Who is Salim Ahmed Salim?

Field Marshall Es,
Mkuu watoto wengi wa mitaa ya huko mjini wamesomea Bunge, usitake kupafanya kama palikuwa sehemu maalum labda unazungumzia kabla ya Azimio.

Wakati wa mwalimu shule ilikuwa chaguo la mzazi na mara nyingi watu walitazama usafiri zaidi ya nafasi ya mzazi...

Ebu jikumbushe kwanza na picha hii:- Bunge Primary School - Wikimapia
 
usitake kupafanya kama palikuwa sehemu maalum labda unazungumzia kabla ya Azimio.

Mkuu nilikuwa ninamjibu aliyesema kuwa moja ya vigezo vya kufaa kwa Salim kuwa rais, ni pamoja na watoto wake kusoma bongo na sio nje, ndio nikamjibu kuwa watoto wa Salim kama Mkapa wamesoma Bunge na US, na alipoondoka US, Salim aliwaacha watoto wake under supervision ya mdogo wa mkewe aliyeolewa na Mnywamwezi mmoja anayeitwa Mr. Jackson ambaye ni Councilman wa New York City, mpaka leo, sasa angekuwa mzalendo sana basi angerudi nao, lakini sidhani kuwa ni sababu muhimu on urais.

Halafu nikaongeza kuwa shule ya Bunge Primary, kama Olympio, enzi hizo waliposoma watoto wa Mkapa na Salim, hazikuwa na access kwa watoto wa masikini, hiyo access unayoisema wewe labda ilitokea baada ya hao watoto kuondoka, kwa sababu watoto wa Mkapa walikuwa siku zote close sana na kijana mmoja ambaye baba yake alikuwa mwanajeshi, mkulu wangu Jimmy (Jimmy Sharp) ninaamini kuwa unamfahamu, juhudi zake zote kutaka asome pale hazikuwezekana kwa sababu baba yake hakuwa an-fit level ya wazazi wa watoto wa pale mkuu,

sasa kweli Bob unaweza kusema mimi "nisitake kupafanya" Bunge Primary School kuwa palikuwa ni special school mkuu na mimi nimekulia pale pale Ocean Road? Mkuu nimekulia nyumba ya tatu toka Ikulu, inaanza Ikulu, halafu inayofuatia zamani alikuwa anaishi Kawawa, and then niliyokulia, na inayofuatia ambayo ni ya mwisho kabla ya kwenda Hospitali ya Ocean Road, alikuwa akiishi Mwakawago, mstari wa mbele walikuwa Amir Jamal, Mark Bomani, Chiduo, Mzee Kitenge na Apiyo, sasa mkuu unasema hiyo shule ilikuwa na access na watoto wa masikini? Hivi unajua hii shule hata lugha yake ilikuwa ni English tu, hakukuwa na Kiswahili? Kabla ya Azimio La Arusha hata shule ya msingi nilikuwa sijaanza sasa ningejuaje hayo mkuu?

I mean sikatai juhudi zako za kutaka kumfagilia Salim, ni haki yako mkuu, lakini ukweli ni kwamba political facts na record ziko very clear kuwa Salim, ameshakataliwa mara tatu ndani ya CCM, ni kweli ana CV nzito sana kuhusiana na kazi zake za nje, lakini hata UN alishindwa walimkataa, tena viongozi wengi wa CCM ukiwauliza huwa wanasema kuwa ni sababu zile zile zilizomfanya akataliwe UN ndio na wao wanazitumia kumkataa,

Bob sina nia yoyote ya kumchafua Salim bila sababu, wakati wa uchaguzi wa rais CCM kule Dodoma, Salim alikuwa na kura 3 tu za wajumbe 2000 wa NEC, sasa huyu atakuwaje rais wa bongo mkuu? Unajua ninajaribu tu kujiepusha na huu mjadala kwa sababu ninajua mengi sana ya Salim, lakini sina mpango wa kuyatoa kwa sababu ninaheshimu sana kitendo chake plae mwishoni wa uchaguzi alipoamua kujiepusha kabisa na siasa za bongo, otherwise ninaomba mkuu unielewe kuwa sipindishi anything kwenye sababu zangu za kumkataa, in fact ninaepuka kuyatoa zaidi mapungufu!

