pingli-nywee
JF-Expert Member
- Sep 16, 2015
- 11,923
- 13,350
Hujui unachosema, kama kuna rais ambaye alikuwa rais wa watu wa kawaida ni MOI. Na ile kauli mbiu yake ya fuata Nyayo na Harambee. Alikuwa ananyanyua mawe kwa mikono yake mwenyewe akijenga zile 'gabion' za kuzuia mmonyoko wa udongo kule vijijini. Pia alikuwa na tabia ya kuhudhuria kanisa, kila jumapili kijiji tofauti kule mashinani. Ila hayo yote yalikuwa ni kiki na alikuwa na allergy kubwa sana na upinzani na alipenda sana kuimbiwa nyimbo za kumsifu na kwaya za 'wazalendo'. Jiwe akijiangalia kwenye kioo sasa hivi ataanza kujiita Arap Magufuli.Aisee acha kumfanisha RAIS wetu na Moi (in serious tone). Moi hakuwa rais wa wakenya, bali ALIKUWA RAIS wa WENYE Kenya. alilinda maslahi ya wachache kwa hasara ya wengi. aliendeleza kuwauza WATU wake kwenye utumwa.