hivi hawa viongozi wa leo mawazo yao yanatoka wapi?
Sio kweli.
Kulikuwa kuna sababu kwa nini J.K. Nyerere alitaka tuimbe "Zidumu fikra za Mwenyekiti..." Maana yake fikra zingine hazikaribishwi.
Hadithi za kina Mzee Bomani ni historia potofu ambazo anaweza kuhadithia wasioelewa kilichojiri tu. Ukimuuliza Mzee Bomani maoni yake kuhusu Nyerere ni kumpelekea ngedere kesi ya nyani. Hawa wote ndio watendaji, "ndio-mzee," chinja-chinja wa kisiasa na kimatendo katika mkoba wa vifaa vya J.K. Nyerere.
Na, hata kusema J.K. Nyerere haambiliki ni kupendezesha lugha tu. J.K. Nyerere alikuwa nduli wa mawazo, kama sio nduli. Alitumia dola kushughulikia waliotofautiana nae (4). Aliyethubutu kubisha aidha alifungiwa kijijini ( Balozi Kassanga Tumbo (1) au jela (Chief Justice Wolfango Dourado ( 3 ), Abdallah Said Fundikira, Mwinyijuma Othuman Upindo, na James Mapalala (2), kufukuzishwa nchini (Waziri Kambona), kufukuzwa kazi (Rais Jumbe) na orodha inaendelea na kuendelea na kuendelea....(Kassim Hanga, Makamu wa Rais wa Zanzibar, na walinzi wake; Waziri Abdulrahman Mohamed Babu (5), na Wabunge Joseph Kasela Bantu na Mbunge Eli Anangisye, aliyekamatwa na kufungwa bila mashitaka baada ya kuchangia mjadala wa kikao cha Bajeti Bungeni, 1968 ( 6).
Kusema J.K. Nyerere alikuwa ana hoja kali sana kiasi kwamba hakukuwa na wengi wanaoweza kujadiliana nae ni kituko kwa sababu inamaanisha watu wote walikuwa watupu ila Nyerere na wachache fulani. Huku ni kupumbazika kulikotokana na kuleweshwa propaganda. Toka mdogo unaimbishwa nyimbo:
"Kambona, kaolewa!
Wapi? Huko Ulaya
Kambona, kaolewa!
Wapi? Huko Ulaya
Na nani ? Waingereza"
Ni lazima upumbazike. Hata mimi utotoni nilipumbazika. Kuja ukubwani nakuja kuambiwa eti Kambona alilazimika kuingia mitini kwa sababu alitofautiana mawazo ya mfumo wa kiuchumi. Hebu angalia hilo ndugu yangu. Sio nduli wa mawazo huyo J.K. Nyerere? Binadamu kweli unamfunga Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar kwa sababu ametoa hotuba kama mgeni mwalikwa kwenye mkutano wa Tanganyika Law Society kujadili kuboresha na kubadili Katiba! (3) Huyu Muasisi Marehemu J.K. Nyerere utasema kweli sio nduli wa mawazo? Eti, "ilibidi ujenge hoja barabara." Ukipumbazwa unaweza kuamini ya ajabu!
Rev. Kishoka, kama nimetoka nje ya mada ni katika kurekebisha historia inayopotoshwa hapa. Nina marafiki mababa zao wameuawa baada ya kuugulia kwenye vyumba vya giza Oysterbay Polisi baada ya kuswekwa miaka bila mashitaka. Umenikamata nishitaki, usiniweke niugue kisukari na magonjwa ya moyo kwenye chumba cha giza polisi, nikitoka nakaa kidogo nakufa!
( 1 ) The Standard (Tanganyika), 28 Sept. 1962.
( 2 ) Chris Maina Peter; A Comparative Study of the African Human and People's Rights Charter and the New Tanzanian Bill of Rights 31 (Studies in Human Rights No. 10, Consortium on Human Rights Development, University of Denver 1990).
( 3) Ahmed Rajab, Foul Play, Afr. Events, Nov. 1985, at 28.
(4) Chris Maina Peter; Incarcerating the Innocent: Preventive Detention in Tanzania; 1997 The Johns Hopkins University Press, Human Rights Quarterly 19.1 (1997) 113-135
(5 ) H.G. Mwakyembe, Issa G. Shivji; The Parliament and the Electoral Process, in The State and the Working People in Tanzania; 1986 Colin Leys, Tanganyika: The Realities of Independence, in Socialism in Tanzania 187 (East African Publishing House Political Studies 14, Lionel Cliffe & John S. Saul eds., 1972).