Ahsante Mkuu!
 
Sikusema kuwa atumie nafasi yake kuwanufaisha ndugu zake lakini ukweli ni kuwa kama kashindwa kumhudumia ndugu yake what makes you think ana uwezo wa kuwahudumia waTZ?

narudia sisemi kuwa atumie rushwa kuwasaidia ndugu zake

naomba nieleweke
 
ukweli ni kuwa kama kashindwa kumhudumia ndugu yake what makes you think ana uwezo wa kuwahudumia waTZ?

Mkuu GT,

Huna sababu ya kuomba radhi hii yako ni very strong na ni valid argument, na ndio hasa aliyoyafanya kule OAU kukataa kuajiri wabongo kabisaa, huyu mambo yake ni ya nje nje tu sasa sisi wabongo atatusaidiaje?
 
Fiueld Marshall Es,
Mkuu watoto wote wa mitaa ya Ohio wamesoma Bunge kama unakumbuka enzi zile tukivizia vimwana wa mitaa hiyo..baba zao walifanya kazi serikalini wengine TRC kwa hiyo bado sioni chachu.

Kulikuwepo na shule kibao za Private na hizi walisoma watoto wa mtu yeyote mwenye uwezo wa kufanya hivyo tena basi navyokumbuka wengi walikuwa wale walioshindwa mitihani ya darasa la nne ama saba na kurudia darasa ilikuwa sio optiuon hivyo walipelekwa Preivate school hata kama walikuwa kabuntas.

Ndio maana shule za Private Bongo enzi za mwlimu zilikuwa chini sana ktk matokeo kuliko shule za serikali. Bunge haikuwa deal isipokuwa sisi tunataka kuifanya hivyo...
 


Mkuu Mwanahabari,

Consultancy kila mtu alizifanya lakini ni wazi kuwa hizi sio ajira za kumpa mtu kipato cha kila mwezi, na ndio maana hufanyika nje ya muda wa kazi.

Mwandosya ana mambo mengi ya kujibu, tokea 1985 alipoingia serikalini hadi alipokuwa PS wa wizara ya viwanda na biashara 1992-93 na baadaye uwaziri.

Lakini tokea alipoupata u-PS & uwaziri , Mwandosya alibadilika na kuwa tajiri overnight, kama ilivyo kawaida kwa baadhi ya mawaziri wetu mafisadi na maPS wetu. Hapa ndio panapoleta maswali hasa ukitilia maanani kuwa ndio kipindi hiki pia alichoweza kupeleka watoto ughaibuni. Ukiongezea na ununuzi wa ndege mbovu ya raisi, Mwandosya anabaki kuwa wa maswali mengi hadi atakapoeleta majibu yake.

"What is the cost of the pride of the nation? The number does not mean anything as long as we buy the plane, maintain it and look after the welfare of our people"[/I].

Mwandosya on the purchase of the controversial Presidential Jet.
 

Mkuu Gaijin,

SAS hajashiriki kabisa mauaji ya Karume. Hakuna ushahidi wowote hata wa kimazingira wa kudhihirisha hilo, ila hizi zimekuwa shutuma zilizotumiwa na wale wasiotaka kumuona muungwana kushika madaraka. SAS ana sifa za kuwa raisi tokea kabla hata ya Mwinyi alipoteuliwa. Lakini kilichomkwamisha ni uwezo wake makubwa ambao umewaogopesha wale waliomtangulia, including Nyerere, kuwa atawa-overshadow.

Nyerere alitaka mrithi wake awe mtu wa uwezo wa chini sana kuliko yeye ili hata kama akifanya mabadiliko kama aliyofanya Mwinyi ya kufungua milango ya biashara n.k., bado asiwe maarufu kuliko yeye.

Just imagine kama mabadiliko yale yangefanywa na SAS, halafu ongezea na uwezo wake mkubwa katika mambo ya kimataifa, leo hii nani angemuona Mwalimu kuwa alikuwa wa maana kuliko waliomfuatia?

