Who is Hussein Mohammed Bashe?

tusimshutumu kwa usomali kuwa alitakiwa aape akiwa na miaka 18 jee baraka Obama alipofika miaka 18 aliapa? sababu baba yake ni mjaluo wa Kenya. wenzetu wa Marekani wamemchagua Mjaluo toka Africa bara lingine kabisa sisi tunahoji usomali?


Baelezee Kamanda bashe, bora umejitokeza! Ila naomba unisaidie kidogo, sheria za Marekani zinasemaje kuhusu Uraia? Manake unauuliza kama Obama aliapa alipofikisha miaka 18? Do you mean we share the same law on citizenship question??? Nafikiri hata wanaJF wengine wangependa kufahamu, ama sivyo mzee wa Habari Corporation, a.k.a division of Kagoda Group Inc LLC.
 
Mwanamalunde kimya kabisa...kama ulikuwa unapima hiyo ndiyo inaitwa kumkoma nyani giladi...hahaha..bwah bwahah..kwikwikwii..tehetehteh..halafu uende ukamwambie na RA aje hapa kwa jina la Sensemamalunde..
 
Huu ni mwanzo wa kupata umaarufu, Selelii has to step down and leave young blood kufanya vitu vyake.
Young blood hata kama ina kirusi cha ufisadi. Tumia akili Urasa ach akili za kushikiwa. Na hii thread kaanzisha Bashe mwenyewe au mpambe wake ili kujitangaza. Huko Nzega alipopita hakukuta jambo lingine la msingi kuliko politics?
 


Wengine huwa wana leta majina ya watu ili kuwa tangaza kiaina !!
 

Ndg uzuri wa JF ni huu watu huonyesha madhaifu yao mapema kwanza umekiri kuwa SIASA ZA TABORA UNAZIJUA KIASI,means uko shallow uelewa wako nimdogo kwa hili,nimefanya kazi kutaka kujua kuhusu huyu kijana ambae wewe umemuita Mpenda SIFA na huwa na mtu ili kufikia malengo yake,hapa umeonyesha uwezo wa BASHE kuwa anafahamu OBJECTIVE ZAKE NI ZIPI NA NAMNA GANI ANAWEZA KUZIFIKIA,kwahili ni sifa ya kiongozi anaefaaa haishangazi kuwa kwa sasa amembana selelii.

Ukiangalia mtoa hoja hajasema alimbana selelii 2005,bali anaongelea 2009,na ukiangalia takwimu ambazo mimi nimezipata kutoka CCM mkoa wa Tabora leo saa mbili na nusu asubuhi ni kwamba, 2005 alikuwa na kura 109,2007 huyu kijana aligombea nafasi y ujumbe wa mkutano mkuu wa CCM ambapo alipata kura 1784,pia kijana huyu aligombea nafasi ya Ujumbe wa halamshauri kuu ya CCM mkoa wa Tabora akapata kura 486 ktk mkutano mkuu wa mkoa kati ya kura 623.

Na ili kuweka kumbukumbu sawa sawa itakumbukwa kuwa kijana huyu ktk politics za mkoa wa Tabora 2007 alimuunga mkono Mwenyekiti wa CCM aliekuwa anaitwa Mzee NKUMBA wakati RA,SELELII,SITA,AZIZA,MAMA MCHEMBA,na wengine wakimuunga mkono Mwenyekiti wa sasa anaeitwa WAKASUVI alisimama kidete akabaki mwenyewe na matokeo yake MZEE NKUMBA ALISHINDWA KWA KURA 20.Bashe huyu kutokana na yaliyotokea TABORA WAKATI HUO UHUSIANO WA RA,SITA,SELELII,NSEKELA ukiwa bado imara waliona huyu kijana anataka kuwavuruga,na itakumbukwa kuwa katika uchaguzi wa NEC ambao SITA alikuwa ndie mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi JINA L BASHE LILIPOTEA NA KUTOTANGAZWA NA BAADA YA UKUMBI KUPIGA KELELE NA KUHOJI SITA AKASEMA NIMESAHAU JINA LA HUSSEIN BASHE NA AKATOA IDADI YA KURA AMBAZO ZILISABABISHA KELELE NA WATU KUJIULIZA KULIKONI JINA MOJA LIWELIMEPOETEA? na hii ni baada ya kijana huyu kusimama kidete katika uchaguzi wa wilaya huku akipimana ubavu na SELELII ALIPOWEKA MKE WAKE MKUBWA ANAEITWA MAMA IGOGO KUGOMBEA UENYEKITI WA WILAYA,HUKU BASHE AKIMUUNGA MKONO MZEE AMBAE ANAITWA MWALIMU SHIJA ALIEKUWA ANATUHUMIWA NA KINA SELELII KUWA NI MTU WA MALECELA HAKUWA MTANDAO 2005,BASHE ALIMSIMAMIA MZEE HUYU MATOKEO YAKE AKASHINDA BAADA YA UCHAGUZI KUVURUGIKA MARA MBILI.

