Whatsssssss!!!!!!!!!????

MWALIMU: Nitajie eneo lililo ndani ya Tanzania ambalo lina herufi 8, herufi 4 za mwanzo ni chakula wazungu wanapenda kula pia herufi 4 za mwisho ni kiungo cha binadamu.
MWANAFUNZI: andazi[emoji12][emoji23][emoji23]
.
.
jibu ni bagamoyo.[emoji736]
 
Mtanzania na mkenya waliingia supermaket moja jijini Daresalaam.
Mkenya akawa anajigamba kwamba wakenya ni wajanja kuliko watanzania huku akimwonyesha mtanzania chocolate tatu alizoiba supermarket.
Mtanzania akamshawishi warudi tena ili na yeye akamwonyeshe ustadi wake walipofika ndani mtanzania akamwambia mhudumu "nataka nikuonyeshe mazingaombwe hebu niletee chocolate tatu"
yule mhudumu akaleta tatu.
Jamaa akazila zote mbele ya mhudumu halafu akasema "unaona nimekula chocolate tatu lakini amini usiamini chocolate zako zote zipo mfukoni kwa huyu jamaa"
Mhudumu akamkagua mkenya mfukoni akachukua chocolate zake zote tatu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Zuzu mmoja kapita sehemu flani akawakuta watoto wanacheza akawadanganya "Nyie nendeni kule kuna chakula kinagaiwa"
wale watoto wakatimua mbio.
Zuzu akajiuliza "Mbona wanakimbia sana labda kuna msosi kweli" nae akaanza kutimua mbio.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
<Tofauti ya ukopaji kati ya mswahili na mzungu>
[emoji117]MZUNGU : HI bro, i need $100 will pay u back on monday.
[emoji117]MSWAHILI : Kaka vp shwari? Dah hatuonani mzee vp mishe? Mnatunyima nini, juzi nimekuona kwa mbali shavu dodo full kipupwe sie tupo bwana shida tu, halafu misiba mingi,wife nae kajifungua ghafla sasa kuna cheque naisubiri haijatoka hadi leo wanasema itatoka next week hapa nimekwama naweza pata ka laki karibu hapo nitakurudishia mwisho wa mwezi.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
UJINGA NI
1. Kuweka majani ya chaji kwenye sprite ili iwe coca cola.
2. Kudhani mzungu ana kivuli cheupe.
3. Kutoa mimba halafu unalala na mdoli.
4. Kupumua mbele za watu ukiwa umevaa headphone.
5. Kumkimbikia simba porini wakat ulikuwa unaenda kujinyonga [emoji12][emoji13][emoji13][emoji13]
 
BAADHI YA MISEMO ILIYOENEA USWAHILINI.
1. Hata uwe na bahati vp huwezi kupata lifti kwenye msafara wa rais.
2. Hata nyani / ngedere awe mtundu vp hawezi kudandia tawi la benki.
3. Hata kuwe na baridi vp huwezi kujifunika leso.
4. Vyombo vya habari havioshwi.
5. Mkaa hauuzwi supermaket.[emoji12][emoji13]
 
Mchaga mmoja alipata ajali akapelekwa hospital akiwa amezimia.
Alipozinduka akamkuta nesi akamuuliza "sasa nesi nilikuwa na saa yangu ya luxury mpya iko wapi? Nesi akajibu" we umekuja hapa bila saa itakuwa imekatika halafu mkeo na mwanao wamekuja kukuona. Jamaa akasema " yeuwiii yesu na maria wamefunga duka."[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dokta wa vichaa aliwachukua machizi wawili na kuwaingiza kwenye chumba chenye giza totoro.
Akawasha tochi kisha akawaambia wale machizi waupande ule mwanga kisha waende makwao.
Chizi wa kwanza akaanza kuurukia ule mwanga bila mafanikio huku chizi mwenzie akiwa anagaragara chini hoi kwa kicheko.
Yule dokta akamuuliza yule chizi ni kwanini anacheka vile, yule chizi akamjibu "mi nimeshakushtukia mpango wako, unataka tukipanda huo mwanga uzime tochi yako halafu sisi tuanguke chini."[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Katika bus mama mmoja alitaka kumnyonyesha mtoto,
Mtoto akakataa,mama akamwambia "nyonya kama hutaki nampa anko anyonye (Anko ni kaka mmoja ambae ni abiria aliekaa pembeni na huyo mama)
Mtoto akanyonya kidogo akaacha, Mama akamtishia tena kumpa anko.
Ndipo yule kaka kwa hasira akahamaki akasema "mama hebu kuwa na msimamo unajua nimepitiliza vituo viwili kwa ajili yako hebu kuwa mkweli unanipa ninyonye au nishuke!"[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji119] [emoji119] [emoji119] [emoji119] [emoji119]
ROHO MBAYA
Jamaa mmoja alitokewa na malaika akaambiwa chagua chochote unachokitaka halafu jirani yako atapata mara mbili kwa mfano ukichagua PRADO jirani yako atapata PRADO mbili,
Jamaa akafikiria akasema "nitoe jicho moja."[emoji12][emoji13][emoji13]
 
