What is wrong here

ongea nae...
though mwatakiwa muaminiane but stage ka hizo mashaka huwa meeengi hivyo if waweza mpeleleza u shud do so upate uhakika if huwa anahudhuria vikao ama??

if it is so n kila mara,then jirudi wewe ,wenyewe ujiulize as to why mmeo aone kampani ya vikao ni better kuliko yako nyumbani,try to work on hilo if tabia ikiendelea lohh sijui tena

while doin yote hayo ukumbuke kumwomba na Mungu wako rehema zake juu ya hili

ol da best
 

Wee 4X4 hivi huyu your hubby ndo yuleyule uliyesema kwamba ni mvivu kwenye jukwaa la mambo ya kikubwa au mwingine. Kule tulikutaka uweke mambo wazi zaidi lakini yaonekana ulificha. Sasa naanza kupata picha nyingine baada ya kusoma maelezo yako kwenye jukwaa hili. Nakushauri rudisha hoja yako kwenye jukwaa la mambo ya kikubwa ili ushauri uwe na wigo mpana zaidi
 

Ndo huyo, je ulitaka kujua nini zaidi! Ok ngoja niende then nikujibu swali lako.
 

Sasa wewe fo by fo by fa!!

Mwanaume gani anapenda kupigiwa simu mara 20? Nani anataka awe under control ya mkewe jamani?!!. Kwa hilo la simu ishirini tu tayari mtu anaweza kupata hisia za tabia zilizobaki

Mimi wakwangu alijaribu simu kede-kede akashindwa; kwa sasa nikivaa na yeye anavaa kisha tunatoka pamoja - Mapenzi yamerudi, hamu imerudi na spidi ni 120 hata kwenye kona

Vaa uende nae, unywe na uwe modern uone utamu
 
Nilijarubi hiyo style ila haikufanya kazi. Maana nilishawahi kumwambia kwamba naenda town kutembea so akimalizana na vikao vyake aniambie kwa kweli ndo ikawa nampa mda wa kukaa zaidi.
Kama hiyo haikufanikiwa,tafuta siku ya week-end/public holiday halafu unajikwatua vizuri;obvious lazima atakuuliza safari ya wapi;halafu mwambie kuna rafiki yangu wa siku nyingi tuliachana kitambo naenda kuonana nae(jinsia=kiume) halafu unatwanga simu mbele yake uko wapi hivi sasa.....
Akikuzuia mwambie mbona wewe unafanya haya lakini.....,sasa kuanzia hapo ndiyo unamshushia zigo la hizo kero zako.
Kama haitafanya kazi ni-PM nitakupatia Plan"B".
 
Banenani hapo hapo hadi kieleweke!

Akitoka nawe toka naye..au mpigie aliko mfate!

Kila abiria sharti achunge mzigo wake!
 

Yani ndugu ni kama unanijua vile. Yani hivyo ndivyo alivyo yani. Nimekuwa nikipigiwa simu na wanaume (za geresha tuu) yeye wala hana habari. Na mimi akipigiwa namuulizaga vizuri tuu, ila anakuwa mkali kweli. Kama jana kuna simu kapigiwa na dada mmoja yuko Norway alimsaidiaga maana alikwamaga one day akamdirect kwa watu husika. Imekuwa nongwa mpaka sasa wanakaribishana kutembeleana...! Mmmh kweli ndoa ndoano.
 

Asante,

Ni PM unipe hiyo plan B mwaya.

Asante.
 

It is very true he is taking my love for granted. Can you give me some clues za kutomuonyesha my love maana nashindwa nifanye nini sasa. Na kupika nimeacha sasa ajipikiege mwenyewe.
 
Ukiona mume wako hana chembe ya kajiwiivu na wewe

...Brown eye, chembe za wivu zikoje? mpaka akutwange makofi au akufungie ndani ndio ujue mumeo ana wivu?


...Loh, maisha ya kutegeana hayo, nilidhani ni wajibu mwenyewe kusema unakwenda wapi na muda gani utarudi bila kuulizwa.

Anataka na wewe usimfuatilie nyendo zake full stop.

...Brown eye, hiyo ndio ile inayoitwa ku ass-u-me
 
It is very true he is taking my love for granted. Can you give me some clues za kutomuonyesha my love maana nashindwa nifanye nini sasa. Na kupika nimeacha sasa ajipikiege mwenyewe.


...huenda mumeo yu katika mid life crisis. Cheche zilizokuwa zinachochea moto wa mapenzi baina yenu kwa kiasi fulani zimefishwa. Bahati mbaya, ndoa nyingi hupitia 'mawimbi' kama hayo, wenye busara na wabunifu wa kung'amua ndio huvuka salama. Jitahidi usijekipindua chombo.