(6) Ludovick S Mwijage, The dark side of Nyerere's Legacy; Raymond F. Hopkins, The role of an MP, Swarthmore College
kama alikuwa hataki si angekataza watu kusema hivyo. tatizo nadhani jamaa alikuwa anapenda watu wanaomwambia "yes sir". Huitaji kuwa Rocket scientists kuelewa hilo.Hivi Nyerere aliwahi kuwataka watu kuimba zidumu fikra zake? Hilo tamko au agizo alilitoa wapi na lini na kwa njia gani i.e. hotuba, memo, sheria ya bunge...?
Mzee Mwanakijiji au mwana-jamii yeyote anayemfahamu Mwalimu naomba mniambie kwamba nani alikuwa anamshauri katika mambo yake? kwa sababu hata kama mtu una vision lazima uwe na washauri au kama alikuwa anakwenda na vision yake peke yake. Ni kweli ilibidi watu wam-convice na waende na strong plan ya kum-convice, what if he was hard head yaani alikuwa hamsikilizi mtu? kwa sababu hata wewe unajua kuna watu huku JF ambao hata uwaambiaje hawakubaliani na wewe!. Kwa hiyo hata ukimuambia nini at the end yeye ndiye Raisi na ndio anaamua cha mwisho kwa hiyo sijui kama alikuwa anawasikiliza hao watu au hawasikilizi, na ni kina nani aliokuwa anawasikiliza.
Na haikuwa lazima Nyerere kukubaliana na mawazo ambayo yalikuwa tofauti kabisaa, ila kama alikuwa anasikiliza hata hoja za kuboresha alichokuwa anakifanya yaani Ujamaa. Mimi naona ndio maana hata na Kwame N hawakuelewana kwa sababu ilikuwa ni vigumu sana kumshauri au kumbadili mawazo kwa sababu alikuwa sio mtu wa kubadilika (yaani anachofikiri yeye ndio uamuzi wa mwisho) haya ni mawazo yangu tu.
kama alikuwa hataki si angekataza watu kusema hivyo. tatizo nadhani jamaa alikuwa anapenda watu wanaomwambia "yes sir". Huitaji kuwa Rocket scientists kuelewa hilo.
Sajo,
Kwa niliyoyasikia na kuyafahamu, kuna watu watatu tuu ambao walikuwa washauri wa na wasaidizi wa Nyerere (watendaji) ambao walikuwa wakiweza kusimama kidete na kubangua mada na Kifimbo. Edward Sokoine, Cleopa Msuya na John Malecela.
Wengine sijui kama walikuwa na ubavu kama Jasusi alivyoeleza kutoa hoja za msingi kwa Mwalimu.
Ukiangalia kwa kina wale waliokimbilia kuua Azimio la Arusha na kulikumbatia Azimio la Zanzibar na kuchangua ni wapi na kina nani walifanya kazi chini ya Mwalimu, utagundua kuwa katika CCM kwa ukubwa walikuwa ni wanafiki na ni wachache sana walikuwa wakweli na kuweza kum-face Mwalimu kwa jambo lolote.
Haya ni maoni yangu kwa mtazamo wangu na natumaini ukiongeza watu kama Kaduma, Msekwa, Sefu Hamad, Salim, Warioba na hata Kolimba, hawa wanaweza kuwa walikuwa na uwezo wa kuongea na Mwalimu bila shida.
Sio kweli.
Kulikuwa kuna sababu kwa nini J.K. Nyerere alitaka tuimbe "Zidumu fikra za Mwenyekiti..." Maana yake fikra zingine hazikaribishwi.
Hadithi za kina Mzee Bomani ni historia potofu ambazo anaweza kuhadithia wasioelewa kilichojiri tu. Ukimuuliza Mzee Bomani maoni yake kuhusu Nyerere ni kumpelekea ngedere kesi ya nyani. Hawa wote ndio watendaji, "ndio-mzee," chinja-chinja wa kisiasa na kimatendo katika mkoba wa vifaa vya J.K. Nyerere.