Uwezo mkubwa na usafi alio nao SAS hivi sasa ndio kikwazo chake katika kuteuliwa kuiongoza nchi. Wapo wengi wanaoogopa kupoteza nafasi walizopewa kwa upendeleo maana jamaa haangalii sura, anajali zaidi uwezo wa mtu.

SAS ana upeo wa hali ya juu na ndio maana baada ya wengi kushindwa kuibadili OAU kuwa AU, walimuomba asaidie na walihakikisha anaendelea kuteuliwa mpaka kazi yake ilipokamilika.

Ukweli ni kuwa tunamhitaji Salim A. Salim, hasa kama tunataka mtu wa kumuondoa Kikwete madarakani.
 


Mkuu FMES,
The point is, kwa madaraka aliyoshika tokea akiwa 22yrs, SAS angekuwa mtu wa makuu, watoto wake wasingegusa penseli za TZ kama maofisa wetu wengi balozini walivyo.
 


Mkuu FMES,

Bunge, Olimpio, Forodhani, Muhimbili, Oyesterbay n.k., hazikuwa special schools. Watoto wa viongozi wa serikali wasiokuwa na makuu walipeleka watoto wao hapo kwa vile wengi waliishi maeneo au walifanya kazi karibu na hizo shule. Wale waliokuwa nazo walipeleka watoto wao kwenye shule kama Arusha School, Nyakaoja, Kifungilo, Greek School, IST n.k. Kama hukusomea hizi shule, then ulisomea shule za kawaida tu ambayo kwa mtu aliyefanikiwa mapema kama SAS, ilikuwa jambo ambalo sio la kawaida.

Ni vema tukamchmbua SAS kulingana CV yake na tukaachana na majungu aliyopakaziwa ambayo hayana ushahidi, maana hivi sasa nafikiri SAS ndio pekee mwenye jina, usafi na uwezo wa kumuondoa Kikwete yr 2010, na kuibadili nchi.

Tuangalie CV yake na yale aliyoweza kuyafanya hapo awali, na yanawezaje kumsaidia kuwa kiongozi mzuri.
 

napingana kabisa, consultants kama Mwandosya wanalipwa ajira kubwa tu, pamoja na kuandika (na kuuza vitabu kadhaa) muda wakati hakuwepo kabisa serikalini, na watoto wake wamekuwa nje wakati hayuko kabisa serikalini na akijiendeleza na private sector huku bado akishika nafasi nyingi tu kwenye makampuni tofauti ambayo yanalipa. Kupeleka watoto nje kwa mtu kama Mwandosya kipindi ambacho hakuwa kabisa serikalini siyo kitu cha kushangaza. pamoja na kuwa chairman wa SIemens Tanzania, TPDC, Director Standard CHartered.. na mengine mengi (wakati hakuwepo serikalini 1993-2000), inasikitisha sana kuona kwamba watanzania wenye kazi halali na uwezo wanahusishwa na ufisadi.

Watoto wote wamesoma nje wakati Hakuwepo kabisa serikalini, wote walienda nje after 2 years yeye kuondoka serikalini.

Nenda Amazon ukaone bei ya vitabu alivyoandika vinauzwa kwa bei gani, kwa hiyo tu mtu yoyote anaweza kupeleka watoto shule.

Kuhusu ndege ya serikali, kwanza G550 siyo mbovu (muulize John Mkony, ceo tgfa - Pilot wa Rais atakuambia), Jk haitumii kwa sababu anazozijua mwenyewe preferres to fly first class commercial including entourage yake kubwa tu, inatumika zaidi na Dr. Shein na wengine. Hata watu binafsi wanaweza kukodi ndege za serikali. Kama argument ni bei ya ndege, G550 ilinunuliwa kwa bei halali kuzingatia specific options serikali ilizochagua zikiwemo custom designs and performance specifications suited for operating in our conditions and usage specification(thats another argument though, maana tukinunua bei rahisi mnaona yanayotokea ---> richmond) hii hapa gulstream ikiwa Cologne this Feb http://www.planepictures.net/netshow.php?id=718457

Labda kama kuna maswali ni vizuri kuuliza kuliko kuhukumu mtu amepataje utajiri au kama una data mpya tuko wengi hapa tunapenda kujua, na kusema alibadilika kuwa tajiri overnight kama kigezo ni kwamba alisomesha watoto wake nje ---> kazi lizokuwa anafanya nje ya kuwepo serikalini zinalipa vizuri tu na mtu yeyote mwenye kazi kama hizo anaweza kusomesha mtu.

