WHO inatakiwa izijibu hoja za Rais Magufuli kwa umakini mkubwa. Tropical diseases kama TB, Malaria kwanini hazina chanjo na zinaua sana?

Ni experience kubwa ya maisha, watu wa vijijini wanajaribu mambo mengi katika maisha kwa namna nyingi kwa hiyo wanakuwa wahenga wanaojua mambo mengi.

Only that,
 
Haya ya kwamba chanjo ni sumu na ni mbaya yanapaswa kuthibitishwa kitaalam,tofauti na hapo ni hoja ambayo haina mashiko!
 
Sijakataa tamaa Mkuu, na vitabu vya nyerere nimevisoma na ni kweli KABISA, Nyerere aliadopt itikadi hii ya kijamaa na kujitegemea kutoka Russia, China na Cuba

Ilitufaa kwa wakati ule, lakini je stagnation yake imesababishwa na nini? Wazungu?
Ndiyo, wazungu walichangia kwa kiasi kikubwa kukwamisha mipango yote ya Nyerere. Nyerere alisisitiza sana umuhimu wa nchi kuwa na viwanda vyake na kuboresha kilimo chake. Enzi za Nyerere nchi ilikuwa changa lakini tuliweza kutengeneza nguo zetu (MWATEX, etc), tulikuwa tunaprocess kahawa zetu (BUCOP, etc.) afu uniambie ndani ya mtu mweusi hamna uwezo wa kufanya makubwa?

Wazungu walituwekea vikwazo vingi tu eti kwa vile sisi ni wajamaa. Si kila sabotage wanayoifanya wakutangazie. Ujamaa na Elimu ya Kujitegemea ulitufaa wakati ule na bado unatufaa sasa. Maana halisi ya Ujamaa si kwamba kila kitu kiwe mali ya serikali au wananchi kulima shamba kwa pamoja na kuwa na duka la ushirika. Maana halisi ya Ujamaa ni recognition kwamba binadamu wote ni sawa, na hasa mkiwa watu wa taifa moja, ni sawa na pia ni ndugu. Maana yake ni kwamba huwezi siku zote ukawa unajiangalia wewe tu, ukijilimbikizia mali wewe tu, kwa kutumia fursa yako ya kushika nyenzo za uzalishaji mali. Maana ya sasa ya Ujamaa ni Uzalendo.

Sasa wewe lishwa propaganda za kibepari kuaminishwa kwamba Ujamaa ni umaskini halafu mapebari wenyewe wa kimagharibi ni wajamaa ajabu. Huko Israeli hadi kuna vijiji vya ujamaa vinaitwa Kibutz.
 
Walijaribu kufanya hivyo kwa Wachina wakafeli, kwa Waamerika wengi hawajafanikiwa watakavyo, kwa waarabu bado wanapambana.....

Kwanini sisi watudrive ilihali tuna wasomi wa kutoka vyuo vikuu wanaojua kureason kwa miaka zaidi ya 40 sasa?
 
Wewe mwenye reasoning capacity hukupitia hizi chanjo?
Binadamu mwenye uwezo mzuri wa kufikiri hawezi kuishi na kufikiria maisha ya hapo alipo, lazima afikirie mbele. Changamoto za leo huleta maarifa ya kusaidia kizazi kijacho.
Mbona leo tunanunua Ndege, kwani Wazee wetu walisafiri vipi zamani? Logic ipi unayoisemea?
 
Nyie nani amewazuia msitengeneze chanjo? Tuanzie hapo make watu wengine akili hazitoshi kabisa.
 
Walijaribu kufanya hivyo kwa Wachina wakafeli, kwa Waamerika wengi hawajafanikiwa watakavyo, kwa waarabu bado wanapambana.....

Kwanini sisi watudrive ilihali tuna wasomi wa kutoka vyuo vikuu wanaojua kureason kwa miaka zaidi ya 40 sasa?
Historia ya nchi yetu uanze kuihesabu kuanzia mwaka 1961, kabla ya hapo tulikuwa vikabila kabila, na vikoo koo hivi.

Disadvantage tuliyonayo ni kwamba nchi yetu ni changa, wasomi wetu walirithi elimu ya mkoloni, na ukirithi kitu bila mizizi yake kuna sehemu tutafika tutakwama. Again Elimu ya Kujitegemea ililenga kuunganisha elimu ya darasani na mizizi ya jamii watoto tulipotoka ili kwamba kuwepo na uhusiano wa moja kwa moja kati ya ujuzi, maarifa na manufaa katika jamii.

Disadvantage nyingine ni kwamba baada ya ukoloni tulihitaji maendeleo ya haraka sana, ili nchi iwe na wasomi walau wa kuendesha nchi kisasa tulipeleka watu wetu waende kusoma karibu dunia yote Ulaya, Marekani, Urusi, n.k. Hiyo kachumbari ya Elimu waliyoipata sidhani kama ndicho kilichofaa kwa mazingira ya nchi yetu iliyohitaji Elimu ya Kujitegemea. Pengine ni makosa yetu, lakini hiyo haimaanishi kwamba hatuwezi kuanza upya na kufanya jambo sahihi leo hii.
 
Sina hio reason capacity Mkuu..just nimeeleza tu..Ili kumchangia thread ..πŸƒπŸƒπŸƒ
 
Sizonje yuko sahihi tatizo jinsi ya kuwakilisha hoja
Hana tafiti yoyote ya kutetea hoja yake. Hoja ya kisayansi hujibiwa kwa tafiti na si hotuba za jukwaani. Anaweza kuwa sahihi, lakini anakosa uthibitisho. Ushawishi upo kwenye siasa si kwenye science.
 
Na anae ahidiwa maji anashangilia na vigelegele kwa fujo. Hamuulizi mtoa ahadi sababu ya kushindwa kwa miaka 60 kuifanya hiyo kazi. Zaidi ya miaka 60 hana kampuni kubwa za wazawa , kila mradi mkubwa unafanywa na makampuni ya kigeni .
 
Umeongea point ,ilibidi uanzishe Uzi wako. Dr. Kaongea kitoto sana
 
Wala corona haitaisha kwa chanjo ya mabeberu
 
Akina nani wanamshambulia ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…