Wewe ni muhimu sana kwangu, naomba ushauri wako

Wewe ni muhimu sana kwangu, naomba ushauri wako

kwanza pole sana mwanaJF mwenzangu kwa kusitisha masomo kwa sababu iiyo nje ya uwezo wako. hakika wakati wa MUNGU ukifika hakutakuwa na kikwazo cha wewe kusonga mbele. kwa mtaji wa 1M ni mkubwa sana na pia nakusifu kwa kujikusanya mpaka kufikia kiasi hiko kingi. kuna mdau kashauri uende shamba, YES ni wazo zuri lkn kama huna ardhi, chanzo cha maji na pembejeo nyingine ni bora kwanza ukakuza mtaji wako ama ukau-reserve huo ushauri manake safari inaweza kuishia njiani kama huna hivyo vitu tajwa hapo juu.. lakini pia kuna mdau kakushauri ufuge napia huu ni ushauri BOMBA sana lkn pia kama huna BANDA ama sehemu ya kuhifadhia mifugo yako, ni vigumu (kama uko nyumba ya kupanga) sana kuendesha hii biashara. sasa iko hivi ..HUMU jf kuna watu wenye upendo na moyo wa kujitolea mawazo mbali mbali juu ya kuinuana na kadhalika. sasa basi mimi nakushauri chukua ushauri lkn uchuje na kuona kipi unaweza kufanya kulingana na STRENGTH yako kimtaji. Kuna mdau pia kashauli ujihusishe na kibanda cha chips pia ni ushauri mzuri sana...

nakutakia kila la kheri na MUNGU akuongoze katika kutimiza ndoto yako BROTHER
Asante sana brother kwa kunitia moyo hakika Jf kuna kila aina ya watu
remain blessed broo[emoji120] [emoji120] [emoji120]
 
Asanteni Sana [emoji120][emoji120][emoji120]
 
Nimependa uwasilishaji wako wa hoja.Unaonekana u mkweli.Ushauri wangu kwako ni huu,usijiingize katika biashara/shughuli hata ukiambiwa inalipa sana lakini wewe huipendi,usianzishe shughuli au biashara kama hairuhusiwi na Serikali au imani yako,usiweke mahali itakapokufanya uvunje sheria.

Kama una moyo wa uvumilivu na subira Millioni moja ni mtaji mkubwa. Ninaweza kukushauri vizuri kwenye maeneo mawili.Kilimo au ufugaji,ukikubali ninakushauru awamu ya kwanza usitumie zaidi ya 600,000/= ili upate uzoefu na kujifunza changamoto na fursa halisi.

Yapo mambo ya kushauriwa nje ya jukwaa.Ushauri ni bidhaa,nitautoa kwako kama sadaka yangu kwa MUNGU
Nimeupenda ushauri wako mkuu
 
Kila kitu ni risk,,maisha ni risk,biashara ni risk,kilimo pia,na kila aina ya vitu vina risk yake. So na bila risk maisha hayawez kua mazur au kuipima akil yako vzr.

Pole sana dogo ila tu hajatuambia uliipataje hyo milion 1 labda ulipiga deiwaka au uliiipata pata vip,,so sio ishu sna ila ishu ni kwamba,unataman kufanya biashara ila unaogopa isipokulipa kwa wakat mtaji utaisha**

Unataka kuwekeza huku hela uendelee kuiona ili usiwe na hofu ya kupoteza hela yako ambayo umeikusanya kidgo kdgo,hali hyo hutokea kwa yyte yule ambae anaanza kuwekeza kwa cchte kwa mara ya kwanza.

Dogo mimi nilianza biashara kwa shng 8000 ( elfu nane) miaka kadhaa nyuma nadhan wewe ukiwa shule ya msingi,lakin leo nauwezo wa kuagiza kontena 40 ft kutoka china, so milion ni kubwa sanaaa dogo wala usiogope wala kuwa na wasiwas maana wasiwasi mwngi au uoga mwingi ni hofu ambayo %1 tu ndio hutokea,lakin vyote mara nying havitokei.. So usiogope

Kuna mtu kakushauri kilimo ni sawa,chips ni sawa pia,ila kwa upande wngu nakushauri km upo eneo zur uza chips au phone accessories.. Chukua vifaa vya simu vya kisasa uza sehem za kisasa bila kuogopa wala kua na aibu,,baada ya miez sita utaleta mrejesho hapa na utaninunulia bia. Chips ukipata sehem nzur ukaanza kidgo kdgo kwa mazingira mazur na usaf na kiwango cha utengenezaj wako wa mahanjumat hutajutia uamuz wako.