Bali nakubaliana na wewe, kila mtu ana maswali ya kujibu na wengine kama Chenge, Lowassa Karamagi, Rostam wote tunaona paper trail na majina yao yanakjitokeza kila sehemu, kama kuna mtu ana data za Mwandosya kuhusika na mambo haya, wekeni humu watu wachambue.

Flashback from JF

Salma atesa na ndege ya Kikwete
Ni ile ambayo rais anaogopa kuitumia kikazi Ulaya
Aipanda kwenda na kurejea katika ziara binafsi
Aitumia kuendea sherehe za mila za Mswati III

na Mwandishi Wetu

BAADA ya Rais Jakaya Kikwete ‘kuogopa’ kutumia ndege yake iliyonunuliwa kwa mabilioni ya shilingi bila idhini ya Watanzania, sasa ndege hiyo inatumiwa na mkewe, Salma katika ziara binafsi.

Mara ya mwisho, Salma alitumia ndege hiyo kwenda kwenye sherehe za kimila nchini Swaziland, kushuhudia Mfalme Mswati III akichagua mke wa 13.

Uchunguzi wa Tanzania Daima umethibitisha kuwa Salma aliondoka Dar es Salaam Agosti 29, mwaka huu saa tisa jioni, akiwa amepanda ndege hiyo aina ya Gulfstreame Jet Engine kwenda Manzini, Swaziland.

Ndege hiyo ya rais namba 05H-ONE, iliondoka Dar es Salaam kuelekea Swaziland, alikokuwa anakwenda kuhudhuria sherehe za kimila, ambazo baadaye zimeshutumiwa na wanaharakati kwamba zinawadhalilisha wanawake.

Septemba 5, mwaka huu, ndege hiyo ilimfuata na kumrejesha Dar es Salaam.

Kwa hakika haya ni matumizi mabaya ya ndege ya rais, kwa kuwa mke wa rais, si rais, na hapaswi kuitumia kama anasafiri peke yake kwa safari binafsi.

Fursa pekee aliyonayo mke wa rais kutumia ndege hiyo, isiyoweza kunung’unikiwa hata kidogo, ni pale anaposafiri na mumewe katika safari za kikazi.

Matumizi haya ni kashfa nzito kwa serikali ya awamu ya nne, inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete, aliyesema tangu awali kwamba urais wake usingekuwa wa ubia na mtu yeyote.

Miezi miwili iliyopita, gazeti hili liliandika habari kuwa Rais Kikwete anahofu kupanda ndege hiyo katika safari zake za kikazi Ulaya, kwa madai kuwa ni gharama kubwa mno kwa nchi maskini kama Tanzania.

Badala yake, ameazimia kuitumia katika safari za Afrika, hali inayotafsiriwa pia kuwa anaona aibu kupanda ndege ya kifahari kwenda Ulaya kuomba misaada kwa serikali zinazoongozwa na viongozi wanaotumia ndege za kawaida katika safari zao za kikazi.
 

Mkuu Mwanahabari,

Ni kweli Mwandosya alikuwa amefanikiwa kwa kiasi fulani lakini hakuwa tajiri wa kutanua. Matanuzi yameonekana kuongezeka alipokuwa PS ambapo u-consultant ulikuwa haupo tena. Huko wizarani ndio alipoona utamu wa siasa na kuamua kwenda kugombea ubunge ili asiwe tu PS bali awe ndio waziri kabisa. Na kati ya alivyotuletea pamoja na utaalamu wake wa electronics ni hiyo ndege na radar. Hivi vyote alivitetea bungeni.

Nijuavyo mimi ni kuwa ile ndege ni pre-owned, maana GS 550 bei yake ni zaidi ya $50million, ni ndege ya anasa. Boeng 737-600 mpya kutoka kwenye makaratasi, Boeng wenyewe wanaweza wakakupa kwa bei sawa na ya GS 550.

