Wenye 'sheli' waiba mafuta ya wateja

Wenye 'sheli' waiba mafuta ya wateja

kama kuna mijitu mijizi mikubwa bi ewura. inakusanya ewura levy toka kwa wananchi, hakuna inachofanya sanasana ni kutafuta kuongea kwenye vyombo vya habari. kukuta pump 15 zinatatizo mpaka wanaqita mkutano na waandishi wa habari. seria zao zimekaa kinyume nyume. samahani jamani kwa kutumia lugha kali. nitawapa mfano wa mambo ya kupuuzi ambayo mamlaka hii inafanya. wanapita kukagua mafuta vituoni, ni kweli wanakuta diseli iyochanganywa na mafuta ya taa, wamtoza faini mwenye kituo- hilo ni jambo jema, baadae wanatangaza kwenye vyombo vya habari- hilo ni jema zaidi. lakini ikumbukwe mafuta husika tayari hayana uboa wa kutumika kwenye magari,na yayaendelea kuuzwa kituoni. nilitarajia kwa mamlaka yenye kufanya kazi ka umakini wangehakikisha hayo mafuta hayatumiki tena kwa magari. wangehakikisha yanapelekwa nyenye matumizi mengine ya viwanda . kuacha mafuta hayo yatumike tena ni hujuma kali kwani wananchi wanachangia uendeshaji wa ewura ili wapate huduma, na hawana msaada wowote wa ewura
 
Mchezo huu mara nyingi hufanya na waajiriwa kwa lengo la kujipatia hela zao binafsi mbali na mauzo halali.

EWURA hawatakiwi kukaa ofisini sasa, yaani suala la ukaguzi liwe ni part and parcel ya majukumu yao ya kila. Wawaajiri wataalamu wengi tu, kwani EWURA inaweza kuongeza mapato yake na kuwalipa vijana kazi wake kutokana na fine za kila siku. Mpaka hapo watu watakapojua kuwa ukiiba robo lita ukakamatwa utatakiwa kulipa lita elfu moja fine.
 
Thanks, lakini EWURA wanatakiwa kufanya vitu hivyo kila mahali, wasilazwe usingizi na visenti wanavyokatiwa kwa lila lita inayouzwa ambayo inadaiwa inaenda Ewura. Kila mahali ni wizi mtupu. Enzi za Mwalimu wizi huu usingekuwa story ya magazetini bali tungesikia watu wako lupango kuisaidia polisi. EWURA hawana meno kwa sababu hawawezi kuukata mkono unaowalisha.

Leka
 
jamani mnasahau sana mizi mitano iliyopita watu waliandamana mafuta yamepanda; jamaa wakashusha ila bei waliyo kuwa wakilalamika watanganyika ndiyo ile ile; ila imepanada kidogokidogo watanganyika hawalalamika na hata wahusika wa udhibiti wako kimya hii inaonyesha ni kiasi gani wahusika kwa kiasi kikubwa katika hili
 
Broda..are you serious with this thread?

Shell is a company and a well respected one.Thread ingetakiwa iwe "Wenye vituo vya kuuzia mafuta...." rather than wenye Sheli.Pengine ndio maana Invisible ameweka ' ' ili kuonyesha ni jina ambalo limezoeleka miongoni mwetu.
 
nafikiri na sisi wateja tuisaidie hao jamaa wa vipimo, kwa kununua kwenye galoni ili mtu uweze jua kweli hii ni litre tano au sio , maana vituo vilivyoko tanzania ni vingi na mpaka hao jamaa wavipitie na wengine wanakuwa compromised itachukua muda mrefu.
 
Imeandikwa na Halima Mlacha;
Tarehe: 15th December 2009
HabariLeo


Kwa mujibu wa Kimaro, pampu nyingine zimefungwa katika kituo cha BP kilichopo Kimara Suka baada ya wakaguzi kuwakuta mafundi wakizitengeneza na EWURA hawakuwa na taarifa.

.
...Nilikua nikisikia kua sio vituo vyote vya mafuta vyenye nembo ya "BP" vinauza mafuta safi na halali sasa nimeamini....Kweli nchi hii inaenda pabaya watu wanajali ubinafsi zaidi ya kufanya biashara halali. Hebu fikiria mtu unaacha mafuta ya bei rahisi unaenda mahali kama BP ukitegemea quality and value halafu wanakufanyia ujanja ujanja.Inauma sana aisee..

Kwa upande mwingine vituo vingi kama sio vyote vya mafuta wanafanya biashara kama wakala wa kampuni za mafuta mf.BP,Total,Oilcom etc. Hizo kampuni za mafuta haziwajibiki kisheria kukagua hao wakala wao? Kwenye biashara kuna kitu kinaitwa 'brand' na kuichafua 'brand' ni kosa kubwa sana..sasa sijui wao wakishauza mafuta kwa mawakala wanaishia hapo au la..
Nawasilisha.
 
Hii michezo ya Pump nadhani ni Tanzania nzima , Na si kama ni issue ngeni sana..! Nakumbuka nilikuwaga na Nyoka wangu kwenye Pump za BP za Tangi Bovu..!

