1-Superdol / bakressa
1-Hawa matajiri naweza kuwagawa ktk makundi 2 kundi la kwanza ni Manji/ Metl, kundi la pili ni Azam/Superdol.
Kiuchumi kwa mtizamo wangu wa macho wako vzr ila wanautofauti ktk kusimamia mpira. Superdol/Azam hawa walijitahidi kusimama wenyewe nje ya Yanga/Simba na ugumu walioupata ni kukosa sapoti ya mashabiki wa soka na mwisho wake kuonekana mpira kwao ni hasara na kutofanikiwa kushiriki vyema kwenye mashindano ya vilabu barani Afrika.
Manji/metl hawa pia wako vzr kiuchumi lkn pia wanatofautiana ktk ushiriki wao ktk soka la bongo, Metl hawa waliingia ktk soka hususani Simba wakiwa kama wafadhili wakishirikiana na matajiri wengine kiasi Simba ilionekana ikifanya vzr Tanzania na kutoa ushindani ktk mashindano ya vilabu Afrika.Naamini Metl walijiona wamekomaa kumiliki klabu hivyo walijitenga na kwenda Singida kujaribu kumiliki timu binafsi wakafanikiwa lkn wakapata ugumu ktk kuiendesha na kuchungulia hasara,vilevile wakajaribu kuiendesha Mbagala Market NAko ikawa hasara na kuamua kuiuza mwisho ikawa African Lyon.
Manji huyu naye aliingia kama mfadhili akiikuta klabu ikiwa na mgogoro mkubwa wa wanachama na khali ngumu ya kifedha, alitatua mgogoro akasaidia viongozi kusajili timu ya ushindani lkn klabu hii inahistoria ndefu ya migogoro inayotokana na njaa za matumbo ya watu,hivyo mgogoro mwingine ukaibuka na yy kuamua kuiongoza klabu hiyo kama Mwenyekiti. Na kwa kuwa ndani ya uongozi ameshuhudia mambo mengi mazuri na ya hovyo ikiwemo msururu wa viongozi wasio Na maana ktk klabu wenye njaa na maneno machafu. Lkn pia ameona na kutambua kuwa klabu ile INA mtaji wa mashabiki ambao ukitumiwa vyema hakuna hasara tatizo kubwa ni jinsi gani? Ya kuwaelewesha wapenzi/mashabiki na wanachama kuwa wao ni mtaji mkishirikiana pamoja, Manji kajitahidi saana sana kupambana ndani ya Yanga na nje ya Yanga kuhakikisha Yanga inakuwa na timu nzuri ilioweza kutawala Tanzania na kushindana Afrika.akiwa peke yake lkn amekumbana na vikwazo vingi mno toka kwa wanachama walaji, viongozi wa serikali na waandishi wa habari ambao kalamu zao wanazitumia vibaya kupotosha ukweli na kudharau mazuri yanayotendeka ambayo kupitia hayo ndo klabu inaimarika na biashara yoyote kufikirika kuiongezea klabu mapato..lkn kuwa kucha utasikia nani? Mkubwa Manji au klabu jibu ni moja kubwa Klabu lkn ikiwa na nia njema moyoni, vinginevyo mkubwa ni yule anayewezesha ndo utatambua ukubwa au udogo, MF singida united imewezeshwa na Metal bado ndogo Azam imewezeshwa na Bakhresa bado ndogo Yanga imewezeshwa na Manji imestawi je? MTU huyu hastahili shukrani ,utakuta anabezwa mno kama vile hajasaidia lolote na Hata kwenye kupambana kuonesha huu mpira,hii ni biashara zaidi kakumbana na uadui na kutokueleweka.
TFF,BMT,SERIKALI kwa pamoja hawa wote ndio adui no 1 wa soka la bongo hawajui nn? Wafanye na kwa wakati gani? Tff pale ambapo Yanga imefanikiwa kusonga mbele haijui majukumu yake nn? Inabaki kugombana na Yanga matokeo yake ni kufungia viongozi sababu ni tff kutazama maslahi yao. Wakati bodi ya ligi inaundwa mmiliki wa Afrcan lyon mr Zamunda kwa kutambua umuhimu wa bodi ya ligi kuwa na viongozi shupavu alimchukulia fomu Yusuf Manji ili awe mwenyekiti wa bodi ya ligi kama TFF ingekuwa inapenda maendeleo ya soka BMT nayo ingekuwa inapenda maendeleo ya soka na serikalu nayo ingemuunga mkono huyu maana mr Zamunda anakwambia mwenyekiti wa bodi ys ligi anapaswa awe mtu mwenye uwezo anatolea mfano (wa kumpigia simu mkurugenzi wa vodacom ) naye akapokea bila wasiwasi sio tunaweka mtu kwa ajili ya kujaza nafasi sasa haya yote kalamu ya waandishi ilipaswa isimame kuelimisha na kukosoa kwa haki.Sasa BMT baada ya shirikisho la soka kujiondoa KUPOKEA AMRI serikalini hao ndo hawana msaada wowote wapo wapo tu bora Hata walivyotumbuliwa. SERIKALI hawa ni mabingwa wa Matamko ila kama wangejitambua walau wangewasaidia watu wenye nia njema kama MANJI/METL ili kuvikwamua vilabu hivi kwa mtindo wa kuondoa wababaishaji wote kwenye hivi vilabu na kusimamia maendeleo ya pande zote ,kusimamia kila mpenda soka anayeingia viwanjani analipa na rasilimali za klabu zinatumika vyema.
Wapenzi hawa wako tayari kuimba nyimbo yoyote lkn udhaifu wa kolumu no 2 ndo unafanya kundi hili halijielewi linaumia saana.