Who Is Mange Kimambi? Jua ukweli wenye facts sio grapevine kumhusu huyu mtu, biography and facts!

Status
Not open for further replies.
Aruhusu ili upate cha Kuandika kuwa hata JPM anamuogopa Mange! Big no
 
kwenye mitandao mange anaonekana shujaa, but kwenye uhalisia sio hivyo, ni kama ilivyo upinzani wafuasi wake ni wachache ila wako busy mitandaoni lakini ccm ina wafuasi wengi na wengi wao hawako mitandaoni.
Ni chizi tu atakayekuamini, ccm inawafuasi wengi wkt inaogopa katiba mpya, inaogopa uchaguzi huru wako bize kuhakikisha uchaguzi unasimamiwa na makada wao. Siku iyyo tukipata uhuru wa kweli utaiona ccm kuwa nyepesi km ubua
\q\~\
 
Kwani huwezi kuishi Moshi baadae ukahamia Mbezi.
 
Mbona wewe unakubali kuongozwa na mtu aliyezaa na shemeji take pamoja na wasaidizi wake?
 
Kwani huwezi kuishi Moshi baadae ukahamia Mbezi.
Ila kwa kipindi alichoishi Moshi na brand aliyoitengeneza kule, sikutegemea kama pasingekuwa kwenye wasifu ulioutoa. Ni kama umzungumzie JK Nyerere halafu usitaje Butiama.
 
Easyfit uzi wako ni mzuri na binafsi nimepata fursa ya kuelewa historia ya huyu binti Mange. Aidha, ushauri ulioutoa hasa kuhusu kuziba ombwe linalotumiwa na Mange. Nasita kukubaliana nawe kuhusu kuruhsu maandamano. Mambo yanayodaiwa na wahamasishaji, yapo yanayoweza kutekelezwa kwa muda mfupi na mengine yanahitaji muda mrefu zaidi. Miye ningeshauri kuwepo na mjadala wa wazi wa mahitaji ya wananchi kama uhuru wa vyombo vya habari n.k. Ni kweli maandamano hasa yenye vurugu yanaweza kuathiri uchumi kwa njia nyingi, mambo hayo yasemwe hadharani na kuwelimisha wananchi.

Viongozi wetu wajitokeza hadharani na kwa lugha za kiungwana badala ya vitisho kutoa maelezo juu ya madai ya wananchi. Mambo ya muda mfupi yafanyiwe kazi na yale yanayohitaji muda mrefu kama katiba, maelezo ya kiungwana na ya kuridhisha yatolewe.

Imani yangu ni kwamba maandamano hayatafanyika; siyo kwa sababu ya vitisho, lkn kwa sababu ya nature na uungwana wa watanzania. Hata hivyo, hata kama hayatafanyika hiyo trh 26/4 hapa tulipofikia tunapaswa kukaa kama taifa na kujiuliza wapi tumekosea na hatua za kurekebisha kasoro hizo zichukuliwe haraka kama tunataka kuendelea kuwa taifa la amani.

Tulipofika leo ni dalili tosha kuwa tuendapo tunaweza kuipoteza amani yetu ikiwa malalamiko yanayotolewa yataendelea kupuuzwa.

Viongozi wastaafu wamsaidie Rais, wanalipwa kwa kazi yao na hata baada ya kazi yao. Uzoefu wao wanaweza kuutumia na kuisaidia nchi badala ya kukaa kimya kama vile hawapo.

Binafsi nawashauri watanzania wenzangu, kuwa hatuna haja ya kuandamana. Tumeijenga nchi kwa muda mrefu, hatuna sababu za kuibomoa kwa siku moja kwa mambo ambazo kimsingi yanatekelezeka kama tutakubaliana kufanya hivyo kama nchi. Siyaandiki haya kwa uoga, lakini kwa kutambua na kuthamini tunu hii ya amani tulionayo ambayo inapaswa kuthaminiwa na kulindwa na kila mtanzania.
 
Katika kosa kubwa sana ambalo serikali ya JPM imefanya ni kumjibu huyu Dada Mange Kimambi juu ya kuhamasisha maandamano ya nchi nzima kupitia mitandao kijamii. Sasa habari zimeenea kila kona. Wengi hawakuwa na taarifa juu ya maandamano ya tarehe 26 /4. Lakini baada ya Magufuli kuyapinga kwa vitisho, Wakuu wa Jeshi la polisi pamoja na mkuu wa mkoa Paul Makonda, sasa kila mmoja kajua.

Nikiwa mtaani, nikapita kwa wazee wenzangu kupata kahawa, kila mmoja anazungumzia habari za maandamano. Jina la Mange Kimambi halikuachwa kutajwa kama kiongozi na mhamasishaji wa maandamano hayo.

Mzee mmoja mwenye heshima zake sana pale mitaa, mstafu wa Jeshi la wananchi. Akauliza " Mange Kimambi ni nani? Anafananaje ? Nataka nimuone tu" haraka haraka nikafungua simu nikaonyesha picha yake, wazee wote walikuja kuchungulia mwanadada Mange Kimambi.

"Kumbe ndo huyu anaitesa serikali hii? Huyu ndio anamtisha Magufuli namna hii? Huyu ndie anaetisha Jeshi la polisi? Kapata wapi hujasiri huu" kweli huyu Dada anamnyosha Magufuli.

Sasa maandamano kila mtanzania anajua, ni bora serikali ingekaa kimya, kuliko kusimama majukwani na kuanza kutoa vitisho vya ajabu zidi ya waandamanaji. Hata yasipofanyika, tayari Mange Kimambi kaishafanikiwa mpaka hapa.
 
mange kawapeleka kibra na wao wameelekea. sasa wamebaki kuweweseka.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…