Alikuwa ananieleza kwamba katika vituo vya mafuta kuna michezo mingi michafu , akasema zipo pump mahususi kwa shughuli hiyo ya kuwapunja wateja na zingine ambazo zimechanganywa kati ya Diesel na mafuta ya taa..! Sasa mchezo ni kwamba unapoingia na usafiri wako wakikuona wewe mzee wa kusinzia wanakuita kwenye zile pump feki na kukupa mambo..!!

Wakiona kidogo una kawelevu wanaweza wasikufanyie ujanja huu..!! Natumaini wale waheshimiwa wenzangu wasiopenda kusumbuka na kushuka ndani ya magari yao wakati wanapimiwa mafuta michezo hii itakuwa imewakuta sana !!!
 
Kwa ushauri wangu nadhani sasa ni wakati muafaka wa mipira ya pampu za mafuta iwe colorless na sio rangi nyeusi kama ilivyo sasa kwani wanatuibia sana, loh.
 
Kwa ushauri wangu nadhani sasa ni wakati muafaka wa mipira ya pampu za mafuta iwe colorless na sio rangi nyeusi kama ilivyo sasa kwani wanatuibia sana, loh.

Au ikibidi itabidi tuwe tunaenda na vidumu. Unawekewa kwenye kidumu cha lita tano nawe unaenda kumimina kwa tenki ya gari!
 
au ikibidi itabidi tuwe tunaenda na vidumu. Unawekewa kwenye kidumu cha lita tano nawe unaenda kumimina kwa tenki ya gari!
wajanja wote, haswa madreva teksi ndio wanafanya hivyo kuepuka kuibiwa.
Tatizo sisi utakuta ndio hivyo unasukuma mkoko vx v8 halafu uende na kidumu sheli kisa kuibiwa mia 500 tu!!, loh. Tunakufa na tai shingoni.
 
Au ikibidi itabidi tuwe tunaenda na vidumu. Unawekewa kwenye kidumu cha lita tano nawe unaenda kumimina kwa tenki ya gari!

Madereva wa taxi walishafanya ugunduzi huo zamani. Ukiwauliza watakujuza ni pamp ipi imefanyiwa usanii na ipi iko sawa. Jamaa wanaweka moja kwa ajili ya EWURA.

Kuna mwanajamii kaelezea kuwa waTZ wote ni wezi kuanzia kutolipa Maji, Umeme n.k. Mimi kwa upande wangu nimefanya utafiti na kugundua kwanini watu wanakuwa na tabia hizo. Upande wa umeme hasa juu ya "Unjustified Billing" Kwanza TANESCO wanasema unit moja ni shilingi 128. Lakini ukweli ni kuwa unit moja ni shilingi zaidi ya 220/= Juzi nilitoa 20,000/= nikapewa unit 91 tu. piga hesabu. Ukitoka hapo ndipo unapotafuta kishoka aondoe kadhia hii. Hakuna haja ya kuongopea watu, waambiwe bei halisi ili wapange bajeti na siyo uhuni eti ni VAT, EWURA, REA, Fixed cost etc. Wanatoza VAT mara mbili mbili bila aibu. Mbona kwenye bia wauza 1400/= wakati kuna madai kuwa zaidi ya nusu ni kodi? kwa nini wasiseme kuwa ni 700/= kwenye matangazo yao?!!

Ukitaka kuunganisha umeme usiseme utapigiwa hesabu za kihuni hadi ushangae. Screw moja 20,000/= vikombe 20,000/= wakati screw zauzwa tabata 2,000/= moja, Waya mita moja 3,000/= in general nguzo moja hadi kwako ni Tshs 1,200,000+. Wakishamaliza wanadai utie sahihi kuwa hiyo ni mali ya TANESCO. Hii haiingii akilini hata kidogo ni WIZI hivyo vishoka wataendelea kuwepo tu. Kumbuka " For every action there is an equal (sometimes greater?) and opposite reaction"
 
invis
GOOD NEWS BR;ILA KWA USHAURI TU NAPENDA KUKWAMBIA HAWA EWURA NAO WEZI MATAPELI WA KUTUPA NDUGU YANGU ,KUNA KAKANGU NAKAA NAE NI MMOJA WA WANAOFANYA INSPEC HAKIKA AKILEWA NA KUANZA KUONGEA UNAWEZA UKAAMUA KUWEKA MAJI KWENYE GARI YAKO,....HAWA MAFUNDI WANAOKUJA KUTENGENEZA HIZO PUPM EWURA WANAJUA HILI NA WAKIFIKA WANAINGIZWA KWENYE CHUMBA CHA MAPATO NA MATUMIZI KWENYE SHELL WANAKATIWA WANAONDOKA NA SI CHINI YA LAKI MOJA MPAKA MBILI KILA MMOJA,....NAPENDA KUWEKA WAZI HILI NIKIJUA HILI NI UMIZO KWA WATANZANIA WENGI,....ZIPO SHELL NYINGI NAWEZA KUWATAJIA KWA MDOMO WAKE ANAZITAJA./////NIANZE NA ZILE ZA SINZA TUNAZOKIMBILIA ZA 1400/1300 PET/DIES NDUGU ZILE KILA LITA NNE MASHINE INAFINYA MOJA,...YAANI UKILIPA YA LIT 4 ZIMEINGIA TATU UJUE,...NA HII NI MCHEZO MICHAFUINAYOJULIKANA NA EWURA WANAIJUA SANA WANACHOFANYA UKIWAONA WAMETULIA MAOFISINI UJUE WANASUBIRI MWISHO WA MWEZI KUZIPITIA SHELL HUSIKA NA KULIPWA KAMA MISHAHARA YAO./////HAKIKA WATANZANIA TUTAENDELEA KUUMIA LABDA NYERERE ARUDI
 