Na, hata kusema J.K. Nyerere haambiliki ni kupendezesha lugha tu. J.K. Nyerere alikuwa nduli wa mawazo, kama sio nduli. Alitumia dola kushughulikia waliotofautiana nae (4). Aliyethubutu kubisha aidha alifungiwa kijijini ( Balozi Kassanga Tumbo (1) au jela (Chief Justice Wolfango Dourado ( 3 ), Abdallah Said Fundikira, Mwinyijuma Othuman Upindo, na James Mapalala (2), kufukuzishwa nchini (Waziri Kambona), kufukuzwa kazi (Rais Jumbe) na orodha inaendelea na kuendelea na kuendelea....(Kassim Hanga, Makamu wa Rais wa Zanzibar, na walinzi wake; Waziri Abdulrahman Mohamed Babu (5), na Wabunge Joseph Kasela Bantu na Mbunge Eli Anangisye, aliyekamatwa na kufungwa bila mashitaka baada ya kuchangia mjadala wa kikao cha Bajeti Bungeni, 1968 ( 6).
Kusema J.K. Nyerere alikuwa ana hoja kali sana kiasi kwamba hakukuwa na wengi wanaoweza kujadiliana nae ni kituko kwa sababu inamaanisha watu wote walikuwa watupu ila Nyerere na wachache fulani. Huku ni kupumbazika kulikotokana na kuleweshwa propaganda. Toka mdogo unaimbishwa nyimbo:
"Kambona, kaolewa!
Wapi? Huko Ulaya
Kambona, kaolewa!
Wapi? Huko Ulaya
Na nani ? Waingereza"
Ni lazima upumbazike. Hata mimi utotoni nilipumbazika. Kuja ukubwani nakuja kuambiwa eti Kambona alilazimika kuingia mitini kwa sababu alitofautiana mawazo ya mfumo wa kiuchumi. Hebu angalia hilo ndugu yangu. Sio nduli wa mawazo huyo J.K. Nyerere? Binadamu kweli unamfunga Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar kwa sababu ametoa hotuba kama mgeni mwalikwa kwenye mkutano wa Tanganyika Law Society kujadili kuboresha na kubadili Katiba! (3) Huyu Muasisi Marehemu J.K. Nyerere utasema kweli sio nduli wa mawazo? Eti, "ilibidi ujenge hoja barabara." Ukipumbazwa unaweza kuamini ya ajabu!
Rev. Kishoka, kama nimetoka nje ya mada ni katika kurekebisha historia inayopotoshwa hapa. Nina marafiki mababa zao wameuawa baada ya kuugulia kwenye vyumba vya giza Oysterbay Polisi baada ya kuswekwa miaka bila mashitaka. Umenikamata nishitaki, usiniweke niugue kisukari na magonjwa ya moyo kwenye chumba cha giza polisi, nikitoka nakaa kidogo nakufa!
( 1 ) The Standard (Tanganyika), 28 Sept. 1962.
( 2 ) Chris Maina Peter; A Comparative Study of the African Human and People's Rights Charter and the New Tanzanian Bill of Rights 31 (Studies in Human Rights No. 10, Consortium on Human Rights Development, University of Denver 1990).
( 3) Ahmed Rajab, Foul Play, Afr. Events, Nov. 1985, at 28.
(4) Chris Maina Peter; Incarcerating the Innocent: Preventive Detention in Tanzania; 1997 The Johns Hopkins University Press, Human Rights Quarterly 19.1 (1997) 113-135
(5 ) H.G. Mwakyembe, Issa G. Shivji; The Parliament and the Electoral Process, in The State and the Working People in Tanzania; 1986 Colin Leys, Tanganyika: The Realities of Independence, in Socialism in Tanzania 187 (East African Publishing House Political Studies 14, Lionel Cliffe & John S. Saul eds., 1972).
(6) Ludovick S Mwijage, The dark side of Nyerere's Legacy; Raymond F. Hopkins, The role of an MP, Swarthmore College
Suala la mapungufu ya Nyerere sikutaka kulifanya liwe ndio msingi mkuu wa mjadala huu.
Mjadala huu ulikuwa ni kujua ni wapi Nyerere alipata mawazo na mwamko wa kutuletea Ujamaa na hata Azimio la Arusha.
Najua kuna thread nyingine ambayo ilishawahi kuanzishwa kuhusu mapungufu, basi tuende kule kulalamikia mapungufu yake.
Suala la mapungufu ya Nyerere sikutaka kulifanya liwe ndio msingi mkuu wa mjadala huu.