Wadada watatu walikuwa wamekaa pamoja wakinywa juisi kwenye mgahawa.
MDADA 1: najua mume wangu sio mwaminifu jana nimekuta rangi la lipstick kwenye kola ya shati lake.
MDADA 2: hata wangu nimekuta condom kwenye mfuko wake wa suruali nilichofanya nikachukua pini nikazitoboa toboa zote halafu nikazirudisha kwenye mfuko.
MDADA 3: ghafla kapaliwa na juisi na kudondoka akazimia. [emoji12][emoji13][emoji13]
 
Madenge na mjomba yake wamepakia mbuzi kwenye lori mara mbuzi mmoja akakojoa madenge akamwambia mjomba yake "MJOMBAA MBUZI MMOJA AMETOBOKA ANAVUJA UKUU" [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Baba anamuuliza mwanae:-
BABA: Eeeh mbona leo unawai sana kwenda shule?
MTOTO: mwalimu wa bagia leo anawai sana kuja.
BABA: pumbavu! Kumbe sio kuwai masomo?
MTOTO: si wanasema elimu haina mwisho ila nikichelewa bagia zinaisha.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Jamaa flani kaajiriwa kwenye kampuni,akapewa supervisor mwanamke.
SUPERVISOR: unaitwa nani?
JAMAA: naitwa john.
SUPERVISOR: john nani? Unajua jambo ambalo nimegundua ni kuwa watu wakianza kuitana kwa majina ya kwanza mnazoeana na kazi haifanyiki mimi si rafiki yako ni supervisor wako.kwahiyo nipe jina lako la pili upesi ndio nitakalotumia kukuitia.
JAMAA: naitwa john mume wangu.
SUPERVISOR: haya bwana john endelea na kazi.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
MISEMO YA ZAMANI
1. Gari la kuvutwa haliovateki.
2. Mganga haagizi tembele.
3. Wimbo wa taifa haupigwi disko.
4. Feni haiwashwi beach.
5. Mbwa hanenepi miguu.
6. Mjini shule, kijijini tuition.
7. Heshima pesa,shikamoo makelele.
8. Hata bibi alikuwa kijana.
9. Mshikaki hauchomwi kwa jiko la gesi.
10. Kipara bila pesa ni kovu.[emoji12][emoji13]
 
Kuna jamaa alienda kupiga stori kwa mshikaji wake.
Mara mvua kubwa ikawa inanyesha,mshkaji wake akamwambia huyo jamaa " itabidi ulale hapa sebuleni mpaka kesho kwakua mvua ni kubwa inanyesha." jamaa akakubali.
Yule mwenyeji akaingia chumbani kama dakika 10 halafu ile kutoka sebuleni akamkuta jamaa kalowa tepetepe... Akamuuliza " vipi mbona umelowa?"
jamaa akajibu " nilienda kuchukua shuka nyumbani."
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Daktari alikuwa anamuandaa mgonjwa ili amng'oe jino,hivyo akawa anajaribu kumpa stori za hapa na pale kama kumtoa wasiwasi.
Daktari "unajua jinsi gloves zinavyotengenezwa?"
Mgonjwa "hapana."
Daktari "huwa wanachukuliwa watu wenye viganja vyenye saizi mbalimbali,wanapakwa material ya raba iliyo kama ujiuji kisha wanawekwa juani,ikikauka wanavalishwa then tayari unapata gloves"
Mgonjwa "kwi kwi kwi,teh tehe tehe aha aha haahahaahaaa."
Daktari "unacheka nini?"
Mgonjwa "nafikiria CONDOMS zinavyotengenezwa."
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Watoto wapo hospitali mtoto wa kwanza kamwona mwenzie analia ikawa hivi :-
Mtoto wa 1: unalia nini?
Mtoto wa 2: nimekuja kupima damu.
Mtoto wa 1: ndio sababu unalia?
Mtoto wa 2: wamenikata kidole changu.
Mtoto wa 1 na yeye kaangua kilio kilio balaa.
Mtoto wa 2: unalia nini?
Mtoto wa 1: nimekuja kupima mkojoo.[emoji24]
[emoji12][emoji13][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…