...

Sasa huo mchezo wakuibia wateja kwenye Petrol station ni jambo sugu nnchi nzima , hawaogopi kwasababu faini zao ni mchekea,...

Ni kweli kabisa, mchezo huu mchafu ni wa siku nyingi sana.
Kwa utafiti wangu,
1. Kutoka Mlandizi hadi Kibaha maili moja (pale mizani), umbali wa kilometa 29, kuna vituo vya mafuta 31! Hapa sijahesabu vipya ambavyo bado havijakamilika!

2. Kutoka makutano ya Barabara za Bibi Titi na Morogoro (pale DIT) hadi Ubungo mataa, makutano ya Mandela/Morogoro na Sam Nujoma kuna vituo vya mafuta visivyozidi 10 ilhali magari ni mengi sana kwa njia hii!
Cha kushangaza sasa, magari ya Kibaha-Mlandizi hii si mengi kama ilivyo kwa Dar, lakini ni eneo ambalo lina vituo vingi sana vya mafuta huenda kuliko mahali pengine nchini, kwa umbali mfupi namna hiyo!

3. Justification ya hali hii ni kwamba hawa wamiliki wa vituo hivi vya mafuta mkoa wa Pwani wanachanganya mafuta ili bei ziwe chini wapate wateja wengi.Na ukiangalia bei zao ziko chini sana kuliko vituo vingi vya Dar!

Imeandikwa na Halima Mlacha;
Tarehe: 15th December 2009
HabariLeo


.....Ewura imefunga pampu 15 , Dar es Salaam, baada ya kubaini kuwa wahusika 'wamezichezea' ili zitoe mafuta pungufu.
.....


....na ukitaka kugundua upungufu huo wa mafuta, uende kununua ukiwa na galoni ya plastiki ambayo ni angavu (transparent), huwa wanachukia sana. Aghalabu ukiwa na chombo cha namna hiyo huwa wanakuelekeza kwenda kujaza mafuta kwenye pampu yao nyingine (ambayo haijachezewa mchezo mchafu) ili wasigundulike kwamba wanapunja wateja! Wanaoibiwa sana ni wale wanaojazia mafuta katika magari moja kwa moja (huelekezwa kwenye pampu zilizochezewa!...

hii khabbari imeniskitisha sana hii. nitahakikisha waziri husika anajiuzulu. fuatilieni sana taarifa za khabbari. senksi sana mleta mada kwa kufichua huu uzembe dume.

Kujiuzulu Tanzania? Thubutu!
Bro, kwa Tanzania ninayoifahamu mimi, waziri (Willy Ngeleja) HAWEZI kujiuzulu kwa ishu "ndogo" namna hii. Mabomu yameua watu kibao Mbagala na bado waziri Mwinyi anapeta madarakani. Kuna watu wamekunywa maji ya sumu kutoka mgodini kule Mara wakafa, na bado waziri anapeta, sembuse kuchanganya mafuta?


SHELL ndiyo ilikuwa kampuni ya mwanzo mwanzo kabisa kusambaa hapa nchini nafikiri kabla ya BP na nyinginezo hivyo waswahili walitohoa neno la SHELL na kufanya kama ndiyo kituo cha mafuta

Asante kwa kumbukumbu hizi Kimbweka, kumbuka pia kwamba tumebadili:-
1. Majina ya mifuko ya plastiki na kuita 'Rambo", kwa sababu mifuko ya mwanzoni mwa 1990 ilikuwa na picha ya mcheza sinema Rambo (S.Stallone)
2. Mifuko ya kubebea mbolea kule kwetu inaitwa 'Salfeti' hata kama imebeba sukari ama chumvi (ilitumika kubeba mbolea za sulphate). Dar wanaita viroba
3. Kule Tanga kila piki piki ni "Honda" hata kama ni Harley Davidson au Yamaha, nk.

Regards,
Idimi
 
Kwa ushauri wangu nadhani sasa ni wakati muafaka wa mipira ya pampu za mafuta iwe colorless na sio rangi nyeusi kama ilivyo sasa kwani wanatuibia sana, loh.

Mkuu nakubaliana na wewe sana, kwa nini iwe na rangi nyeusi kama sio wizi mtupu!
 
upuuzi huu wanafanya hadi kwenye premium unleaded petrol?!what about BP za posta?!
 
Back
Top Bottom