Sasa kwa ukonsaltanti wa Mwandosya kwa nini hakuishauri serikali vizuri wakati national airline ilikuwa inarusha Boeng 737-200 ambazo hata uundwaji wake umesitishwa? Huyu bwana ana maswali mengi ya kutujibu.
 
Sikusema kuwa atumie nafasi yake kuwanufaisha ndugu zake lakini ukweli ni kuwa kama kashindwa kumhudumia ndugu yake what makes you think ana uwezo wa kuwahudumia waTZ?

narudia sisemi kuwa atumie rushwa kuwasaidia ndugu zake

naomba nieleweke

Mkuu,
Mbon ni wengi ambao hata watoto hawana lakini utumishi wa umma wako safi sana? Inawezekana huyo kijana naye anamatatizo yake maana ndugu wengine wote wa Salim ninaowafahamu wako wametulia na shughuli zao za kihalali.

Ubora wa uongozi wake ameshatuonyesha kwa kuongoza OAU na AU, na maraisi wa Afrika walifanya kumuomba aendelee na uongozi. Hkuna aliyeweza kujitokeza kum-chalenji.
 

Shekhe hana matatizo hata kidogo

namjua sana na hata nyumba ya kulala nilimtafutia mimi...na si peke yake katika fe- mili ya huyo SAS anayelalamika

Lakini tushaambiwa ndio hulka yake SAS hana tofauti sana na AHMED RAJAB, ndio maana AH alikuwa akimkampenia sana SAS awe prezi daa kwani wanajuana.

That said, SAS kawapa kazi kubwa kubwa ndugu zake OBASANJO wa NIGERIA ....hatusemiu awape ndugu zake lakini huo ni mfano tuu wa allegiance za SAS
 
na walionufaika ktk ndugu zake mbona huwataji na wako wengi.

sisi tulipokuwa india na waliosoma pale miaka ile ya tisiiini watakwambia kuwa kulikuwa na ndugu zake wanasoma tena kwa pesa yake
 
FMES,

..ninavyoelewa mimi wakati wa utawala wa Mwalimu shule za bongo zilikuwa bomba kuliko za Kenya.
kipindi hicho nakumbuka text books, daftari, na hata kalamu, vilikuwa vikitolewa bure na serikali.

..Mawaziri wote [Kawawa,Sokoine,Malecela,Msuya,Mtei,Ali Mwinyi,...]ninaowajua mimi walioserve wakati wa Mwalimu walisomesha watoto wao Bongo. Tena wengine walipeleka watoto wao hata boarding schools mikoani.

..Tabia ya kupeleka watoto kusoma nje ya nchi ilishamiri wakati wa utawala wa Mzee Ruksa. Salim Salim alifanya kazi chini ya Ruksa kwa miaka kama 3 tu.

Kubwajinga,

..Nyerere hakumuogopa Salim Salim hata kidogo. Baada ya Sokoine, Salim Salim ndiye alikuwa "mtoto kipenzi" wa Baba wa Taifa.

..Nyerere alitaka Salim Salim awe mrithi wake wa kiti cha Uraisi.

..Wakati anang'atuka mwaka 1985, Nyerere alipendekeza jina la Salim Salim. Walioharibu mpango huo wa Nyerere ni wajumbe toka ZNZ kama Abdallah Natepe, wakisaidiwa na wabara kama Alfred Tandau.

..Nyerere alipompendekeza Salim Salim wajumbe wakamuuliza hivi: "..Ndugu Mwenyekiti Makamu wako ana tatizo gani?" Nyerere alishindwa kujibu swali, na Ally Mwinyi, Makamu wa Mwenyekiti wa CCM, akapitishwa kugombea nafasi ya Uraisi.

..pia Salim Salim is on record akisema kwamba hata mwaka 1995 Nyerere alimfuata tena akimshawishi agombee Uraisi. Majibu ya Salim Salim yalikuwa kwamba after Mwinyi the country was not ready for another Zanzibari.

..hii habari kwamba Nyerere alimuogopa Salim Salim kutokana na uwezo wake mkubwa haina uzito hata kidogo. Au kwamba Nyerere alitaka nchi ishikwe na mtu wa hovyo-hovyo pia siyo ya kweli.
 
