Who influenced Nyerere: His Ujamaa Philosophy and Azimio Principles?

Who influenced Nyerere: His Ujamaa Philosophy and Azimio Principles?

Sasa tujiulize ilikuwaje ghafla katika miaka ya 70 JKN aliingiwa nini akilini mpaka akakubali viongozi waanze kutumia nguvu za dola kulazimisha wananchi waende kuishi misituni?Nini kilisababisha fikra za JKN zibadilike na aanze kutekeleza yale ambayo hakuyadhamiria hapo awali? Hivi hayo mawazo yake ya mwanzo nayoyanukuu hapo chini kutoka kwenye hicho kijitabu chake cha sera yana tatizo gani - mbona mengine wanayaiga kwenye hizi refomuzi tulizoletewa na hao hao ambao sasa wanabeiliauti na kutaifisha makampuni yao?.,!

Companero,

Nina deni kwako kukujibu kuhusu kauli ya uvivu wa Mtanzania(Mwafrika), nilikuwa nimekujibu, bila kufahamu mitambo ilipoteza mawasiliano kwa muda, hivyo majibu yangu yakapotea. Lakini nitakujibu swali na masikitikmo yako baaday.

Kwenye hili uliloliuliza hapa juu, nafikiri baada ya vurugu zote za 60's mpaka kifo cha Karume an Obote Kupinduliwa, Nyerere si ajabu aliingiwa na na Paranoia!

Ilipokuwa kitu kuhusu Usalama wa Taifa au Usalama wa uongozi wake, nafikiri woga ulimtawala kimawazo na hivyo kama Kawawa au DC fulani waliwasilisha habari ambazo zilionekana credible on surface, Nyerere inawezekana aliidhinisha hatua za kidola kufanya kazi.

Sasa wale wanaompinga Nyerere watasema mbona yeye hakusimama kidete bila woga? Waswahili wanasema, "kwa mwgoa hakujaenda kilio" au wengine husema "kinga ni bora kuliko tiba"

Sasa kama aliamua kutumia madaraka yake iwe kwa kuweka watu kizuizini au kamata kamata ili kuwepo hali ya utulivu na kuzuia mawazo ya kuleta chokochoko ambazo zingehatarisha ustawi na usalama wa Taifa letu changa ambalo lilikuwa ndio linaanza kujijenga kiuchumi, kisiasa na hata kiitikadi huku likijihami na Ubeberu na ubabe wa Makaburu, Ian Smith na Wareno wa Msumbiji, je tutasema haikuwa haki yake kutumia madaraka yake kwa manufaa aliyoyaona kuwa ni ya Taifa?

Leo hii tunapata nafasi nzuri kumchambua na kutofautisha ni yapi aliyoyafanya yalikuwa mazuri na ni yapi yalikuwa si sahihi na mabaya. Lakini tusimnyime haki yake kuwa alifanya mengi kwa nia ya kulijenga Taifa imara.

Kama Nyerere angekuuwa hana utu, basi wengi wangeuawa, angekuwa ni tajiri wa kupindukia na si ajabu angekua anaishi ukimbizini!

Nyerere aliwaamini sana wasaidizi wake. Wengi walifanya mambo na kumletea kila aina ya habari na aliwasikiliza na kuwapa uhuru ambao leo hii, tunaupinga!

Leo DC anakuwa huru tunadai ana nguvu nyingi. Lakini katika pumzi hiyo hiyo, tunataka demokrasia na DC wawe na uwezo wa kujiamulia.

Zoezi la Vijiji vya Ujamaa, Uhujumu Uchumi, Operesheni Maduka na mengine mengi ambayo yalikwenda kombo, mabaya yaliyotokea hakuyafanya Nyerere. Kosa lake ilikuwa kushindwa kusitisha uonevu ulipotokea.

Hilo nitakuwa wa kwanza kusimama mbele kulitamka na bado mapenzi na heshima yangu kwa Nyerere hayatabadilika!

Historia inatufundisha mengi, labda sasa ni wakati tuwafuate kina Mwinyi, Malecela, Msuya, Kingunge, Kawawa na wazee wengine waliokuwa madarakani kati ya mwaka 1967-1985, tuwaulize, nini kilitokea hasa baada ya mauaji ya Karume na Tanzania ikaanza kudidimia na ubabe wa Serikali na TANU/CCM kushika hatamu?

Tuwaulize hawa ndugu, je Nyerere alikuwa mtu wa namna gani miaka hiyo baada ya Azimio la Arusha na Uasi wa kina Kambona?
 
"But we must add to these [three] principles [of the Ujamaa family] the knowledge and the instruments necessary for the defeat of the poverty which existed in traditional African society. In other words, we must add those elements which allow for increased output per worker, and which make a man's efforts yield more satisfactions to him."

"We must take our traditional system, correct its shortcomings, and adapt to its service the things we can learn from the technologically developed societies of other continents."

"It is obvious, however, that with the variations in potential in soils and in social customs, it would be absurd to set down one pattern of progress or one plan which must be followed by everyone."

"What is necessary is the objective of an ujamaa commuity. The interim steps and the detailed organization should be adapted to the local circumstances - which includes an understanding of the people's traditional attitudes as well as the degree of the people's political understanding and their acceptance of this social objective"

"It is essential to realize that within the unity of Tanzania there is also such diversity that it would be foolish for someone in Dar es Salaam to try to draw up a blueprint for the crop production and social organization which has to be applied to every corner of our large country"

"Principles of action can be set out, but the application of these principles must take into account the different geographical and geological conditions in different areas, and also the local variations in the basically similar traditionals structures."

