What about R&D?..The Case of Foreign Aid Influx & 'A Japanese Expert' Invite


Nadhani umei-miss point yangu.....
 
Tatizo: Ndivyo Tulivyo!!

Ngabu:

Sivyo Tulivyo. Nakumbuka sherehe ya uhuru kama miaka miwili iliyopita na Mwanakijiji aliandika posti moja kule Darhotboard. Katika mchango wangu nilitoa mfano wa wanaIsrael walitoka utumwani Misri.

Safari yao kwa mwendo wa miguu isingechukua zaidi ya miezi miwili lakini Mungu aliwafanya watangetange jangwani kwa miaka 40.

Katika kutangatanga kwao kuna waliotaka kurudi Misri kwa sababu walikosa mbogamboga. Na kuna wengine hawakuwa na imani ya kidini. Na kuna waliochonga ndama wa kuabudu. Hivyo miaka 40 ilikuwa ni therapy kubwa kwao.

Kuanguka kwa miradi mingi katika kipindi cha nyuma kulikuwa kumeandikwa UKUTANI. Vitu vingi tulivyofanya vilikuwa havijaota mizizi katika jamii yetu. Mtu anamaliza chuo na kwenda kuwa meneja wa Benki. Je ulikuwa unataka nini kama sio disaster. Mtu alikuwa anasomeshwa shule ili arudi nyumbani awe jaji tena wa mahakama kuu, unategemea nini?

Vitu vingi vimeanza kuota mizizi. Hiki ni kipindi tunachoweza ku-kick off maendeleo ya maana.
 

It all depends on the visionary of our leaders. When JKN was asking for assistance in the 60/70s, he would go for grant to build UDSM, TAZARA, Urafiki e.t.c. Nowdays, we are hosting a US prez and are asking him to buy us mosquito nets and the Chinese build us 'our' national stadium. At the same time, we busy stealing 3x of the cost of the stadium from our BOT coffers with impunity. What a joke.

If we have ministers fighting for tenders, 10% and ubia with investers, when will they have time to stratergise on behalf of the nation? We are doomed to fail unless there are big changes.
 
Bin Maryam, kwanza tunakubaliana kabisa kuwa hii R & D tunayoizungumzia siyo kuendeleza kompyuta na Ipod tu.. lakini is a total revolution in our research and development capability that would impact every sphere of our lives.. Kwa sababu sidhani kama tunaweza kufanya mabadiliko kwenye Ipod tu bila kusababisha mabadiliko kwenye kilimo, elimu n.k nilidhani tulenge kuleta mabadiliko katika ujumla wake.

Lakini ni nini basi kinatuzuia kufikia lengo hilo? Ni nini vilivyo vikwazo vya kufanya mabadiliko hayo. Kimoja ambacho nina uhakika si tatizo ni fedha.
 

So tell us my friend...if it's not money then what is it? Don't dance around just tell it like it is that you think it is...
 
mimi kama mchumi(business economist) nina mengi ya kuchangia hapa. lakini nitaishia kuchanganyikiwa tu.

naungana na nyani ngabu: waafrika ndivyo tulivyo. naongezea jingine: ng'oa ccm madarakani ili tuanze upya kuhusu utume(mission), malengo, sera, mikakati na mipango ya kuendeleza tanzania.
 

Just an observation...ktk baadhi ya nchi jirani vyama tawala vimekwishang'olewa lakini hakuna tofauti yoyote iliyotokea.
 
Just an observation...ktk baadhi ya nchi jirani vyama tawala vimekwishang'olewa lakini hakuna tofauti yoyote iliyotokea.

which brings us back to the same question.. what is wrong with us; and you of course provide what seems to be the only answer "ndivyo tulivyo"...
 

Mababu na mabibi zako waliochukuliwa kwenda Latin Amerika, visiwa vya karibian na Marekani ya kaskazini. Mababu na mabibi zako waliokatwa mikono na mfalme Leopold wa Ubelgiji ili kama adhabu ya kutovuma zao la mpira pori katika misitu ya Kongo. Mababu na mabibi zako waliowindwa kama wadudu waharibifu katika jangwa la Kalahari. Mababu zako waliochukuliwa kwenda kupigana Burma na Ulaya katika vita isiyokuhusu. Watu kama nyinyi mliosoma the Bell Curve na kuamini kuwa kweli mmelaaniwa kutokana na rangi yako!
 
Nani Ngabu,
Mkuu nakubaliana na wewe 100%, na hasa nikitazama maelezo ya KUBWAJINGA yaani ndio tumefunga msahafu...
It all depends on the visionary of our leaders. When JKN was asking for assistance in the 60/70s, he would go for grant to build UDSM, TAZARA, Urafiki e.t.c. Nowdays, we are hosting a US prez and are asking him to buy us mosquito nets and the Chinese build us 'our' national stadium. At the same time, we busy stealing 3x of the cost of the stadium from our BOT coffers with impunity. What a joke.
If we have ministers fighting for tenders, 10% and ubia with investers, when will they have time to stratergise on behalf of the nation? We are doomed to fail unless there are big changes.