Nilichfurahia hapa ni kuwa umekiri huna taarifa za kutosha kuhusiana na siasa za mkoa wa Tabora,pia nikufumbue macho 2008,MH SPIKA aliweka mgombea wake kwa ajili ya kiti cha UVCCM mkoa ambae ni katibu wa mbunge urambo mashariki anaitwa PAULO shija,Bashe nae kwa kuwa alikuwa anajiandaa kugombea UENYEKITI UVCCM alihakikisha anaweka mtu wake katika uchaguzi huo amabao PAULO SHIJA ALIKUWA ANASIMAMIWA NA SITA NA SELELII,wakati KAMOGA ALIKUWA ANASIMAMIWA NA BASHE ,mgombea ambae bashe alikuwa namuunga mkono alishinda na kumuangusha msaidizi wa spika ambae selelii alizunguka mkoa mzima kumpigia kampeni.

Mtoa mada hakutaka kujua abt 2005 or 2000,lakini nikukumbushe seleii 1995 alizidiwa kura na bwana aneitwa KATUGA jina lake likakatwa na NEC akarudishwa selelii na kufanya huyu bwana kujiunga na CUF,pia 2000 alishindwa na ABDALAH NASSOR,nae jina likakatwa na NEC akarudishwa selelii,na ukumbuke kuwa mara zote hizi amerudishwa kwa msaada wa RA pia 2005,alishinda baada ya RA kuhamia Nzega kumsaidia selelii nA KURA kupigwa usiku wa manane,na matokeo kutangazwa hata hivo JUMLA YA KURA WALIZOPATA WAGOMBEA ZIKAZIDI IDADI YA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CCM WILAYA JAMBO LILILOLETA VURUGU LAKINI BASHE NI MGOMBEA PEKEE ALIEKUBALI MATOKEO NA HAPO SAFARI YA KUJIJENGA KISIASA IKAANZA.

KAMANDA MAO SE TUNG ALIWAHIKUSEMA NO DATA NO RIGHT TO SPEAK

NAOMBA KUWASILISHA.
 

SAWA kANDA 2: tunajua kwamba kosa si kosa bali kuendelea kukumbatia kosa ni kosa kubwa. Selelii kajua ukweli kajitoa huko, je waliobaki unawachukuliaje? Hussein Bashe umeshamsikia akitoa kauli kuhusu ufisadi au akiongea lolote kuhusu waliohusika na epa au richmond? Bashe atoe kauli tujue yeye ni clean.
 
Kwa atakayependa kujua hali halisi ya siasa za Nzega!

Mwaka 2000 Selelii alishindwa kura za Maoni na Abdallah Natco hivyo seleli akawa wa pili, 2005 Selelii alipata kura 365, Abdalla 149, Bashe 109, Henry Mapalala 52, Ndg Lile 36 na Hamis Kigwangala 25 kwa maana hiyo basi mtu aliyekuwa wapili (Bashe) 2005 kwa kampeni za wiki mbili tu na amejipanga vizuri baada ya hapo kwa kuwa karibu na wapiga kura wake ni wazi kuwa uwezekano wa seleli kushindwa ni mkubwa sana.

Kingine ambacho ni kibaya sana kwa Mh Selelii kwa siasa za Nzega amegombana na kundi kubwa la wapiga debe wake wa 2005 ambao wengi ni wapiga kura kwa mabadiliko yaliyofanywa na CCM kwa chaguzi zijazo, amejitahidi kupandikiza udini amekwama, amepandikiza ukabila amekwama, amepandikiza ueneo au uzawa kama alivyouita bila mafanikio na sasa anaanza kuwapigia magoti wale anaojua kuwa watamsaidia hata hivyo amekwama so kwa Selelii mbuzi yake kamba!
 
Rais BARAKA OBAMA mjaluo toka Kenya aliapa akiwa na miaka 18?

Sheria za kila nchi zinatofautiana. USA ukizaliwa hata kwenye anga lao tu unakuwa raia automaticaly, hata kama utaamua pia kuwa na uraia wa nchi ya wazazi wako.

TZ ni tofauti. Kwetu ni lazima uukane uraia asilia wa wazazi wako ili uruhusiwe kuwa raia wa TZ, kitu ambacho watu wengi hawafanyi. Kwa hiyo kama Bashe hakufanya hivyo basi yeye sio mTZ mpaka atakapoomba uraia na hivyo yuko nchini kinyume cha sheria, na hawezi kugombea wadhifa wowote.

