Whatsssssss!!!!!!!!!????

Jamaa mmoja alifikishwa hospitali akiwa na malaria kali,
DOCTOR: Huyu lazima apewe kitanda.
MGONJWA: kitanda ninacho labda kabati [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nesi mmoja alipewa kazi amhudumie mgonjwa na akapewa maagizo ikifika saa 8 ampe chakula,
ila nesi akala yeye kile chakula kabla ya saa 8,
ilipofika saa 8 kasoro ndugu wa mgonjwa akampigia nesi simu akasema " naomba umlazimishe ale chakula humo kuna sumu tumekubaliana wanafamilia bora afe kwakua hatuna hela za kumpeleka india. "
Nesi hoi[emoji13][emoji13][emoji13][emoji13]
 
Jamaa alipanda tax akamwambia dereva "zima mziki dini hainiruhusu kusikiliza nyimbo za kidunia kwasababu wakati wa yesu hakukuwa na redio".
Dereva akatii akazima alafu akasimamisha gari na kufungua mlango wa abiria,jamaa akamuuliza " nini tena?"
Dereva akajibu " wakati wa yesu hakukuwa na tax shuka ungoje punda."[emoji12][emoji13][emoji13]
 
Mlevi alimkuta ostadhi akitoa mawaidha:
ole wenu mtendao dhambi mtakutana na moto mkubwa siku ya kiama,
Mlevi akamjibu:
na nyie uko peponi mkipewa mahindi mabichi msije kutuomba moto wetu.[emoji12][emoji13][emoji13]
 
Teja baada ya swaumu kuwa kali saa 6 mchana akaamua kupiga simu redion.
MTANGAZAJI: eeh wimbo gani unachagua?
TEJA: adhana ili nifuturu.[emoji23][emoji23]
 
Mchungaji flani wa kichaga alikuwa akimtoa muumini wake pepo:-
MCHUNGAJI: Toka na ushindwe kabisa.
PEPO: sitoki.
MCHUNGAJI: tokaaa tena ushindwe na ulegee na usirudi.
PEPO: sitoki nimemuingia huyu ili nimpe mamilioni.
MCHUNGAJI: ( kwa sauti ya chini) nakuamuru mtoke na uniingie mimi. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dogo mmoja alipakizwa kwenye gari na mama yake akiwa anaelekea mbeya na kumuachia maagizo konda gari ikifika morogoro amjulishe dogo.
Gari lilianza kuondoka na yeye akiwa amelala,
baadaye aliposhtuka akauliza " konda tuko wapi hapa?"
konda akajibu " bado vituo viwili tufike mbeya"
dogo akaanza kulalamika " maamaaa konda umenipitisha morogoro,nirudishe umenipitisha"
Abiria wote wakaanza kumtetea dogo " mrudisheni acheni uonevu,mrudisheni aliposema."
Dereva akageuza gari mpaka morogoro walipofika konda akasema " aya dogo moro ndo hapa."
Dogo akajibu " haya sasa tunaweza kwenda kwasababu mama aliniambia nikifika morogoro nianze kula maandazi yangu."[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wageni wengine noma.
MWENYEJI: utakunywa nini soda au chai?
MGENI: nitakunywa soda wakati nikisubiri chai ichemke.
MWENYEJI: hapa kuna sprite na coca nikupe ipi?
MGENI: nipe coca,sprite niwekee kwenye friji iendelee kupoa.
MWENYEJI: nikupe mkate au maandazi?
MGENI: nipe maandazi kwanza mkate nitakula na chai ikichemka.
<Jioni ilipofika>
MWENYEJI: nikuandalie chipsi mayai au kuku?
MGENI: niandalie chipsi kuku kwanza mayai naomba uchemshe 10 ili nishushie na ile sprite.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna walevi wawili walikuwa wanapiga stori hivi:-
MLEVI 1: Hivi nchi ya china iko mbali eeeeh?
MLEVI 2: Sidhani mbona kazini kwetu kuna mchina anakuja na baiskeli.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Bosi mpya katika construction site aliamua kuonyesha yeye ni mchapa kazi hodari kuliko wa zamani katika pita yake akamkuta jamaa amelala kivulini muda wa kazi.
Akamuuliza " we kijana kwanini umelala muda wa kazi unalipwa sh ngapi kwa mwezi?"
kijana akajibu " nalipwa tsh 400,000 bosi"
bosi kwa hasira akaenda naye mpaka ofisini akamlipa hizo tsh.400,000 na kumfukuza kazi muda ule ule baada ya hapo akaenda kuwauliza wafanyakazi wengine yule kijana niliyemtimua kazi alikuwa anafanya kazi section ipi?
Jamaa wakamjibu "Samahani bosi unamaanisha yule muuza ice cream aliyekuwa amelala pale kivulini"
[emoji12][emoji13][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mlevi kakutwa akikojoa eneo la shule mwalimu akamuuliza:-
MWALIMU: hilo bango hapo linasemaje?
MLEVI: usikojoe hapa.
MWALIMU: kwahiyo?
MLEVI: mimi nilijua ndo jina la shule. [emoji12][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
ahahah nimerudi tena kwa uzi juu nivunje mbavu mie.
Waziri flani wa japani alipata safari ya kwenda marekani kumuona obama.
Sasa yeye kingereza kilikuwa tatizo akamtafuta mkalimani ili afundishwe angalau hata jinsi ya kusalimia.
Akaambiwa ukifika sema " how are u?"
obama nae atakujibu " am fine u?"
na wewe utasema " Me too."
waziri akaenda kufika airport akamkuta obama na mke wake ikawa hivi:
Waziri: who are u?
Obama ( akiwaza huyu jamaa ni dharau ama?) akajibu: Am mishells husband.
Waziri: Me too[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwa wale tuliosoma shule za fagio na kidumu cha maji pia wamekutana na hii:-
1. Juma na uledi.
2. Hawafu mwenye nguvu.
3. Mfalme juha.
4. Jua na upepo.
5. Pwagu na pwaguzi
6. Muwa uliozamisha meli.
7. Sikulamba sukari.
8. Sizitaki mbichi hizi.
9. Heka heka za abunuasi
10. Nani atamfunga paka kengele.
 
<<<HIVI HIZI SIKU HIZI BADO ZIPO:>>>
1. Kung'olewa jino kwa uzi na kutupwa juu ya bati ili liote jingine.
2. Ubwabwa kupikwa siku za jumapili tu.
3. Kidonda kutibiwa na unga wa vidonge au mafuta ya taa.
4. Ukumbi wa sherehe kupambwa na toilet paper.
5. Kunyolewa na mkasi.
6. Kufunga hela kwenye leso au pindo la khanga.
7. Kwenda kuangalia sinema za ukimwi na lishe sokoni.
8. Kurewind kanda kwa pen.
9. Ndala kuchemshwa ili zisiishe.
10. Kucheza umeshikilia kaptula sababu lastic imeisha.
11. Kuchonga penseli kwa meno.
12. Kukata ndala ili uwe ufutio.[emoji12][emoji13]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…