Wewe ni mzazi yupi: Unaruhusu mtoto kumiliki na kutumia simu na mitandao ya kijamii au simu ni marufuku mpaka afike chuo?

Wewe ni mzazi yupi: Unaruhusu mtoto kumiliki na kutumia simu na mitandao ya kijamii au simu ni marufuku mpaka afike chuo?

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu salaam,

Tuna wazazi na walezi wa aina tofauti kwenye jamii, kuna wale wanaokwenda na wakati na wale ambao kidogo ka ukoloni kapo wakiamini njia zilizotumika miaka 47 kwake zitafanya kazi katika kizazi hiki.

Matumizi ya digitali yakua kadri siku zinavyosonga, si tu kwa watu wazima kwani hata watoto wanatumia digitali kwenye masomo yao na hata michezo. Sasa kuna wazazi ambao katika ulimwengu huu nyumbani kwake ni marufuku mtoto kumiliki na kutumia simu mpaka atakapofika chuo ikionekana huu ndio umri 'sahihi' au kwa wengine ni mpaka pale atakapokuwa na uwezo wa kujinunulia mwenyewe simu.

Kuna wazazi wengine siyo simu tu, hata TV nyumbani kwake ni marufuku, kwa kisingizio kuwa 'zinaharibu watoto', au 'siku hizi hakuna maadili', nk, unakuta TV inakaa chumbani kwa wazazi waangalie wenyewe, msiwafanyie watoto jamani 😁😁.

Nikwambie tu, kama wewe ni mzazi huyu jua tu kwamba mtoto wako anatumia simu kama hana akili nzuri, tena inawezekana anajua kutumia simu kuliko wewe, na wengine wanamiliki kabisa simu, ametoa wapi nani kamnunulia, hiyo inaweza kuwa topic ya wakati mwingine (ntawapa story sehemu ya comment mambo yasiwe mengi hapa, jinsi mzee wetu alivyokuwa mkoloni kwenye suala la TV na simu, na kama hilo lilituzuia kutumia vifaa hivyo).

Badala ya kumzuia, ambayo huwezi na unamnyima mtoto njia nyingine ya kujifunza na kukuza ubunifu, mwongoze kwenye matumizi mazuri ya simu, mueleze hatari anazoweza kukutana nazo kwenye mitandao hii na jinsi anavyoweza kutumia vizuri.

Apps nyingi zina matoleo ya watoto, muwekee hizo atumie na mara kwa mara fanya mazungumzo naye ya kirafiki ujue anafanya nini mtandaoni na vipi unaweza kumsaidia kuboresha zaidi matumizi yake.

Tukiwa tumeweka kalam chini kama Robert Heriel Mtibeli, tuambie, wewe ni mzazi wa aina gani, unamwongoza mtoto kwenye matumizi mazuri na kuhimiza matumizi ya digitali salama au team mafuruku mpaka mpaka mtoto awe na 'akili', pia tuambie kwanini?
 
Simu inategemea na akili yake pia na Jinsia.

Mtoto wa kiume nitampa vifaa karibia vyote, wakike ktk Simu nitalimit.. ila baadhi ya vifaa nitampa.

Pia kuna apps za Parental guide.. nitainject na kufatilia mienendo yake na kuzima baadhi ya services nikiona zimekuwa misused.

TV ndio tutagombana.. mara nyingi tamthilia za ajabu nyimbo za ajabu ndio zinaharibu watoto kuliko simu. Watoto wanajifunza how to Kiss somebody via TV.. wanajifunza kukata Mauno via TV.
 
Anachezea simu kucheck Youtube na TV cartoon aangalie apendavyo ili asivione vigeni akifikia ukubwani.
 
Mpee tu cm atumie c mpk afike chuo maana akifika chuo atakuwa bd mgeni wa cm Kali..km ww bb umenunulia Tecno ,bac jiandae likizo atarudi na macho matatu na atakuwa kashatoa jicho mojaa,ss cjui hapo utakuwa ulidhibiti nn kipindi akiwa secondary ..
 
Simu inategemea na akili yake pia na Jinsia.

