Who is Salim Ahmed Salim?

Who is Salim Ahmed Salim?

kwani hadi leo hajachunguza pamoja na kuwa madarakani kwa miaka 8!!!???? Kama hajafanya uchunguzi inamaanisha anajua chanzo cha kifo cha baba yake, na kama sivyo atakuwa mjinga kwa kutokujari (taking it for granted)

Kwani kesi si ilifanyika Mahkamani, kisheria. Na hukumu zikatolewa. Na msamaha ukatolewa kwa wengi tu ambao walihukumiwa kifo na Mahkama. Mnataka uchunguzi wa nini.

Haturudi nyuma. Na tusonge mbele.
 
Rekebisha historia yako. Kassim Hanga amekufa kabla ya Karume kufa. Inakuwaje marehemu amuue aliyemzima.
Kasim Hanga inasemekana ndie alieuwawa na Karume kwa kufungwa jiwe na kurushwa baharini na mpaka leo watoto wa Hanga hawajaona mwili wa baba yao ili kuzika kwa heshima. Wengi tu waliuwaw, wapi Twala nk. Wakati Karume anauwawa na Humud, SAS wala hakuwapo nchini alikuwa ubalozini. UMMA walipewa tu kifo kile ili kuwafuta kabisa katika siasa za Zanzibar lakini ninaamini sio Babu wala SAS wala Sultan Ali waliohusika. Uchunguzi huru ufanyike na Karume mtoto ili kujua ukweli wa kifo cha baba yake.

Who was Mr X katika ile kesi? Kama alivyokuwa akimtajs Wakili Dourado?
 
Zitto said:
Hata Uhizbu wa SAS kikweli haupo kwani alikuwa ZNP muda mfupi sana kabla hawajaanzisha chama chao kipya cha UMMA chini ya Babu.

Zitto,

..ZNP walikuwa wakijulikana kama HIZBU. Lengo lao lilikuwa ni ZNZ "huru" iliyochini ya Sultani.

..ZNP au HIZBU walikuwa na matatizo ya kuwatambua weusi wa ZNZ kama raia kamili wa nchi hiyo.

Mkandara said:
Zitto,
Shukran, nachojaribu kusema hapa ni kumwonyesha tu ndugu yangu Jokakuu kuwa Salim hakuwa na nafasi yoyote ZNZ.. kila wadhifa alopata umetokana na Bara kama vile hakutoka ZNZ....
Sijui kama aliwahi kushika hata Ukatibu kata ktk kitongoji chochote ZNZ

Mkandara,

..tatizo ninaloliona mimi ni la Salim Salim kushindwa kutengeneza base yake mwenyewe ya kisiasa. inaelekea kila nafasi alikuwa anasubiri Mwalimu amteue au ampendekeze.

..wakati Salim yuko Tanzania, Ally Mwinyi na Idiris Abdul Wakil, walichaguliwa Uraisi wa ZNZ. Kwa msingi huo basi Salim Salim angeweza kujaribu bahati yake.

..Pia kuteuliwa Ubalozi isiwe kisingizio cha yeye kutoku-serve nyumbani. wako Mabalozi kibao walioomba warudishwe watumikie wananchi nyumbani. kusisitiza tu, Balozi wa kwanza wa Tanzani UN, alijiuzulu Ubalozi na kuamua kugombea Ubunge.

..kwangu mimi naona kutumikia nje muda mrefu na kutokujijengea mtaji wa kisiasa ni a major POLITICAL MISCALCULATION iliyomkosesha Salim Salim Uraisi.

..Kwa upande mwingine sidhani kama Salim Salim atatufaa kuwa Raisi wetu katika zama hizi. Sababu zangu nimezieleza ktk postings zilizopita.
 
Wakati Karume anauwawa na Humud, SAS wala hakuwapo nchini alikuwa ubalozini.

Mkulu Zitto,

Heshima mbele mkuu, hapa panahitaji nyongeza siku ya mauaji Salim alikuwa kwenye ndege anarudi bongo akitokea Lagos, mkulu mmoja bongo aliwahi kuniambia kuwa aliwasiliana kwa siri na lile shirika la ndege alimokuwemo Salim, ili kuhakikisha kuwa hashuki ndege ilipotua bongo na pia kujificha ili isijulikane kuwa alikuwemo kwenye ile ndege ambayo ilikatiza muda wake wa kukaa bongo na kuutimua mara moja, huyo mkulu kwa maneno yake ndiye aliyemuokoa ile siku, otherwsie mambo yangekuwa mengine!

Again mjadala safi, ahsanteni wakuu kwa elimu nzito tunaendelea kule kwa pembeni!
 
mwanahabari thanks for the useful information...nimesoma nikakuta kumbe baraza la mwisho la mawaziri la mwalimu lilikuwa na wizara 14..mawaziri na manaibu jumla 21...safi sana!!

kikwete angetufurahisha kama angeweza kupunguza idadi ya mwawaziri na mnaibu 60..wabaki angalau 28!!!

PM
HESHIMA MBELE MKUU,unajua mkuu muda ule wa nyerere tofauti na sasa,kisiasa,hali ya wananchi na hata hao wabunge bungeni.

mhesh zitto,mkandara,ES and others.....
yes mjadala safi sana.
 