"For example, in the Kilimanjaro Region not only is the practice of individual land-holding [Kihamba system] almost universal, but also there is no unused land on the mountain. This affects social attitudes and create some family problems which do not exist in those parts of Tanzania where a young man can get land of his own quite near to his father's farm as soon as he is ready to start his own family. Again, some part of our country suffer from great water shortage or uncertainty; their agricultural organization, their density of population - and thus their social organization - must inevitably take account of these facts, just as the organization in well-watered areas must take advantage of its greater potential. All these things affect what can be grown, and the degree of investment in land or the implements which is necessary for a given output. It would be absurd to try and settle all these questions from Dar es Salaam, particularly as such variations as those of the type of soil sometimes occur within a very small area. Local initiatives and self-reliance are essential"

"The social customs of the people also vary to some extent. The Masai are traditionally a nomadic cattle people; their family structure, their religious beliefs, and other things, have been shaped by this fact. They are therefore somewhat different from the social beliefs and organization of, for example, the traditionally agricultural Wanyakyusa. The steps which will be necessary to combine increased output with social equality may therefore also vary; the important thing is that the methods adopted should not be incompatible with each other, and should each be appropriate for the attainment of the single goal in a particular circumstance."

"'[T]here must also be an efficient and democratic system of local government, so that our people make their own decisions on the things which affect them directly, and so that they able to recognize their own control over community decisions and their own responsibility for carrying them out."

"In Tanzania it is clear that as a general rule new development of this kind should be operated by the public, although some private or joint private and public investment may be appropriate in certain cases where expertise or capital is an immediate problem."

"Marketing must be properly organized so that, even while our nation is in grip of international market forces which contol world prices, still we get the maximum possible for our goods, and our producers - that is, our farmers - get a fair return for their contribution to the national wealth."

Haya mambo JKN aliyafikiria 1967!Huyu Mzee aliona mbali sana! 'He wa far ahead of his time - it seems he is even far ahead of our time'! Ndio maana bado hatumuelewi, labda tutamuelewa mwaka 2050 baada ya MDGs2015, MKUKUTA2005+, MINITIGER2020 na VISION2025 kutimiza ile methali ya 'mbio za sakafuni huishia ukingoni'!Nadhani aliliona hilo ndio maana alisisitiza kuwa 'mwisho wa siku tutayarudia maadili na misingi muhimu ya Ujamaa'!Na mwisho wa siku ndio huu wa EPA, KAGODA, RICHMOND, MEREMETA,TANGOLD, BUZWAGI, TULAWAKA,....,!

Mzee Companero,

Wengi wanaompinga Nyerere hata rafiki yetu mchumi Zakumi, wanampinga kwa kutumia reaction ya walichokiona na kuamini hiki ndicho.

Ukimuuliza Zakumu kama kakisoma hiki kitabu ambacho umenukuu vifungu kadhaa atakwambia hakuona haja yeyote kuvisoma kwa kuwa kimejaa "upupu".

Sasa nikitumia fasihi, "Upupu" ulioko kwenye haya maandiko, hata Azimio la Arusha ni ukweli ambao hawautaki kuusikia, kwa kujidai kuwa wao wana mawazo na mbinu za Kisasa.

Wengi wanaompinga Nyerere, hawajawahi kuka chini na kusoma vitabu vyake na kuelewa kilichoandikwa.

Naona umeleta bandiko kutoka Hatima ya uongozi. Ikiwa Nyerere alikiandika hicho 1994-1995, na sisi leo tunakirudia kwa nguvu kubwa dhidi ya CCM na Kikwete, je hatuoni kuwa tulipuuzia kuelewa maana ya kilichoandikwa nyakati zile zile yalipoandikwa na leo tunahamaki na kubaini kuwa "upupu" unawasha na ulikuwa ni ukweli kutuzindua?

Hivi kweli kama tungekuwa na Wanasiasa na Watendaji makini ambao wangechukua muda kusoma vitabu vya Nyerere au miongozo yake nyakati zile na kujiamini kuwa yaliyoandikwa yanawezekan, hivi leo si tungekuwa sawa na Misri, Morocco au hata Ugiriki kiuchumi?

Mwinyi aliposema Uchumi tumeukalia, tuligeuza kauli na kuifany alugha ya mtaani kuwa ni makalio! Lakini ni kweli tunakalia uchumi na hata mawazo na mipango imara ya kulijenga Taifa letu, tunaipuuzia na kukimbilia kutafuta win win solution kutoka kwa IMF/WB!

Mkapa alisema, Watanzania ni wavivu, tukakasirika sana. Kikwete kasema majuzi, tutumie Sayansi, tumemdhihaki, lakini ikipita miaka 20, tutazitafuta hotuba hizo za kusema Watanzania ni Wavivu na Watanzania tutumie Sayansi na kuanza kujutia ni kwa nini hatukuzifanyia kazi zilipotolewa kauli hizo na kujirekebisha!

Nyani Ngabu kasema, Ndivyo tulivyo, kauli mbiu hiyo inaelekea kuwa ni kweli kila siku!
 
Ilipokuwa kitu kuhusu Usalama wa Taifa au Usalama wa uongozi wake, nafikiri woga ulimtawala kimawazo na hivyo kama Kawawa au DC fulani waliwasilisha habari ambazo zilionekana credible on surface, Nyerere inawezekana aliidhinisha hatua za kidola kufanya kazi.

Blaming Kawawa for Nyerere's sins jamani, masikini mzee wa watu. Kweli Nyerere ku crack down on dissent na haki za watu tuna mu impute Kawawa jamani, jamani. Daaaah! Au, maamuzi ya Ikulu tuna wa impute ma district commisioners ? Sio vizuri hata kidogo. Kawawa akisoma hicho ulichoandika atasikitika sana.
 
Tuwaulize hawa ndugu, je Nyerere alikuwa mtu wa namna gani miaka hiyo baada ya Azimio la Arusha na Uasi wa kina Kambona?

Kishoka,

alikuwa ni dikteta, asiyesikia la muhadhini msikitini wala la mpiga kengele kanisani!! dikteta, kwenye ligi moja na kina Tito!!
 
Blaming Kawawa for Nyerere's sins jamani, masikini mzee wa watu. Kweli Nyerere ku crack down on dissent na haki za watu tuna mu impute Kawawa jamani, jamani. Daaaah! Au, maamuzi ya Ikulu tuna wa impute ma district commisioners ? Sio vizuri hata kidogo. Kawawa akisoma hicho ulichoandika atasikitika sana.


