Unaweza kufuata njia hizi,kwangu siku zote zimefanikiwa kwangu.
-Kunywa maji ya moto asubuhi changanya na ndimu glass kubwa
-Chai yako achana kabisa na chakula cha wanga na sukari isahau,soda acha kabisa ,hata coke diet
-Chai waweza kula protein kama mayai,sosage,bagia za kunde,dagaa,samaki,supu ya nyama isiyo na mafuta
-Mchana usile kabisa wali wala ugali,kula tu protein,mayai ya kukaanga,mboga,nyama isiyo na mafuta,maharage,ndizi
-Usiku usile kabisa chakula cha aina yoyote ya wanga
-Beer isahau kabisa
-Jitahidi kuwa na mazoea ya kutembea,kupanda ngazi badala ya lift
-Ukiweza kufanya mazoezi ya kunyanyua vyuma kdg,au push up itasaidia kupungua haraka kwani unatumia nguvu nyingi
hapo usipopungua unayo shida,epuka kukaa njaa,kula chakula sahihi.
Karanga pia ni snacks nzuri iwapo una njaa
Kila la heri