Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 94,296
- 122,540
Hivi nini kinaendelea?
ni mental issues au kuna mengine?
nimeona kuna watu wanahusisha na Illuminati....
nimeona clip ya DMX....
Kanye West ana tatizo gani hasa?
Paulo Sergio De Souz Nyani Ngabu
BAK
Inawezekana kabisa kuwa anasumbuliwa na matatizo ya kiakili na hata ya kihisia.
Kwa vile tu yeye ni nyota wa muziki, hiyo haimaanishi kwamba yuko tofauti sana na wengine.
Na yeye mwisho wa siku ni binadamu tu kama tulivyo binadamu wengine.
Halafu, kwa watu observant kama mimi, hilo la yeye kuwa 'volatile' hajalianza leo.
Tokea zamani yuko hivyo ila sasa ndo naona hiyo 'volatility' yake imeshika kasi.
Unakumbuka 2009 alipomvamia Taylor Swift na kumnyang'anya kipaza sauti na kuanza kutiririka kuhusu nani alistahili kushinda hiyo tuzo aliyoshinda Taylor?
Hiyo ilikuwa ni moja ya dalili alizozionyesha hadharani.
Kwa hiyo mimi naamini kabisa kuwa huenda ana matatizo ya akili na kihisia ambayo bado hayajapatiwa ufumbuzi muafaka.
Kuhusu Illuminati, mi nadhani hizo ni hekaya za Abunuasi tu.