 

Ongeza kwenye orodha hiyo:
Dhahabu inayouzwa kwa bei ya juu kabisa duniani sasa hivi inachimbwa hapa hapa lakini sisi wenye mali tunagawiwa rasharasha ya kutulaza usingizi.
 

I fully concur.

Acha wizi wa watu. Mali ghafi, madini na hata teknologia waliyokwenda kui-refine na kudai kila kitu ni chao.

Lakini hata hayo maendeleo tunayowasifia, kwa mfano waMarekani - msukumo mkubwa umeingia katika miaka hii ya karibuni kabisa - kwenye 1960s walipoamua kupanua elimu yao ya vyuo vikuu.
Sasa hivi watu wanataka tuamini kuwa Marekani hali zao zimekuwa hivi hivi kama tunavyoziona leo hii. Hii sio kweli.

Nasi pia pamoja na matatizo yetu mengi, hasa ya wizi na kutokuwa na mipango na utendaji mzuri, hali zetu zimebadilika kidogo. Bila shaka ningependa hali iwe imebadilika zaidiya hii iliyopo sasa; lakini ni tofauti na kusema kuwa hatubadiliki kabisa.

'Mwalimu' alitamani sisi tuwe tunakimbia wakati wenzetu wakitembea. Tujuavyo sote, hili limetuwia gumu kwa sababu mbalimbali, nyingi zikiwa tunazozisababisha sisi wenyewe.
 
Kwa wakina Nyani Ngabu,


Tusisahau tulikotoka. miaka karibu 30 baada ya muingereza kuchukua nchi, tulikuwa na shule moja yenye kutoa mafunzo ya sekondari nchi nzima na ilchukuwa wanafunzi sita tu. Miaka 41 ya utawala wa muingereza tulikuwa na graduates 70. Katika hao madaktari hawakuzidi kumi. Sijui kama wahandisi walifika watano! Miaka 41 ya kujitawala wenyewe, tunaexport madaktari Botswana,wahandisi wako kwenye mamia (kama sio maelfu), wasomi wetu wa nyanja mbalimbali wameenea dunia nzima. Leo hii maelfu ya watoto wetu wako kwenye vyuo vyetu vikuu wakitafuta elimu.

Frantz Fanon alisema ( si kwa maneno haya haswa) kuwa dhambi kubwa aliyofanya mkoloni ni kuwafanya waliowatawala kuamini kuwa wao wameumbwa duni kuliko huyo anayewatawala. Mtawaliwa hataweza kujikomboa hadi hapo atakapoikabili na kuiondoa imani hiyo ndani yake mwenyewe. Itachukua vizazi vingi mpaka sisi wenye ngozi nyeusi kuweza kuondoa sumu hii tuliyowekewa kwa takhriban miaka mia tano. Hii si sababu ya kukata tamaa.

Katika miaka ya sabini kuna mwandishi wa habari mmoja alimhoji mwanamapinduzi wa ANC kuhusu mapambano yao yasio na tumaini dhidi ya utawala wa makaburu. mwanaharakati huyo akamjibu " tulipoanzisha Umkhonto we Sizwe mwaka 1961 tuli'estimate' tutamng'oa kaburu katika miaka miwili which I think was a pretty good estimate! Yule mwandishi akasema hapo ndipo alipotambua kuwa hawa jamaa wata'prevail'.

pengine si kesho wala kesho kutwa lakini najua iko siku sis watu weusi tusimama bega kwa bega na wale waliotufananisha na tumbili!

Aluta Continua.
 

Nimemnukuu Bw. Godfrey Mwakikagile.
Nilikosea mwanzo, madaktari walikuwa 12! Ndiyo hali waliyotuacha nayo hao mnaowasujudia!
 
Kwa maneno yake mwenyewe Frantz fanon kutoka kitabu chake " The Wretched of the Earth". Someni na muelewe. Alizungumza haya wakati Tanganyika inapata uhuru! Kipi kimebadilika?

 

Koba,

Private sector ya wazawa si wabunifu, bali huchapia (copy) kilichofanywa na mwingine. Wao ni kukoroga dawa kwa vipimo, case closed!
 
Pamoja na kuwa na mtazamo wa kufuatilia Wachina, Wacuba hata Wamalaysia kwenye Teknolojia, mimi nafikiri tungeweka mkazo katika vitu ambavyo tuna uwezo mkubwa kuoanisha Utafiti na Uzalishaji mali.

Tumeshasema kuwa Kilimo ndio uti wa Mgongo. Tunacholima ni mbegu na mali ghafi ambazo ni hafifu na ubora wake ni mdogo. Kwa nini tusiweke kipaumbele kupitia SUA, Ukiliguru na vyuo vyote vya masuala ya Kilimo, Mifugo na Ufugaji ili kuleta mapinduzi ya Kilimo?