There you go again Bwana Kuhani, always trying to pick and choose what you think witll be a talking point!

Did you read the whole response or you just chose to pick what you think suite your obsessive desires?

You are better that that Bwana!
 
Kishoka,

alikuwa ni dikteta, asiyesikia la muadhini msikitini wala la mpiga kengere kanisani!! dikteta, kwenye ligi moja na kina Tito!!

YNIM,

Wewe ni mtaalamu, dakitari wa mambo ya sayansi na saikolojia, nilitarajia kupata jibu from clinical and medical perspective describing Nyerere's Paranoia and not a cheap response ya kiukanjanja kama jamaa yako Nyani anavyojibu kuhusu Kisura na Mjaluo😱
 
Rev.Kishoka,Kuhani,YNIM,

..hakuna mwalimu mzuri wa falsafa za Nyerere kama life experience/kuishi wakati wa utawala wake.

..Nyerere alitaifisha mashamba yaliyokuwa yakizalisha kwa faida, alipoondoka madarakani mashamba hayo yalikuwa mzigo kwa walipa kodi.

..Nyerere alianzisha viwanda lukuki, vikafanya kazi miaka miwili mitatu, alipoondoka vilikuwa sawa na magofu.

..Nyerere alikuta vyama vya ushirika vilivyokuwa na umri wa miaka 30 na kuendelea. akavivunjilia mbali na kuanzisha mamlaka ya mazao zilizoishia kuwakopa wakulima.

..Mwalimu alitaifisha mashirika na makampuni mengi binafsi yaliyokuwa yakifanya kazi kwa ufanisi, kuajiri na kulipa kodi. alipoondoka makampuni hayo yalikuwa yanakaribia kufa.

..hayo niliyoyaeleza hapo juu kwangu mimi ni somo/shule tosha ya maandiko ya Mwalimu Nyerere.

..somo kubwa zaidi ni kwamba; maandiko yoyote yawe ya Ujamaa, au Ubepari, yana ushawishi mkubwa sana ktk makaratasi, kinachogomba ni wakati wa utekelezaji.

..

NB:

..wakati Nyerere anangatuka nafasi ya uenyekiti wa CCM alimpendekeza Kawawa kuwa Makamu mwenyekiti.

..katika kuelezea wasifu mrefu wa Kawawa, Mwalimu alieleza kwamba Kawawa alipokea lawama nyingi kwa kutekeleza maamuzi yaliyotokana na vikao, au maagizo yake Mwalimu.

..sasa nashangaa hapa watetezi wa Mwalimu wanataka kumbebesha lawama zote Mzee Kawawa.

..zaidi, natatizwa kidogo na sincerity ya Mwalimu. nakumbuka ktk hotuba hiyo alilia machozi. kwanini hakumtetea Kawawa when it realy mattered, badala yake anakuja kusema baada ya miaka mingi kupita, na Kawawa ameshachafuka?
 
Mchungaji hivi hapo 'Ivy League' ulipo hakuna makabrasha yanayoonesha jinsi gani hii 'discourse/ideology', yaani, mtazamo uliojificha wa kiitikadi wa kudai kuwa waafrika na 'watu weusi' kwa ujumla ni wavivu ulivyoanzishwa na wakoloni na wabaguzi wa rangi ili kujipa moyo kuwa ni haki kabisa kututawala na kututumikisha? Kama waafrika ni wavivu ilikuwaje tukatumikishwa sana kama watumwa kujenga miji ya Liverpool huko Uingereza, Boston huko Marekani, Cape Town kule Afrika Kusini na sehemu mbalimbali duniani? Kama sisi ni wavivu sana kwa nini tulikata sana katani kama manamba kule Tanga na kuongeza sana pato la Serikali ya Mkoloni wa Tanganyika?

Kwa kweli Mchungaji umenisikitisha sana. Kuna makala ya Ayub Ryoba inaongelea jinsi gani watu hawa hawa unaowaita wavivu hapa Bongo wanavyopiga mzigo kinoma huko Ulaya. Kaisome maana hayo maboksi mnayoyabeba huko mpate dola 7 kwa siku hapa Bongo mkiambiwa myabebe hamtakubali alafu mtaitwa mvivu. Leteni utaratibu wa kulipana kwa masaa hapa Tanzania uone jinsi madei waka watakavyopiga mzigo kama hawana akili nzuri! Yaani, kha, kweli hawa wamachinga na wabeba mikokoteni mchana kutwa kwenye hili jua kali la Dizim ni wavivu?

Companero,

Ikiwa uzalishaji mali wetu na kujituma ulikuwa marudufu wakati tukiwa tunatawaliwa na mijeledi migongoni ikitusukuma, iweje leo tuko huru tumelegeza uzi na kuachia kamba tukiporomoka?

Tumechangia neema ya Mabepari na Wakolonisi kwa hiyari bali kwa kushurtishwa.

Kama tungechangia neema yao kwa hiari, basi nasi tungekuwa tumeendelea kama wao na lile bakuli wanalorithishana viongozi wetu la kuomba misaada lisingekuwepo.

Sasa kama si uvivu kujituma kuwa wachapa kazi na wazalishaji mahiri tukiwa huru ni kitu gani?

Leo tuko huru miaka karibu 50, bado hatuna nguvu za utashi na kujisukuma wenyewe kujitosheleza au kufanya kazi kwa bidii.

Angalia jinsi uzalishaji mali na kufanya kazi kulivyoborongwa chini ya utawala binafsi na uongozi wa Mtanzania!

Mashirika na viwanda yanakufa, huduma ni mbovu lakini kila shirika la mzungu, mhindi, mwarabu au hata waafrika wenzetu wenye kutuchapa mijeledi, kuna nidhamu ya hali ya juu na huko ndiko unaona jinsi Watanzania wanachapa kazi na hata pato kubwa la Serikali linatoka huko kwenye umiliki wa Mgeni anayetumia mijeledi!

Umezungumzia mashamba ya katani, tuongeze wigo na kusema kilimo kwa ujumla.