Mtoto wa kiume nitampa vifaa karibia vyote, wakike ktk Simu nitalimit.. ila baadhi ya vifaa nitampa.

Pia kuna apps za Parental guide.. nitainject na kufatilia mienendo yake na kuzima baadhi ya services nikiona zimekuwa misused.

TV ndio tutagombana.. mara nyingi tamthilia za ajabu nyimbo za ajabu ndio zinaharibu watoto kuliko simu. Watoto wanajifunza how to Kiss somebody via TV.. wanajifunza kukata Mauno via TV.
Unafikiri hivi unavyomzuia kwenye TV hawezi kuviona kwenye simu?

Sijaelewa hapo kuzuia kulingana na jinsia, nini kinafanya umpe wa kiume vifaa vyote na wakike ulimit kwenye simu?
 
Anachezea simu kucheck Youtube na TV cartoon aangalie apendavyo ili asivione vigeni akifikia ukubwani.
Nimekupata, sasa unamuongoza vipi upande huo wa katuni na youtube? Maana hata kwenye katuni zipo za aina nyingi, na sasa nyingi zimejaa maudhui ya ovyo wakiwa wamedhamiria kupenyeza ajenda zao
 
Mimi nadhani inategemeana na uelewa wa mtoto katika kupambanua mambo,Mimi nimeanzia kumiliki simu nikiwa kidato Cha pili nikiwa na simu yangu Motorola C113 Hadi A-level nawala sijakuwa na tabia mbaya
 
Mimi nadhani inategemeana na uelewa wa mtoto katika kupambanua mambo,Mimi nimeanzia kumiliki simu nikiwa kidato Cha pili nikiwa na simu yangu Motorola C113 Hadi A-level nawala sijakuwa na tabia mbaya
Asante kwa mchango wako Mkuu, mtoto akipata mwongozo mzuri hawezi kutetereka, na hata ikitokea amekumbana na changamoto au kitu kibaya atarudi kwa mzazi kuomba msaada
 
Mimi ana miaka 8 na anamiliki simu, nimeinstall baadhi ya mitandao ya kijamii mfano WhatsApp na Telegram ambayo anawasiliana na ndugu wa karibu upande wa baba na mama tu. Kuna YouTube na chaneli nyingine za watoto.

Natumia Parental Control kudhibiti kila anachokuwa anafanya, hawezi kuinstall App mpya bila idhini yangu

Kwa siku za kawaida nimeset atumie kwa saa moja na weekend kwa saa sita muda ukiisha inafunga apps zote.
 
Nimekupata, sasa unamuongoza vipi upande huo wa katuni na youtube? Maana hata kwenye katuni zipo za aina nyingi, na sasa nyingi zimejaa maudhui ya ovyo wakiwa wamedhamiria kupenyeza ajenda zao
Kwenye youtube nimewawekea Youtube for Kids ,Netflix User ya watoto ,na hata hizi za kwenye Madish wanazi moderate maana mara nyingi ni Mr bean Cartoon ,Titans ,Big Shark,Masha and the bear etc ambazo hazina mauchafu.
 
Kuna uncle wangu Boy 10 Yrs akiona Miziki ambayo wanawake wamevaa nusu uchi kwenye Tv analilia aangalie, hataki ubafilishe.
Makuzi pia yanachangia, bado ni mtoto na wana uwezo wa kumuelesha na kum-introduce kwenye content nyingine ambazo zitamfanya afurahie na kumjenga pia
 
Unafikiri hivi unavyomzuia kwenye TV hawezi kuviona kwenye simu?

Sijaelewa hapo kuzuia kulingana na jinsia, nini kinafanya umpe wa kiume vifaa vyote na wakike ulimit kwenye simu?
Hawezi.. kutokana na active monitoring nitakayoifanya.

Jinsia nikimaanisha mtoto mdg hasa wa kike huwa ni wapenzi wa Camera.. picha etc.

Hakuna app mbaya sana kama Camera kwa mtoto, ataanza kujipiga picha mbalimbali na hapo ndio anakuw mjinga/chizi mapicha akiwa bado mdogo. Na kwa jinsia yake ni mbaya sana sana...