Mgomba huo mama, palilia...
 

Kwa mimi kusema kumpigia simu mara ishirini ishirini huo ni msemo tuu. Ila napigaga kama mara tatu,nne hivi na sometimes ashike au asishike! Sio kwamba namcontrol na pia sipendi kufanya hivyo maana naona kama namnyima uhuru wake. Ila sasa inaonekana mimi kufanya hivi haisaidi ndo nikaomba kuuliza watalamu wanisaidie zaidi. Na kwenye vikao vyao ni wanaume tuu ndo wapo huko sasa mimi sitajiskia vizuri kama mwanamke pekee kuhudhuria jamani! Na hapo hapo wapo walio oa na wasio oa. Sasa kikao kikiisha tuu aliyeoa anaondoka mbio na kwenda kwa mkewe. Then yeye anabaki na wasioa mpaka huo usiku wa saa nane. Kuna siku pia kikao kilifanyika hapa hm. Baada ya kikao walioa walisambaratika mapema then wasioa wakawa wanaendelea na kinywaji taraatibu, nilishangaa sana wanachokiongelea ni kuhusu mademu tuu hamna stori zingine. Nilibakia kuchat tuu kwenye computer na JF nilipojisikia kulala nikaenda kulala zangu.
 

Asante, but nadhani mgomba hupaliliwa kwa pamoja sio mtu mmoja kama sijakosea!
 
Asante, but nadhani mgomba hupaliliwa kwa pamoja sio mtu mmoja kama sijakosea!

...whatever the scenario, Marriage is like mathematical equations, solving one means you get another one... the "turbulence" you are facing now and your ability to cope, will make you more stronger when facing even greater challenges ahead.
 
...chenga ya mwili, huenda 'better half' wake pia ni mwanachama hapa...


Tobaaa....Mungu apishie mbali LOL


Nikirudi kwenye mada,, mi naona kwa maelezoya 4x4xfar (By the way haya nagari yanasifika kupita njia zozote zile sio kama vicorolla) ningeshauri kuwa while keeping an eye on him, usiwe too nagging hadi ashindwe kuona sababu ya yeye kuwa na wewe muda mrefu na matokeo yake anaona ahueni kuwa na marafiki zake. haijalishi kama hawajaoa, jiulize hao waliooa kwa nini wakimaliza kikao wa ni mbi nyumbani? lazima kuna kitu wanachowapa ambacho labda wewe humpi mumeo.

Na pia, uvumilivu, kama hakuna nyumba ndogo mahali, jua ni mapito tu timiza wajibu wako kama mke mambo yatanyooka...huwezi kushindwa kitu at least from your name hehehehehehe
 
hodi humu ndani! nimeguswa na hii thread ikabidi niingie nichangie kidogo, wangu alikuwa na tabia kama hizo , alianza kidogo kidogo mwisho alizoea kabisa, tligombana sana wakati wa mwanzoni baadae nikaona ngoja nimuache amalize mambo yake then akiamua atatulia mwenyewe, tulikaa miezi kama 3 akitoka anaamua kulala huko akiamua anarudi ili mradi tu, ndani ya hiyo miezi 3 nilimuwekea ngumu haswa, sikuwahi kumuuliza umelala wapi wala hiki wala kile, akija asubuhi anakuta nimemuandalia kama kawaida bila kumuuliza lolote, akakaa akafikiria akaona hali ni mbaya,mwenyewe siku hiyo kajirudia mapema akaniomba maongezi, tukayasuluhisha, but alikoma mpaka leo hajarudia kulala/kukaa nje mpaka mausiku.jitahidi kupambana hawa wanaume ukiwaendekeza tu basiiiiii
 

...dddduuuuhhh! kwanza karibu, pili nakusifu. Wanawake kama wewe karne hizi ni mmoja katika alfu moja na moja 😀!
 
Dadangu kwa kweli una mtihani, ila kama walivyokueleza wenzangu hakuna dawa mbadala. Jaribu zote huenda moja itafanyakazi kwa hubby wako. Si unajua tena uendawazimu wao unatofautiana.

Ndugu yangu ngoja nikupe neno, hakuna mtu mwoga wa kuachwa kama mwanaume, ndiyo maana kila wakati anajitahidi awe na pa kuegemea akijifanya mjanja kumbe hana lolote. Mwambie aende jumla huko anakoona kunamfaa siyo anaugawa usiku, nusu huko nusu karudi. Dunia yenyewe hii ukimwi kibaooo. asije akakuletea la kukuletea bure.

Hebu mvalishe chupi nyeupe wakimchezea utajua halafu mshughulikie sawasawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…