Hii ni moja ya sababu zilizomfanya Kinana aachie ubunge wa Arusha maana alishaanza kuchunguzwa na wapinzani wake.
 
No! matokeo halisi ya Nzega 2005 ni haya , Seleli 365, Abdala 149, Bashe 109, Mapalala 52, Ndugulile 36 na Kigwangala 25. haya ndio matokeo halisi yalivyokuwa si kama yalivyoripotiwa na mchangiaji hapo juu
 

Hard Hitter nimeona nijaribu kukushauri kuwa huyu bwana kama unataka kupata taarifa sahihi juu ya Idara ya usambazaji (circulation) na perfomance yake nivizuri ukapata taarifa ya Steadman ya media report ya 2007,2008,na 2009,then utakuwa katika nafasi ya kuongelea juu hili.

kuhusu kuporomoka kwa mauzo ya magazeti ya mtanzania unatakiwa uwe specific hata hiyo post uloitumia kama fact yako ilikuwa nattarifa ambazo si za kweli historia ya bashe katika Media iindustry inaanza 2006 akiwa Sales and Marketing manager wa Mwananchi na the guy he did a wonderful job hapo,mimi nimefanya nae kazi yeye akiwa manager idara niliyotaja mwanachi na mimi nikiwa editorial na sasa yeye anafanya New Habari na Mimi Nipo Nipashe kwahiyo ninapoongelea swala hili nafahamu.

Tukiwa wanahabari wapo watakaokubaliana na mimi kuwa BASHE ni mmoja wa Best managers wa maswala ya CIRCULATION NA MARKETING ya news paper, matatizo ya HABARI sote tunafahamu si matatizo ya usambazaji ingelikuwa ni TATIZO LA USAMBAZAJI leo gazeti la michezo la kila siku linalongoza katika soko tunafahamu ni BINGWA na katika magazeti ya wiki ya michezo gazeti la DIMBA ni moja kati ya magazeti mawili au matatu yanayoongoza kwa mauzo, mbali na hilo Gazeti la Rai ni gazeti ambalo lilionekana kuporomoka leo ni gazeti ambalo baada ya Mwanahalisi ni lapili katika mauzo ingawa PROFESSINALLY RAI na mwanahalisi yanaangalia wasomaji aina Tofauti RAIA mwema ndie msindani wa RAI ambae kimauzo bado hajalifikia RAI.

Nivizuri post zetu ziwe za uhakika zaidi
 
Tunaomba ze dataz na facts.
 

Acha hizo Kanda2. Msimamo wako unafahamika kwa wanaJF. Ile janja ya Bashe kuchuana na Beno Malisa kuwania ukuu wa UVCCM ilikuwa ni plan ya kambi moja tu ya wanamtandao. Bashe akiwa upande wa Rostam Aziz na Malisa ambaye ni rafiki mkubwa wa Ridhiwani Kikwete akiwa upande wa Kikwete, huku ikieleweka kuwa RA na JK lao ni moja.

Hii ilikuwa ni janja yao ya kuhakikisha kuwa liwalo lolote lile mshindi anakuwa ni mtu wao, kwa kuwa wagombea wote wawili ni watu wao.
 

Du! Wewe ndiye Bashe au?????
 
...lakini nikukumbushe seleii 1995 alizidiwa kura na bwana aneitwa KATUGA jina lake likakatwa na NEC..

Daylight Lies. Hamis Katuga hakugombea ubunge mwaka 1995 kwani wakati huo alikuwa ni diwani wa kata ya Nzega Mjini hadi 2000 alipoamua kujitosa kwenye ubunge. Kusema siasa za Tabora nazijua kiasi maana yangu ni kuwa sitaki kujikweza kihivyo! Tatizo la Bashe na wafuasi wake ni day dreamers. Ndio maana wanatoa matokeo ya 2005 kuonyesha kipenzi chao alikuwa wa pili na alizidiwa kura 36 then ukiwaambia ukweli wanakiri na kuleta matokeo mapya ambayo bado yanamuonyesha kuwa wa tatu lakini bado wanang'ang'ania alikuwa wa pili sijui wanatoa wapi takwimu hizi.

Wana JF. Naombeni niwaulize swali; hivi unapogombea na mtu "anakubana" hadi unamshinda anakuwa wa tatu. Then kwenye kampeni anakuwa lulu badala ya yule wa pili. Nani anaweza kukusaidia ipasavyo kuzindua kampeni wa pili au wa tatu?

Sitaki kumsaidia Seleli hapa yeye kama atagombea tena atapimwa na wapiga kura wake kwa aliyoyafanya toka '95. Kama hawataridhika waweke damu mpya. Lakini wana JF tusome posts za hawa watetezi wa Bashe btn lines mtagundua illogical ideas nyingi tu!

Naomba kutoa hoja!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…