Mjerumani kabla ya kuondoka Tanganyika 1919, alikuwa ana master plan ya kulisha East and Central Africa kupitia bonde la Wembere (Singida Magharibi) mpaka Tabora na kutumia maji ya bonde na kuvuta mifereji kutoka Ziwa Nyanza (Victoria). Ikiwa wakati huo ni miaka karibu 100 imepita Mjerumani aliliona hili, tunashindwa nini sisi leo kuekeza nguvu zetu kuleta Mapinduzi ya kilimo na kuboresha kazi hii ambayo 75% ya Watanzania wanaitegemea kama njia ya kufanya kazi na kujipatia pato na mkate?

Ingekuwa mimi nipo katika kufanya haya maamuzi, ningefanya 65% ya allocation ya pesa na nguvu za utafiti ziende kwenye shughuli ambazo zitakuwa na immediate impact kutuongezea pato la Taifa. Mapinduzi haya ya Kilimo yangeanzia kwenye zana za kilimo, mbegu, mbolea, udongo, uhifadhi wa mbegu na mavuno kutokana na mali ghafi tulizonazo, kusindika na hata kutengeneza bidhaa kamili.

Starbucks walikataa kununua Kahawa ya Tanzania kwa pesa za kumrudishia Mkulima wa Tanzania walau 75% ya gharama kutokana na Kahawa yetu kuwa butu (isiyo na vikolombwezo)! Je tungekuwa na wataalamu wa kuongeza ubora na nakshi kwa kahawa yetu pale Mamlaka ya Kahawa au kampuni a kubagua kahawa si tungejipatia pesa nzuri tu kwa kilo? Mimi niliyeko Marekani nikitaka kahawa nzuri iwe ya Kenya, Ethiopia, Colombia hata Tanzania nikienda Starbucks, kilo moja kwenye kifurushi ni US $10! Kwa nini tusimpe nafasi mkulima wetu kupata japo $5 kwa kilo kwenye soko la dunia kwa kuongeza ubora wa kahawa yetu?

Somewhere in far east Asia, wamegundua mtindo mwingine wa kupata kahawa ya bei mbaya. Wanaacha aina fulani ya ngedere au nyani wale zile berries za kahawa halafu wakienda kunya, hiyo mbegu ya kahawa iliyopikwa kwa acid na kinyesi husafishwa na kukaangwa na kuuza kwa bei karibu US $ 150 kwa kilo!

Hakuna haja ya kukimbilia nguvu zote za utafiti kwenye Kompyuta au Magari yanayotumia maji ikiwa bado mkulima wa Kiembesamaki anatumia jembe la mkono. Si dhambi kuanza fikiria kutengeneza magari, lakini tuangalie priority iende wapi? Je tunaweza kufanya utafiti wa kuongeza marudufu uzazi wa samaki? Kule Lake Victoria Sangara anatafuna kila kitu, je tunawezaje kubadilisha tabia ya Sangara ili aina nyingine za Samaki ziwe na uhai na hivyo kuongeza aina za samaki wa kuuzwa nje?

Je tuendelee kukausha samaki kwa mkaa au tutumie kuni vilizoloweshwa maji ili harufu za kuni ziingie kwenye samaki kuongeza ladha?

Ukisoma manifesto za CCM, haya mapinduzi ya Kiteknolojia yametajwa, lakini nafikiri yamekaa kama mapambo na hakuna mwenye kujua njia nzuri ya kuweza kuhakikisha tunafika huko.

Tuna Sido, Veta, Tirdo, TFA, na upupu mwingi, kwa nini tusianze kwa kutoa nguvu hizi za kumapinduzi ya utafiti kwa hawa jamaa na si UDSM, SUA na sehemu yeyote inayoitwa Chuo?

Wale jamaa wa Gerezani wenye mambo ya kuchomea, wana design za ajabu jhujawahi ona, lakini wanatumia zana hafifu kufanya kazi zao za ubunifu, je hawafai kufanywa special project?

Je bwana Mianzi wa Iringa ambaye alipewa Kibunda na Mwalimu Nyerere siku ya Wafanyakazi kwa kutengeneza mabomba ya Mianzi, mradi wake umefika wapi?

Kama tuna nia ya kuhakiksha tunaleta mapinduzi ya Sayansi na Teknolojia, tutafanikiwa. Tusikimbilie sababu za kujizuia hata kuanza kufikiri eti tunaogopa Ufisadi au ni mpaka tuwe na Sheria zinazofanya kazi. Hii subiri subiri ndio inayofanya Barrick anachukua tani 10 za mchanga kwenda kupima rangi na tindikali nje ya nchi, kumbe kuna tani moja ya dhahabu ndani yake halafu wanatuambia wamepata kilo 10 kwa mwaka!
 
Nimeiona hii Daily News nikasema labda tuweze kujadili kama tuna uwezo wa kutosha kufanya kilmo cha mbegu za GM au kufanya utafiti wenyewe na si ule wa kupelekewa uliofanyikia Iceland!

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…