Ni vzr kufanya roho inachopenda,ufanye huku unafurahia unachofanya utafanikiwa zaid..Tchao .Xav Bero au Bero Communication.
 
Kila kitu ni risk,,maisha ni risk,biashara ni risk,kilimo pia,na kila aina ya vitu vina risk yake. So na bila risk maisha hayawez kua mazur au kuipima akil yako vzr.

Pole sana dogo ila tu hajatuambia uliipataje hyo milion 1 labda ulipiga deiwaka au uliiipata pata vip,,so sio ishu sna ila ishu ni kwamba,unataman kufanya biashara ila unaogopa isipokulipa kwa wakat mtaji utaisha**

Unataka kuwekeza huku hela uendelee kuiona ili usiwe na hofu ya kupoteza hela yako ambayo umeikusanya kidgo kdgo,hali hyo hutokea kwa yyte yule ambae anaanza kuwekeza kwa cchte kwa mara ya kwanza.

Dogo mimi nilianza biashara kwa shng 8000 ( elfu nane) miaka kadhaa nyuma nadhan wewe ukiwa shule ya msingi,lakin leo nauwezo wa kuagiza kontena 40 ft kutoka china, so milion ni kubwa sanaaa dogo wala usiogope wala kuwa na wasiwas maana wasiwasi mwngi au uoga mwingi ni hofu ambayo %1 tu ndio hutokea,lakin vyote mara nying havitokei.. So usiogope

Kuna mtu kakushauri kilimo ni sawa,chips ni sawa pia,ila kwa upande wngu nakushauri km upo eneo zur uza chips au phone accessories.. Chukua vifaa vya simu vya kisasa uza sehem za kisasa bila kuogopa wala kua na aibu,,baada ya miez sita utaleta mrejesho hapa na utaninunulia bia. Chips ukipata sehem nzur ukaanza kidgo kdgo kwa mazingira mazur na usaf na kiwango cha utengenezaj wako wa mahanjumat hutajutia uamuz wako.

Ni vzr kufanya roho inachopenda,ufanye huku unafurahia unachofanya utafanikiwa zaid..Tchao .Xav Bero au Bero Communication.
Kwa ufupi mkuu nmeitengeneza pesa hii kwa deiwaka mbalimbali lakini zaidi ni kumwaga zege sehem mbalimbali apa mjini nmeikusanya kwa mwaka mzima na zaid kwani kwa kila nachopata lazima wazaz na wadogo zangu ambao hawana wanaemwangalia zaidi yangu niwape chochote kitu
Lakini yote kwa yote umenitia moyo sana mkuu kazi ya mikono yako iwe njema as days goes
Asante Sana kaka
 
Wengi ni waoga ndio maana wanataka sana utafiti...
Kweli mkuu uthubutu ni mdogo sana uoga umejaa kila wazo huonekana si jema
Lakin zaid watu kuwaza faida kubwa kwa mtaji mdog tena kwa mda mfupi
 
Fanya biashara ya kuuza maji mvua ikikata kuanzia kimara, ubungo tabata mabibo mwambao wote huo maji ya bomba ni shida sana, nunua madum unakodi kirikuu unachukua maji hapo udsm ukifika tu ubungo dum moja 900-1000 wateja wakubwa ni mama ntilie, bar, hotel nk
 
Fanya biashara ya kuuza maji mvua ikikata kuanzia kimara, ubungo tabata mabibo mwambao wote huo maji ya bomba ni shida sana, nunua madum unakodi kirikuu unachukua maji hapo udsm ukifika tu ubungo dum moja 900-1000 wateja wakubwa ni mama ntilie, bar, hotel nk
Asante Sana mkuu ngoja nifatilie mchanganuo wake
 
Asanteni sana wakuu nyie ni ndugu zangu Mungu awabariki
 
Back
Top Bottom