Whitedent wanatumia Siri gani "kuua" brands nyingine za dawa za meno eg "Aha, AfyaDent na Colgate ?

Kwakweli bei ndio inayofanya watu wengi watumie whitedent.
 
Colgate ni bora kuliko whitedent, tatizo ni upatikatanaje wake mfano kwa sasa nipo geita wiki ya pili nimezungua maduka kibao ila haipatikani.
 
Hahahaaaaa!! Umenikumbusha mbali aiseee!! Kweli ulikuwa ukitumwa dukani unaambiwa ukanunue colgate sio dawa ya meno. Colgate ndio ilikuwa dawa niloizoea hadi nilipohamia kwa sensodine.
 
Kuna kampuni mbili hapa bongo zilikuwa juu sana ila walipo jichanganya tu miaka ya tisini basi wakapigwa bao la ajabu.

1. Back in time Colgate ilikuwa dawa pendwa sana na watz miaka hiyo but waliingia mitini kiaina Whitedent akachukua nafasi.

2. Pepsi alikuwa hana mpinzani Tz hii,lakini alipo zingua tu Coka akampiga bao la uhakika.

"the highest risk shoud give the maximum profit"
 
Hizi product zote hakuna hata moja yenye urafiki na mtumiaji zipo kwa ajiri ya biashara
Kumbuka kadri unavyotumia hizi product ndivyo na uimara wa meno yako unavyopungua hakuna ukipatacho kwa kutumia dawa za mswaki zaidi ya fleva na ladha tamu lakini ndani yk kuna comical maalum iliyowekwa ili kumuathir mtumiaji ili aendelee kutumia bidhaa yao
Jiulize kwa nini wazee wakizungu wote ni vibogoyo?
 
Wewe umenena na atleast ni mkongwe,toka zamani tulikuwa tunatumia Colgate kama dawa ya meno enzi hizo kuna redimedi.

"the highest risk shoud give the maximum profit"
 
pikipiki pia zilikuwa zikiitwa 'Honda'

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mass marketing, ujazo, kuelewa wateja wanataka nini (yaani kubadili taste ya dawa kulingana na vionjo vya wateja).
 
Kuna kijana mmoja pale Muhimbili alifanya utafiti kwenye hizi brands za dawa za meno zilizoko sokoni

Yeye alikua akilinganisha uwezo wa kuua bacteria wanaopatikana kwenye kinywa na wanaosababisha matundu kwenye meno and other oral conditions

Alichogundua ni kuwa dawa yenye activity kubwa kuliko zote ni Whitedent yenye ticlosan (ilikua na zone of inhibition kubwa zaidi) ikifuatiwa na colgates huku Aloevera zikishika mkia
 
Samahani mkuu hiyo topic ya Demand form 2 ni ya nchi gani?
 
Plus vituo vya mafuta tunaviita Shell mara nyingi wakati Shell ni cama total, puma etc
 
Naunga mkono kiongozi. Kuna size tofauti, kuna mswaki. Mimi mdau wa Whitedent Herbal
 
Nimetumia mara ya mwisho mwaka jana hiyo whitedent, nilipooa tu wife akasema achana na hizo tope [emoji16][emoji16][emoji16] sasahivi ni mwendo wa colgate tena mwenyewe anajua duka lenye colgate original

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Colgate ni dawa nzuri sana na inaondoa matatizo mengi sana madogomadogo ya kinywa.
Tangu nilipoanza kuitumia 2012 nikiwa chuo sijawahi kubadilisha nyingine. Ni bora nisafishe meno bila dawa ya meno kuliko kutumia whitedent

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…