Mkoloni alikuwa akitulazimisha tumlimie heka 100, anatupa heka moja tujilimie tujilishe. Mkoloni kaondoka, tumeona hakuna tena faida ya kulichukua shamba zima na kujizalishia wenyewe, tumeng'ang'ania kale ka heka kamoja ketu, humo tunajaza maharage, nyanya, mahindi na muhogo, tukiuita mseto.

Zile heka 100 anakuja mwingine mwenye nguvu kuzichukua na kuwekeza, tunalalamika, akitumia mijeledi kutuajiri tumzalishie tunalalamika na kulia.

Angalia kule TPC jinsi wafanyakazi na vibarua kwenye mashamba ya Sukari walipotoa kilio kusikia kuwa Mashamba yanabinafsishwa kwa kuwa ni hasara tupu na tuna mpa mwenye uwezo kuzalisha atulipe kodi!

Kwa nini kama Taifa tumefikia hatua kuwa ile dhamira ya kujenga Taifa linalojitegemea imepotea kabisa na tunabakia kutafuta njia fupi na za urahisi na haraka haraka bila kutoka jasho kujipatia mapato?

Na hili si la Watanzania wananchi pekee ni mpaka kwenye Serikali na uongozi wa nchi.

Nitakachokubali kuwa nilikosea katika kauli yangu ni kutoa tamko ambalo linamaanisha Watanzania wote.

Nitabadili kauli yangu kutoka kusema Watanzania ni Wavivu na kuwa Watanzania wengi ni Wavivu, ikiwa na maana si yote, maana kuna wachache kati yetu ambao hujituma bila kusubiri kusukumwa na hao ndio wale walibaoni umuhimu wa kujitegemea kwa kutumia juhudi na maarifa.

Angalia Mpemba, Machinga na Mchaga wanavyochacharika kujitafutia. Nenda kila kona ya Tanzania utamkuta Mpemba, Machinga na Mchaga wakifanya kazi za kujitegemea na kujiajiri,wakitumia nafasi yeyote kuchapa kazi iwe ni biashara, huduma au kilimo kuzalisha mali.

Ukimkuta Mhehe, Msukuma Mpare, Mkurya, Mnyaturu, hata Mkwere ni kibarua kaajiriwa akisubiri ujira😉

Gharama za kujenga Taifa ni kubwa na mtaji wake wa kwanza ni kwa Wananchi wake kujitoa muhanga na kujituma kwa kutumia juhudi, maarifa, ufanisi na ubunifu katika uzalishaji mali.

Sisi hatutaki gharama wala kuingia gharama iwe ni kutumia misuli yetu, kutoka jasho au maarifa yetu. Mbaya zaidi tumejiunga na viongozi wetu kutafuta suluhisho la umasikini wetu kwa kumtafuta mtu mwingine aje atutatulie matatizo yetu na kutufanyia kazi!

Hivyo Mzee Companero, uvivu wetu utakoma pale tutakapoweza kujitosheleza na kuachana na utegemezi. Uvivu wetu utakoma pale tutakapojituma tukiwa huru na hata kujitegemea kwa uhuru wetu na si kwa kutumikia wengine au kuogopa mijeledi!
 
YNIM,

Wewe ni mtaalamu, dakitari wa mambo ya sayansi na saikolojia, nilitarajia kupata jibu from clinical and medical perspective describing Nyerere's Paranoia and not a cheap response ya kiukanjanja kama jamaa yako Nyani anavyojibu kuhusu Kisura na Mjaluo😱

LOL.......weekend njema!!!😀
 
..wakati Nyerere anangatuka nafasi ya uenyekiti wa CCM alimpendekeza Kawawa kuwa Makamu mwenyekiti.

..katika kuelezea wasifu mrefu wa Kawawa, Mwalimu alieleza kwamba Kawawa alipokea lawama nyingi kwa kutekeleza maamuzi yaliyotokana na vikao, au maagizo yake Mwalimu.

..sasa nashangaa hapa watetezi wa Mwalimu wanataka kumbebesha lawama zote Mzee Kawawa.

..zaidi, natatizwa kidogo na sincerity ya Mwalimu. nakumbuka ktk hotuba hiyo alilia machozi. kwanini hakumtetea Kawawa when it realy mattered, badala yake anakuja kusema baada ya miaka mingi kupita, na Kawawa ameshachafuka?

Ningetumia jina la Malecela au mtu mwingine, haya mnayodai kumbebesha Kawawa lawama yasingetoka mioyoni mwenu.

Ukirudia nilichosema, nimetamka kuwa ni maoni yangu Nyerere alikuwa na Paranoia, kiasi kila alichoambiwa na wasaidizi wake kuwa kuna njama, au chochote mbaho hakiendani na sera zake au mawazo yake, aliruhusu yaliyotoka yatokee.

Hivyo kauli yako na hata ya Kuhani kudai nambambikia lawama Kawawa ni kuzungusha na kuheresha umma japo mpate cha kusema kuwa siye wapenzi wa Nyerere ni vipofu.

Umesema hapa inakutatiza kuwa ilimchukua muda Nyerere kukiri lawama dhidi ya Kawawa, lakini si afadhali alikuja na kuw amuwazi na kukiri udhaifu wake baada ya kuondoka katika madaraka na kukaa barazani kama sisi na kupima aliyoyafanya?

Kila mara mwanadamu anapopata nafasi ya kufanya reflection, huwa hayupo katika hali ya awali, huwa katika sehemu nyingien ya maisha na ndipo huweza kwa urahisi na kwa utu kujiona pale alipopotoka na hata kutaka kujisahihisha!
 
Mzee Companero,

Wengi wanaompinga Nyerere hata rafiki yetu mchumi Zakumi, wanampinga kwa kutumia reaction ya walichokiona na kuamini hiki ndicho.

Ukimuuliza Zakumu kama kakisoma hiki kitabu ambacho umenukuu vifungu kadhaa atakwambia hakuona haja yeyote kuvisoma kwa kuwa kimejaa "upupu".

Sasa nikitumia fasihi, "Upupu" ulioko kwenye haya maandiko, hata Azimio la Arusha ni ukweli ambao hawautaki kuusikia, kwa kujidai kuwa wao wana mawazo na mbinu za Kisasa.