Kuna Jamaa yangu aliacha simu nyumbani kwake.. dogo akabeba na kuanza kujipiga picha nyingine zilikuw za nusu Uchi. Kufuta akazifuta nyingine akazisahau. Simu za siku hizi zina recycle bin, jamaa ikabidi aende ktk recycle bin na kukuta picha chafu chafu nyingi tu, muda huo dogo akiamini kafuta ushahidi.
 
Kwenye youtube nimewawekea Youtube for Kids ,Netflix User ya watoto ,na hata hizi za kwenye Madish wanazi moderate maana mara nyingi ni Mr bean Cartoon ,Titans ,Big Shark,Masha and the bear etc ambazo hazina mauchafu.
Umetisha sana Mkuu, kunywa soda kwa mangi ntalipa👏👏
 
Mimi ana miaka 8 na anamiliki simu, nimeinstall baadhi ya mitandao ya kijamii mfano WhatsApp na Telegram ambayo anawasiliana na ndugu wa karibu upande wa baba na mama tu. Kuna YouTube na chaneli nyingine za watoto.

Natumia Parental Control kudhibiti kila anachokuwa anafanya, hawezi kuinstall App mpya bila idhini yangu

Kwa siku za kawaida nimeset atumie kwa saa moja na weekend kwa saa sita muda ukiisha inafunga apps zote.
Safi sana Mkuu, hapo kwenye youtube unaweza kuinstall youtube for kids badala yake akawa anapata maudhui ya watoto pekee
 
Vitu ambavyo huwezi kushindana navyo/kuvizuia
1. Muda
2. Utandawazi
 
Nadhani ni swala la akili ya huyo mtoto mwenyewe na malezi aliokulia,hata kama ni wa kike kama yuko above 18,mpe huku ukifanya very close monitoring,ukigundua kuna shida chukua hiyo simu,ila kama hana shida yoyote muachie tu kwani dunia imebadilika sana,kuishi bila simu umri huo kunamfanya awe nje sana ya huu ulimwengu.Nina uhakika hata wale wazazi miaka ile hakuna simu,mambo haya ya hovyo hovyo kuanzia miaka 10 wengine walikwishayajua ila malezi kwakuwa yalikuwa mazuri unakuta hukuyaendekeza na ukafika pazuri,kwahiyo hata kwenye simu ni hivyohivyo......
 
Hawezi.. kutokana na active monitoring nitakayoifanya.

Jinsia nikimaanisha mtoto mdg hasa wa kike huwa ni wapenzi wa Camera.. picha etc.

Hakuna app mbaya sana kama Camera kwa mtoto, ataanza kujipiga picha mbalimbali na hapo ndio anakuw mjinga/chizi mapicha akiwa bado mdogo. Na kwa jinsia yake ni mbaya sana sana...

Kuna Jamaa yangu aliacha simu nyumbani kwake.. dogo akabeba na kuanza kujipiga picha nyingine zilikuw za nusu Uchi. Kufuta akazifuta nyingine akazisahau. Simu za siku hizi zina recycle bin, jamaa ikabidi aende ktk recycle bin na kukuta picha chafu chafu nyingi tu, muda huo dogo akiamini kafuta ushahidi.
Tunachokosea wazazi na walezi ni kufikiri kuwa kwanza; tunaweza kuwacontrol watoto, na pili ku-underestimate inteligence ya watoto... unaweza kufikiri hafikii maudhui hayo, utakuja kupata mchangao wa mwaka ukija kujua mtoto wako anaelewa mambo gani. Badala ya kumuwekea control nyingi, mwongoze... kwanza kuwa rafiki yake na pia usiwe mkuda ujue anajua nini, baada yapo unaweza kuweka mwongozo mzuri kwake

Kwenye jinsia hapo naomba nitofautiane kidogo na wewe, watoto wote bila kujali jinsia zao ni moja ya kundi ambalo liko targeted mno na ni rahisi kuwa influenced, kama unaweka bidii kwa wakike uweke bidii the same kwa wakiume, siyo kuwacontrol, kuwangoza katika matumizi salama
 
Back
Top Bottom