosa la mpangaji maafa makubwa unapata ww mwenye nyumba
 
Kwanini MWANANCHI apewe tabu katika Taifa lake lililo na UWAZI NA UKWELI unaohubiriwa na viongozi wake?

Nini maana ya viongozi wa serikali ya mitaa ? Tunakwenda kufanya CHAGUZI kwa ajili ya nini?

Sheria hii IBADILISHWE iwe ya kwanza KUTAMBUA nguvu za viongozi wa mtaa!! AMBAO tunaishi nao! WASIMAMIE mikataba ya upangaaji na wawatambue WAPANGAJI kwani jukumu la usalama linasimqmiwa na wao.

Ukijenga kwa haki huwezi tamka sheria hii.
 
Ujaelewa mchezo uliopo apa ,shida sio kazi aliyonayo mpangaji shida ni kosa la mpangaji maafa makubwa unapata ww mwenye nyumba
Nimeelewa sasa Mkuu, hapo ni kama Kuna mtego mtu ametegewa ili kumnasa

Ukiwa na Bunge linalojitambua, hawawezi kupitisha Sheria za hovyo za namna hii, bahati mbaya huku kwetu Wabunge wetu hawako pale kutusaidia Wananchi wake, isipokuwa Serikali 🙌
 
Inaskitisha sana...

Inabidi wapangaji kuanzia sasa wawe na Police clearance Certificate, ili uweze kupanga nyumba...

Ili wakibainika wana magendo haramu mwenye nyumba hausiki...


Cc: Mahondaw
 
Hata misokoto miwili ya bangi? Je,dawa ikikutwa kwenye nyumba ya serikali?
 
Nyumba ya kupanga si mali ya mwenye nyumba waache ukuda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…