Wengi wanaompinga Nyerere, hawajawahi kuka chini na kusoma vitabu vyake na kuelewa kilichoandikwa.

Naona umeleta bandiko kutoka Hatima ya uongozi. Ikiwa Nyerere alikiandika hicho 1994-1995, na sisi leo tunakirudia kwa nguvu kubwa dhidi ya CCM na Kikwete, je hatuoni kuwa tulipuuzia kuelewa maana ya kilichoandikwa nyakati zile zile yalipoandikwa na leo tunahamaki na kubaini kuwa "upupu" unawasha na ulikuwa ni ukweli kutuzindua?

Hivi kweli kama tungekuwa na Wanasiasa na Watendaji makini ambao wangechukua muda kusoma vitabu vya Nyerere au miongozo yake nyakati zile na kujiamini kuwa yaliyoandikwa yanawezekan, hivi leo si tungekuwa sawa na Misri, Morocco au hata Ugiriki kiuchumi?

Mwinyi aliposema Uchumi tumeukalia, tuligeuza kauli na kuifany alugha ya mtaani kuwa ni makalio! Lakini ni kweli tunakalia uchumi na hata mawazo na mipango imara ya kulijenga Taifa letu, tunaipuuzia na kukimbilia kutafuta win win solution kutoka kwa IMF/WB!

Mkapa alisema, Watanzania ni wavivu, tukakasirika sana. Kikwete kasema majuzi, tutumie Sayansi, tumemdhihaki, lakini ikipita miaka 20, tutazitafuta hotuba hizo za kusema Watanzania ni Wavivu na Watanzania tutumie Sayansi na kuanza kujutia ni kwa nini hatukuzifanyia kazi zilipotolewa kauli hizo na kujirekebisha!

Nyani Ngabu kasema, Ndivyo tulivyo, kauli mbiu hiyo inaelekea kuwa ni kweli kila siku!

Rev:

Mjadala mzima ni Nyerere na kilichomwamasisha kuja na siasa ya ujamaa na Azimio la Arusha.

Kwanza Nyerere alikuwa muumini mzuri wa Kanisa Katoliki kabla ya kuanza na siasa ya Ujamaa.

Alipokuwa masomoni alijifunza usoshalist na siasa za mlango wa kushoto. Siasa hizi zilizungumza mambo mengi mazuri kuhusu maendeleo ya binadamu lakini zilizikuwa ni siasa zilizomkataza kwa kiasi kikubwa mambo ya dini (materialism).

Kwa maoni yangu Nyerere alitaka asipoteze Imani ya Mungu lakini wakati huohuo alitaka siasa za mlango wa kushoto ambazo zilimpa matumaini kuwa ndizo zenye uwezo wa kuweza kumuendeleza masikini.

Kitu kingine kilichompa hamasa ni siasa za kisoshalisti zilizofuatwa na wasomi wa Ulaya Magharibi. Wasoshalisti wa Ulaya Magharibi waliamini kuwa ukisomesha watu, utawapa nguvu ya kubadili mazingira yao na kufikia usoshalisti wa kisayansi bila kumwaga damu.

Wale wa Ulaya mashariki, walikuwa wanaamini kuwa ni mapinduzi ndio pekee yanayoweza kubadilisha jamii kufikia usoshalisti wa kisayansi. Hivyo Ulaya mashariki, mtu akiwa na mawazo ya ulanguzi ata kama wa kuuza ugoro basi adhabu yake ni kubwa. Kwa sababu waliamini masikini mwenye mawazo ya kibepari ni adui mkubwa kwa usoshalisti kama bepari mwenyewe.

Hivyo sehemu kubwa ya Ujamaa wa Nyerere ni kujenga usawa kama wasoshalisti. Lakini Ujamaa utofautiane na usoshalisti kwa kutoa nafasi kwa watu kuamini dini zao. Na vilevile atumie elimu ya siasa kuwabadilisha watu, hili weweze kujenga jamii yenye usawa.

Kama angejuwa kuwa elimu ya siasa haiwezi kumbadilisha mtu kuwa mjamaa naamini angelisaidia taifa sana. Kwa sababu ujamaa ungejengwa kwa mabavu na kumwaga damu kitu ambacho kingempa taabu katika imani yake ya dini.

Kitu ambacho sipendi siasa za Nyerere ni siasa zilizojaa maneno. Ujamaa ni maneno. Azimio la Arusha ni maneno. Maneno haya hayajibu mahitaji ya binadamu kwa sababu binadamu anabadilika.
 
Kumbe ni wewe Tuta, nilikuwa nakutafuta sana na wale wapinzani wenzako wa JKN kule DHB ya enzi zile. Kumbuka mlikubali wito wangu wa kurejea Tanzania tunoe bongo zetu, tuangalie wapi tulijikwaa na tusawazishe pale JKN alipochemka. Najua mna uchungu sana na JKN tena uchungu binafsi unaochochewa na aliyowafanyia aidha ninyi, wazazi wenu,ndugu zenu au marafiki zenu wa karibu hasa wale waliokuwa wameanza kuwini maisha wakati wengine wanalosti. Msameheni tu mzee wa watu. Na yeye pia alikuwa anataka tuwe na 'wini-wini situesheni'.

Sasa rudini jamani rudini nyumbani tulete hayo mabadiliko ili tuondoe ule ubaya wote ambao mnadai tumerithi kutoka kwa JKN, yaani woga wa kuthubutu, ukosefu wa ufanisi kazini, ukiritimba wa mawazo n.k. Ila mkumbuke daima lazima tuanze mwanzo na mwanzo wa Tanzania ni JKN na sera zake za Ujamaa na Kujitegemea. Lazima tuanze kwa kuangalia asili ya fikra na dhana za JKN kwa undani kama swali kuu la mada hii ya Mchungaji inavyoonesha.