Mjadala huu ulikuwa ni kujua ni wapi Nyerere alipata mawazo na mwamko wa kutuletea Ujamaa na hata Azimio la Arusha.
Najua kuna thread nyingine ambayo ilishawahi kuanzishwa kuhusu mapungufu, basi tuende kule kulalamikia mapungufu yake.
Mapungufu ya Nyerere sio mahala pake hapa; na mapambo ya Nyerere yasiyohusiana na Azimio la Arusha na vyanzo vya fikra zake? Hayo ni sawa, sio?
Tena mapambo ya kupotosha, ya uongo, hayo hayakataliwi? Nimeona wasifu wa uongo umejipenyeza nikapinga mapambio hayo, na nikijua ni mada nyingine, nikaeleza kwa nini nimeandika niliyoandika.
Sasa tukikataa yasiyohusika hapa tukatae yote, mapambio ya uongo na mapungufu ya Nyerere. Yote sio mahala paka.
Haya nawaacha na majadiliano yenu, al muradi yasisemwe ya uongo yasiyohusika, maana hatutaruhusu vizazi vya kesho kutwa vidhanie woooote tulikuwa bado tumepumbazika (hoodwinked ) na bunk za Nyerere, mpaka mwaka 2008.
(Kwanza nilichokiongelea hata hivyo kiko on point, kwamba Nyerere hakutaka kutofautiana na mtu. Kimewashtua kwamba nimeongelea jinsi alivyosweka watu ndani waliojaribu kutofautiana nae ? Come on guys!)
Kuhani,
Kosa lako ni kujiona kuwa ni wewe pekee ambaye unajua watu walioathirika na utawala wa Mwalimu Nyerere. Na hii si mara ya kwanza kulifanya hili!
Je unajua ni mangapi ambayo familia yangu iliyapata au kuyapoteza kutokana na huyo huyo Nyerere? If you would have known ungekaa kimya, ila ni jambo la binafsi na sitalileta hapa!
Kuna wengi ambao walipoteza mali, marafiki hata watu kuwekwa ndani kama ulivyotuletea listi, lakini katika mada hii, hakuna hata mmoja wao aliyesema kuwa aaah Nyerere ni hive au vile isipokuwa wewe.
Imekuwa ni kawaida yako kuyasema haya, na hilo naliheshimu, lakini kama nilivyosema, mjadala haukuwa unachunguza ni nini Mwalimu alikifany aau kukosea, ni kujiulilza, chimbuko la Mwalimu Nyerere kuwa mjamaa na kutuletea siasa za Ujamaa, Kujitegemea na Azimio la Arusha.
Kwa nini usianzishe basi thread nyingine ya facts na data zako kuhusu waliofungwa, kupoteza mali au kunyanyaswa na Nyerere na tuje huko kufocus machungu yetu kuhusu Nyerere?
Mchungaji!... hii inaitwa kumtolea mtu uvivu; kuna watu wanadhania kuwa ni wao peke yao wanaijua historia ya nchi yetu na wimbo wao kila wakati umekuwa ule ule kana kwamba sisi wengine tumezaliwa na kukulia Ulaya! Hapo umemkoma nyani giledi.
Kuhani,Mapungufu ya Nyerere sio mahala pake hapa; na mapambo ya Nyerere yasiyohusiana na Azimio la Arusha na vyanzo vya fikra zake? Hayo ni sawa, sio?
Tena mapambo ya kupotosha, ya uongo, hayo hayakataliwi? Nimeona wasifu wa uongo umejipenyeza nikapinga mapambio hayo, na nikijua ni mada nyingine, nikaeleza kwa nini nimeandika niliyoandika.
Sasa tukikataa yasiyohusika hapa tukatae yote, mapambio ya uongo na mapungufu ya Nyerere. Yote sio mahala paka.
Haya nawaacha na majadiliano yenu, al muradi yasisemwe ya uongo yasiyohusika, maana hatutaruhusu vizazi vya kesho kutwa vidhanie woooote tulikuwa bado tumepumbazika (hoodwinked ) na bunk za Nyerere, mpaka mwaka 2008.
(Kwanza nilichokiongelea hata hivyo kiko on point, kwamba Nyerere hakutaka kutofautiana na mtu. Kimewashtua kwamba nimeongelea jinsi alivyosweka watu ndani waliojaribu kutofautiana nae ? Come on guys!)