Ni vema tukamchmbua SAS kulingana CV yake na tukaachana na majungu aliyopakaziwa ambayo hayana ushahidi, maana hivi sasa nafikiri SAS ndio pekee mwenye jina, usafi na uwezo wa kumuondoa Kikwete yr 2010,

Salim na Kikwete, wamegombea mwaka 2005, Kikwete akamshinda Salim kwa kupata kura 1500, against kura 500 za Salim, leo unasema miaka mitano baadaye wakigombea tena, huku Kikwete akiwa rais tayari na Salim akiwa nje, Salim ndiye mwenye uwezo wa kumuondoa Kikwete madarakani?

Yaani kina Slaa, Mwakyembe, na Zitto walale macho kutondolea wananchi kero za ufisadi, na mikataba mibovu, lakini Salim aje tu na kumuondoa Kikwete na kuwa rais wetu, what a dream! Ninaamini Salim mwenyewe hana this kind of low political thinking!
 
Bunge haikuwa deal isipokuwa sisi tunataka kuifanya hivyo...

Bob ni watoto wangapi wa masikini unaowajua waliosoma pale? Nimesema kuwa hii sio ishu, lakini still ni lazima tuweke record straight kuwa Bunge Primary School haikuwa sawa na Mchikchini au Gerezani Primary,

Watoto wote wa mabalozi walikuwa wakisoma pale na International school, watoto karibu wote wa experts toka nje walikuwa wakisoma pale, naona mnazitaja shule za uzunguni hivi ni nani mtoto wa masikini aliyewahi kusoma hizo shule then?

I mean mambo ya shule za watoto, hazihusiani kabisa na uwezo wa baba zao na uongozi wa taifa letu, it just out!
 
Field Marshall Es,
hata mimi nakubaliana nawe katika hili.. Salim muda wake uimeshapita hawezi tena mitulinga ya nchi hii hasa baada ya Kikwete. Utawala unaofuata sasa hivi lazima apatikane mtu kuyafanya yale aliyoshindwa Kikwete na sio kurudi nyuma tena kama vile nchi iko shwari.

Tanzania kwa mara ya kwanza imepigwa na wimbi kubwa la Kisiasa na Kiuchumi kiasi kwamba anayetakiwa kuongoza ni mtu mwenye ubavu na nguvu kubwa ya kupambana na Mafisadi wa ndani.

Hivi sasa Salim ni mtu anayetakiwa kukaa pembeni kama kina Kennedy Marekani, kupiga debe na kuwaongoza watu kama kina Zitto na Slaa hata kama wako vyama tofauti.

Nadhani hivi sasa tumefika wakati wa kuondoa tofauti zetu na kuwa kitu kimoja against Ufisadi..Unless nitarudia tena LABDA kama Kikwete ataweza kuboresha uongozi wake ktk miaka miwili na nusu hii iliyobaki..then kazi kubwa itabaki kwa vyama vya Upinzani kumwangusha CCM ktk Ubunge kuhakikisha mabadiliko makubwa ktk katiba ya nchi yetu, lakini focus kubwa iliyopo sasa hivi ni hicho kiti cha Mugabe - Utawala wa kiafrika where winner takes All...
 
Ubora wa uongozi wake ameshatuonyesha kwa kuongoza OAU na AU, na maraisi wa Afrika walifanya kumuomba aendelee na uongozi. Hkuna aliyeweza kujitokeza kum-chalenji.

Hakuna aliyemuomba kuendelea mkuu, najua una access na baadhi ya viongozi wa juu sasa vipi ukiwauliza ni hela ngapi Mkapa alitumia kumsaidia kuendelea kubaki huko OAU, tena hela za taifa letu ambazo hazikuwa accounted mahala popote!

Mengine muwe mnauliza wakuu, unafikiri after all this ni kwa nini baadaye hata Mkapa, aliyekuwa one of the best friend wa Salim, ambaye hata siku ya kutangaza kwake kugombea walikuwa pamoja mbele ya waandishi, alimgeuka?
 
Field Marshall es,
Ok tuweke record sawa unazungumzia miaka gani watoto wa Salim walisoma Bunge...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…