Narudia tena kuwa JKN mwanzoni hakuwa na nia kabisa ya kuwaburuza Watanzania ndio maana kwenye toleo la mwaka 1967 la kijitabu chake cha sera cha 'Socialism and Rural Development', yaani 'Ujamaa na Maendeleo Vijijini' alisema kila jamii itabidi ibuni mbinu zake yenyewe kuendelea maana huwezi kuwa na mbinu hiyo hiyo ya maendeleo kwa Mmasai aliyebobea zaidi kwenye ufugaji na Mnyakyusa ambaye amejikita zaidi kwenye ukulima.

Sasa tujiulize ilikuwaje ghafla katika miaka ya 70 JKN aliingiwa nini akilini mpaka akakubali viongozi waanze kutumia nguvu za dola kulazimisha wananchi waende kuishi misituni?Nini kilisababisha fikra za JKN zibadilike na aanze kutekeleza yale ambayo hakuyadhamiria hapo awali? Hivi hayo mawazo yake ya mwanzo nayoyanukuu hapo chini kutoka kwenye hicho kijitabu chake cha sera yana tatizo gani - mbona mengine wanayaiga kwenye hizi refomuzi tulizoletewa na hao hao ambao sasa wanabeiliauti na kutaifisha makampuni yao?

"But we must add to these [three] principles [of the Ujamaa family] the knowledge and the instruments necessary for the defeat of the poverty which existed in traditional African society. In other words, we must add those elements which allow for increased output per worker, and which make a man's efforts yield more satisfactions to him."

"We must take our traditional system, correct its shortcomings, and adapt to its service the things we can learn from the technologically developed societies of other continents."

"It is obvious, however, that with the variations in potential in soils and in social customs, it would be absurd to set down one pattern of progress or one plan which must be followed by everyone."

"What is necessary is the objective of an ujamaa commuity. The interim steps and the detailed organization should be adapted to the local circumstances - which includes an understanding of the people's traditional attitudes as well as the degree of the people's political understanding and their acceptance of this social objective"

"It is essential to realize that within the unity of Tanzania there is also such diversity that it would be foolish for someone in Dar es Salaam to try to draw up a blueprint for the crop production and social organization which has to be applied to every corner of our large country"

"Principles of action can be set out, but the application of these principles must take into account the different geographical and geological conditions in different areas, and also the local variations in the basically similar traditionals structures."

"For example, in the Kilimanjaro Region not only is the practice of individual land-holding [Kihamba system] almost universal, but also there is no unused land on the mountain. This affects social attitudes and create some family problems which do not exist in those parts of Tanzania where a young man can get land of his own quite near to his father's farm as soon as he is ready to start his own family. Again, some part of our country suffer from great water shortage or uncertainty; their agricultural organization, their density of population - and thus their social organization - must inevitably take account of these facts, just as the organization in well-watered areas must take advantage of its greater potential. All these things affect what can be grown, and the degree of investment in land or the implements which is necessary for a given output. It would be absurd to try and settle all these questions from Dar es Salaam, particularly as such variations as those of the type of soil sometimes occur within a very small area. Local initiatives and self-reliance are essential"

"The social customs of the people also vary to some extent. The Masai are traditionally a nomadic cattle people; their family structure, their religious beliefs, and other things, have been shaped by this fact. They are therefore somewhat different from the social beliefs and organization of, for example, the traditionally agricultural Wanyakyusa. The steps which will be necessary to combine increased output with social equality may therefore also vary; the important thing is that the methods adopted should not be incompatible with each other, and should each be appropriate for the attainment of the single goal in a particular circumstance."

"'[T]here must also be an efficient and democratic system of local government, so that our people make their own decisions on the things which affect them directly, and so that they able to recognize their own control over community decisions and their own responsibility for carrying them out."

"In Tanzania it is clear that as a general rule new development of this kind should be operated by the public, although some private or joint private and public investment may be appropriate in certain cases where expertise or capital is an immediate problem."

"Marketing must be properly organized so that, even while our nation is in grip of international market forces which contol world prices, still we get the maximum possible for our goods, and our producers - that is, our farmers - get a fair return for their contribution to the national wealth."

Haya mambo JKN aliyafikiria 1967!Huyu Mzee aliona mbali sana! 'He wa far ahead of his time - it seems he is even far ahead of our time'! Ndio maana bado hatumuelewi, labda tutamuelewa mwaka 2050 baada ya MDGs2015, MKUKUTA2005+, MINITIGER2020 na VISION2025 kutimiza ile methali ya 'mbio za sakafuni huishia ukingoni'!Nadhani aliliona hilo ndio maana alisisitiza kuwa 'mwisho wa siku tutayarudia maadili na misingi muhimu ya Ujamaa'!Na mwisho wa siku ndio huu wa EPA, KAGODA, RICHMOND, MEREMETA,TANGOLD, BUZWAGI, TULAWAKA,....,!

Nipo hapa. Lakini bado unaboronga big time. Maneno mengi hakuna hata Equation. Nitakujibu vizuri baada ngoja nivute uladi kwanza.
 
Rev:

Hivyo sehemu kubwa ya Ujamaa wa Nyerere ni kujenga usawa kama wasoshalisti. Lakini Ujamaa utofautiane na usoshalisti kwa kutoa nafasi kwa watu kuamini dini zao. Na vilevile atumie elimu ya siasa kuwabadilisha watu, hili weweze kujenga jamii yenye usawa.

Kama angejuwa kuwa elimu ya siasa haiwezi kumbadilisha mtu kuwa mjamaa naamini angelisaidia taifa sana. Kwa sababu ujamaa ungejengwa kwa mabavu na kumwaga damu kitu ambacho kingempa taabu katika imani yake ya dini.

Kitu ambacho sipendi siasa za Nyerere ni siasa zilizojaa maneno. Ujamaa ni maneno. Azimio la Arusha ni maneno. Maneno haya hayajibu mahitaji ya binadamu kwa sababu binadamu anabadilika.

Zakumi,

Hata Biblia na Kurani zimejaa maneno na historia na ni imani ya mtu mmoja mmoja kuamini anachokisoma, kuishika imani na mafundisho anayosoma na ni wajibu wake binafsi kutenda yale anayoaswa afuate katika imani yake!
 
