Wezi/Matapeli wanaweza kupatikana kwa kutrace namba zao za Simu?

Wezi/Matapeli wanaweza kupatikana kwa kutrace namba zao za Simu?

Inanambo

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2011
Posts
4,039
Reaction score
2,840
Hivi karibuni TCRA imesisitiza kutokuwapa mawasiliano wanaotumia namba za Simu ambazo hazijasajiliwa tena kwa kutumia vitambulisho halali vya wateja. hii ina maanisha hakuna MTZ anayetumia Simu sasa hivi bila kusajiliwa.Umezuka utapeli mjini wa kupora watu pesa baada ya kuwasiliana na Tapeli. Matapeli wakishapora pesa hunyanganya pia simu ya Victim wao na kutoweka nayo hata kama ni ya Mchina. Wanaotapeliwa hawana jinsi ya kuwapata Wezi hao zaidi ya Kutrace namba za Simu. Polisi wanaweza kuwasaidia wanyonge hawa kwa kufuatilia mawasiliiano na za CCTV Benki au Hotel kubwa. Naomba kuwasilisha wanaJamii ili tuwasaidie wale wanaopoteza mali zao kwa njia ya Kutapeliwa na Wezi wanaotumia mitandao ya simu kuwapata wa kuwaibia hapa Mjini na kwingineko. Yupo Mstaafu ametapeliwa MILION 80 anataka kukodi FBI wamsaidie kupata wezi wake. Huu ni Ulimwengu wa Science na Technolojia na Tz kwa hili hatuhitaji FBI au CIA kufuatilia.
 
huko mbali ni kufuata utaratibu aende mtandao hucka mfno voda kuna systems zitasaidia kama mophius ambayo utaona kila kitu tangu line ianze kutumika mpaka sasa sehemu aliko na watu anaowasiliana nao.muda saa sekunde na anatumia mnara ulioko sehemu gani.fanya mchakato.
 
Inawezekana kabisa hasa jeshi la polisi likiamua kutenda kwa weledi, tatizo ni kwamba ukisharipoti polisi ili usaidiwe, unageuzwa deal na wanamtafuta mwizi wako wakimpata naye anageuzwa dili
 
Tatizo rushwa imetawala ktk jeshi la polisi, wamekua sio waaminifu kabis. hata sijui ni kwanini?
 
Inawezekana kabisa hasa jeshi la polisi likiamua kutenda kwa weledi, tatizo ni kwamba ukisharipoti polisi ili usaidiwe, unageuzwa deal na wanamtafuta mwizi wako wakimpata naye anageuzwa dili

hahaha umeniacha hoi sana mdau, yani usiombe umeibiwa alafu ukaripoti jamaa hawajui kua ushaishiwa ulichonacho baada ya kuibiwa wenyewe wanakuchukulia wewe ndio dili sasa wakukamue zaidi. :becky::madgrin:
 
Inawezekana kabisa hasa jeshi la polisi likiamua kutenda kwa weledi, tatizo ni kwamba ukisharipoti polisi ili usaidiwe, unageuzwa deal na wanamtafuta mwizi wako wakimpata naye anageuzwa dili

Niliripoti jeshi la polisi kuhusu tapeli/mwizi flani nikatoa na namba sasa ni mwaka wa pili sijapata jibu,huenda mpaka uwe kigogo flani au mtoto wa kigogo ndio gereshi la polisi litashughulikia,kampuni za simu zina uwezo wa kumtrace na hata kuwatonya polisi lakini hawana haki hiyo kisheria
 
Back
Top Bottom