Zakumi,

Hata Biblia na Kurani zimejaa maneno na historia na ni imani ya mtu mmoja mmoja kuamini anachokisoma, kuishika imani na mafundisho anayosoma na ni wajibu wake binafsi kutenda yale anayoaswa afuate katika imani yake!

Rev:

Umesema kweli kuwa Biblia na Kurani zimejaa maneno lakini zile ni Imani. Kwa upande wangu pamoja na kuwa Ujamaa ulisemakana kuwa ni Imani, Ujamaa utabaki kuwa siasa na sera. Kama tunakubaliana kuwa ujamaa ni siasa na sera basi katika kipindi maalumu ni lazima tupime matokeo yake.

Vilevile kuna watu wanajiita waIslamu, waKristo, waYahudi na wengine. Vipimo vya Imani zao ni wakati hukumu itakapotolewa na Mwenyezi Mungu siku ya mwisho.

Ujamaa ni hapa hapa duniani. Na kama ni Imani yapimwe hapahapa duniani. Na kibaya zaidi mnaosema kuwa ujamaa ni Imani mko USA, UK akifuatilia stock zenu.

KUJUA NA KUTOFANYIA KAZI UNACHOJUA NI KUTOJUA KAMILI.
 
Na kibaya zaidi mnaosema kuwa ujamaa ni Imani mko USA, UK akifuatilia stock zenu.

Mimi siko UK wala USA, nipo hapa URT. Karibu sana tujenge nchi ya watu ambao Mwalimu Nyerere aliwatabarukia vitabu vyake vya Ujamaa. Sasa tunaanza upya baada ya SAPs na PRSP kushindwa kazi kwa miaka 28 ambayo ni miaka mingi zaidi ya miaka 10 tuliyotekeleza Azimio la Arusha la Ujamaa na Kujitegemea. Tunaanza kwa kurudisha Mwongozo. Hii itasaidia watumishi wa umma wasichanganye utumishi na biashara binafsi kama walivyochanganya kina Richmonduli. Hivi jiulize inakuwaje waziri awe na biashara ya ndege alafu akipoteza tu uwaziri eti hiyo biashara inafilisikia!Mwongozo utahakikisha kuwa kamwe kodi zetu hazibeiliauti mafisadi!Kwa jasho lao watakula!Ujamaa, kama ulivyo Uhuru, ni kazi!Na hata misahafu inasema asiyefanya kazi na asile!Haisemi liwa ule!
 
Date::2/7/2009
Kunguni waliupekecha ujamaa Tanzania–Mwinyi

Na Elias Msuya
Mwananchi​

WAKATI Tanzania ikiwa bado haieleweki ni siasa ya aina gani inafuata Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi amekata ukimwia na kuweka bayana kuwa, sera ya ujamaa na kujitegemea iliyoasisiwa na Mwalimu Julius Nyerere ilipekechwa na kunguni.

Mwinyi ambaye kwa siku za karibuni ameanza kuhubiri siasa zisizokuwa na unazi wa kichama kama ilivyo kwa mtangulizi wake Mwalimu Nyerere, alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akihutubia katika maadhimisho ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho sasa kimetimiza miaka 32, yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mwembeyanga, Temeke jijini Dar es Salaam.

Alisema sera ya ujamaa iliyoanzishwa na Mwalimu Nyerere ilikuwa nzuri, lakini kutokana na watendaji kutokuwa waaminifu aliowafanananisha na kunguni, sera hiyo ilikufa.

"Baba wa Taifa alianzisha sera ya ujamaa na kujitegemea. Madhumuni yake yalikuwa mazuri mno, mno, mno…Watu waligawana sawa kile walichozalisha kwa usawa. Ilikuwa ni sera iliyokuwa ikiondoa matabaka ya watu. Haya yalikwenda vizuri tu mpaka walipozuka kunguni wakapekecha mfumo," alisema Mwinyi na kuufananisha mfumo wa ujamaa unaodaiwa kuwapo sasa kama mti uliopekechwa na wadudu.

"Unajua mti uliopekechwa, ukiona nje msafi, kumbe ndani kuna uwazi".
Mwinyi alitumia nafasi hiyo kutakasa sera ya soko huria, maarufu kama ruksa, aliyoanzisha mwenyewe baada ya kuingia madarakani kurithi mikoba ya mwalimu mwaka 1985, akisema kuwa hiyo ilikuwa ni hatua ya kurekebisha hali iliyokuwa taabani.

"Waliopekecha mfumo ule walikwenda mbali na sisi tuliomrithi Baba wa Taifa tukagundua hali hiyo jinsi ilivyokuwa mbaya, kiasi ambacho hata ukitaka sabuni dukani hadi upange foleni. Ikabidi tuuweke uchumi mikononi mwa wananchi. Wao walipe kodi tu, lakini kila kitu wafanye wenyewe. Milango na madirisha ikafunguliwa ikawa rukhsa," alisema Mwinyi huku akishangiliwa na wanachama wa CCM waliokuwa wamefurika katika uwanja huo.

Mwinyi pia aliusifu utawala wa awamu ya nne wa Rais Kikwete kuwa umefanya mambo makubwa na hasa kusahihisha makosa ya awamu zilizopita.

Alisema kazi anayoifanya Kikwete kwa sasa ni kurekebisha makosa yaliyofanyika katika awamu ya kwanza, ya pili na ya tatu.

Mwinyi alisema kinachofanyika ni kama mcheza mpira na mtazamaji kwamba, wananchi tunaona makosa ya awamu hii, lakini ukweli ni kwamba makosa mengi yametokea katika awamu zilizopita.

"Mtazamaji siku zote humkosoa anayecheza, sasa awamu ya nne imetazama makosa yale na inarekebisha. Mmeyaona mambo mazuri kabisa yaliyotajwa kama mafanikio ya utekelezaji wa sera za CCM," alisema.

"Tumsifu kijana wetu Kikwete, amefanya kazi nzuri. Amemwaga fedha kwa wananchi, yanaitwa mabilioni ya Kikwete. Juzi juzi tu alikwenda Zanzibar na kuwatangazia wananchi kuwa ataongeza fedha hizo. Ukizipata fedha hizo, zifanyie biashara ili uendelee. Hizo ndiyo sera nzuri za CCM," alisema.

Katika mkutano huo pia Mwinyi alivaa sura ya ubaba wa taifa kama alivyofanya akiwa Mbeya Vijijini, alipowataka wapiga kura kuchagua kiongozi wanayeona anafaa bila kujali vyama, pale aliposisitiza ushirikiano baina vyama vyote vya siasa, akiwataka wana-CCM kuimarisha uhusiano na vyama vya upinzani.

Alisema wapinzani sio maadui, na kwamba Watanzania walikubali wenyewe mfumo wa vyama vingi, yeye akiwa mwasisi wa mfumo huo, licha ya kwamba asilimia 80 walikuwa wameukataa maoni ya asilimia 20 ya watu waliohojiwa yalikubaliwa.

Lakini rais huyo mstaafu tangu mwaka 1995, aliwatupia wapinzani dongo la kushindwa kwao kukua: "tangu wakati huo wamebaki na asilimia 20 zao na CCM imebaki na ushindi wake wa asilimia 80," alisema.


Aliwataka pia viongozi wa CCM kuimarisha ushirikiano na mshikamano na kuwataka wanaoshindwa katika chaguzi ndani ya chama wakubali matokeo.

"Hata wakati wa uchaguzi, mnagombea pamoja, ukishindwa ukubali kushindwa…Kumbukeni Hillary Clinton na Barack Obama wa Marekani, leo Obama amemteua mpinzani wake kuwa Waziri wa Mambo ya Nje."

Aliwakumbusha pia kujiandaa na chaguzi zijazo, Napenda kuwakumbusha wana CCM wenzangu kwamba msisahau kuwa tuna uchaguzi mwaka huu wa Serikali za Mitaa na mwakani tuna uchaguzi mkuu.

Nguo ya kusalia Ijumaa hufuliwa Alhamisi. Kwa hiyo maandalizi yaanze sasa, tusije tukajing'ata vidole. Tujiandae pia kwa kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Kuna waliokuwa wana umri mdogo na sasa wamefikisha umri wa miaka 18, wapo waliopoteza kadi zao…Kazi hii tuifanye sote nikiwamo mimi".

Sherehe hizo ambazo pia zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM mkoa wa Dar es Salaam na wageni maalum kutoka Chama cha ANC cha Afrika Kusini, ni mfululizo wa maadhimisho ya kuzaliwa kwa chama hicho ambazo zinafanyika kitaifa mkoani Shinyanga.

Naye Awila Silla, anaripoti kutoka Singida kuwa, vyama vya upinzani nchini vimetakiwa kuungana ili kuunda chama kimoja chenye sera, ili kuleta changamoto kwa chama tawala badala ya kuendeleza marumbano.

Hayo yalisemwa jana na Spika wa Bunge, Samwel Sitta wakati akitoa salamu kwa wananchi kwenye maadhimisho ya miaka 32 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi katika viwanja vya jengo la CCM Mkoa mjini Singida.

Alisema marumbano mengi yanayotolewa na viongozi wa vyama hivyo, yamekuwa yakileta hisia tofauti bila ya kujenga chochote kwa jamii.

Kutokana na hali hiyo Sitta alisema hakuna haja ya kuwa na mafungu ya vyama vingi visivyokuwa na nguvu, hivyo kusababisha vyama hivyo kukosa sera.


Alisema CCM haitaogopa wala kutetereka ikiwa vyama vya upinzani vitaungana na kuunda chama kimoja, kwani bado kinawaenzi waasisi na wazalendo wa chama hicho waliopita.

Alisema kutokana na uroho wa madaraka kwa baadhi ya watu wamesababisha kuwepo kwa vyama vingi zisivyokuwa makini na havina sera, hivyo kukosa nguvu katika kujinadi.
 
Kwa kweli mzee Mwinyi na Spika Wameongea mambo yenye mantiki na tija kwa taifa hili.

huu in ukomavu wa siaisa za vyama vingi na demokrasia nchini, hongera chama tawala ccm kWA KUWEKA UWANJA mpana kwa kila mtu kuvinjari kivyake.
 
Mzee Mwinyi ni kunguni mwingine tu aliyetafuna taifa. Yeye na mkewe ndio walikuwa wa kwanza kuanzisha biashara Ikulu, wakituuzia Stella Artois na majenereta ya umeme. Sasa anasema nini kuhusu kunguni? It takes one to know one.
 
Mzee Mwinyi ni kunguni mwingine tu aliyetafuna taifa. Yeye na mkewe ndio walikuwa wa kwanza kuanzisha biashara Ikulu, wakituuzia Stella Artois na majenereta ya umeme. Sasa anasema nini kuhusu kunguni? It takes one to know one.


Jasusi:

Wakati mwingine sioni kwanini mna wahukumu watu tu. Inaonyesha Tanzania watu wakifanya biashara primitive mnawakubali. Na wakifanya biashara yenye mtaji mnawakataa.

Kwa mfano rais akiwa anafanya biashara ya kuuza mihogo au mchicha kutoka kwenye shamba lake haonekani mbaya.

Lakini akifanya biashara ambayo watanzania wengine hamwezi tayari anakiuka miiko.
 
Jasusi:

Wakati mwingine sioni kwanini mna wahukumu watu tu. Inaonyesha Tanzania watu wakifanya biashara primitive mnawakubali. Na wakifanya biashara yenye mtaji mnawakataa.

Kwa mfano rais akiwa anafanya biashara ya kuuza mihogo au mchicha kutoka kwenye shamba lake haonekani mbaya.

Lakini akifanya biashara ambayo watanzania wengine hamwezi tayari anakiuka miiko.
Zakumi,
Mimi nisingekuwa na shida kama mkewe rais alikuwa mfanyibiashara kabla ya kuingia Ikulu. Why should they use Ikulu as a stepping stone? That is my question! The same applies to Mama Mkapa.
 
Back
Top Bottom