Jokakuu,
bado nadhani unachanganya vitu hapa, itakuwa bora ufahamu kwamba UMMA party na member wake wote walitemwa nje na waliokolewa na Mwalimu kupewa nafasi bara baada ya kuvungiwa Kanyaboya la Muungano...Ebu rudi nyuma msome Zitto alivyosema.

Hawa jamaa hawakupendwa na wanasiasa wa visiwani hata kidogo na ndio maana hadi leo utasikia kuwa mapinduzi yale yalifanywa na WAHUNI tu...iwe mwanachama wa ASP ama HIZBU wote wanafahamu kuwa Babu na chama chake walihusika kwa kiasi kikubwa ktk Mapinduzi yale... kuna picha moja huonyeshwa Babu akipiga kasia kuelekea visiwani siku baada ya Mapinduzi na hakuna maelezo zaidi.. Hata siku moja hakuna mtu aliyetufahamishja WHY alikuwa akirudi Zanzibar siku baada ya Mapinduzi. Tumefunikwa gunia la uso.

Kwa hiyo unapomtaka Salim ajenge base yake ajenge wapi?... Alijenga bara na kama unakumbuka kuna mchangiaji kasema alihamisha familia yake Tabora.

Swala la kuomba serikali ikurudishe nyumbani ni wazo wazimu kwa sababu huyu jamaa hakutakiwa na watu wa visiwani kwa sababu UMMA party ni chama kilichopingana na nadharia zote zinazojenga jamii kwa race zao.. tofauti na wao kisiasa hawa jama walichukua Ukomunist kama ndio mrengo wao kisiasa na walipigwa vita na serikali zote za ndani na nje.

Hivyo Salim kama kijana mdogo sana tena nadhani kuliko hata J.J Mnyika unaweza mwenyewe kufikiria mwaka 1960 tayari alikuwa ktk siasa enzi hizo...
Kwa hiyo huyu jamaa alikuwa hatari tupu na ndio maana alitupwa nje kila akikohoa.

Na sidhani kama kuna mwanachama yeyote wa UMMA party ambaye leo anayo nafasi ndani ya serikali ya Mapinduzi kwa hiyo unaweza kufikiria mwenyewe nafasi ya Salim.
Na kama hukupewa nafasi na utawala unafikiri Salim angefanya nini at his age na kafungwa kamba? Hivi mkuu wewe nambie kama sio Nyerere kuwapa nafasi viongozi wetu nani angewajua leo hiii.. hao waanzilishi wa TAA then TANU wenyewe hakuna Mbongo anayewafahamu zaidi ya kusoma ama kusikia kuwa kulikuwepo na Abdoul Wakil Sykes, tena naweza kusema ni asilimia moja (1) ya Watanzania wanaweza kukwambia kuwa wanafahamu nani mwanzilishi wa TAA nchini.. hata shule haifundishwi...Katika list nzima mzee Mwapachu ndiye alipeta zaidi.

Je, tuwalaumu hawa waasisi kwa nini walikaa pembeni ama nje ya Utawala wasianzishe base yao sehemu? sidhani ni sisi wenyewe kuiweka record clear na pengine kuongeza majina yao ktk Mashujaa wetu.

I doubt marehemu Abdoul Wahid Sykes yupo ktk majina ya mashujaa wetu!...
 
Field Marshalles,
Mkuu kulingana na habari nilizokuwa nazo, habari ya kifo cha Karume ilimfikia Salim akiwa nje hivyo alikatiza kazi zake na kurudi Tanzania lakini alipofika Dar, lawama zilikuwa tayri kwa chama cha UMMA party kuhusika na mauaji hayo.

Hivyo, angefanya kitu gani?
 
Field Marshalles,
Mkuu kulingana na habari nilizokuwa nazo, habari ya kifo cha Karume ilimfikia Salim akiwa nje hivyo alikatiza kazi zake na kurudi Tanzania lakini alipofika Dar, lawama zilikuwa tayri kwa chama cha UMMA party kuhusika na mauaji hayo..
Hivyo, angefanya kitu gani?.

Ndio maana nasema ni lazima salim aandike kitabu kuelezea mengi yaliyojificha, hata kama akiandika aweke script kikachapishwa miaka ijayo itakuwa sawa, maana inaelekea bado kuna kivuli anakiogopa!
 
Hakuna wakati kama mwaka 1984-85 ambapo Salim aliingia kwenye sebule ya Ikulu yetu mara nyingi akiwa kama Waziri Mkuu. Nani sasa anaweza kunielimisha kidogo ni kwa nini hakuteuliwa kugombea Urais wakati huo baada ya Mwalimu kung'atuka?

Ni nini kilifanyika wakati ule hadi Ali Hassan Mwinyi akapewa nafasi ile na Nchi ikaanza kutengeneza/kuzalisha MAFISADI kwa nguvu sana?

Ikaja 1995. Mwalimu alikuwepo, na alipotaja sifa za Rais tunayemtaka wakati ule wengi wetu tukadhani anamlenga Salim. Baba wa watu hakujitokeza kabisa hata kujaza fomu!

Kwa kuwa watu kama Getrude Mongella, Waryoba, Kawawa na wengine bado wapo; wanaweza kutuambia ni nini kilimfanya Salim asite wakati ule? Naamini Tanzania ingekuwa nyingine kabisa kama Salim angeukwaa Urais hasa mwaka 1985.
 
tusiulize masuala mengi kwa nini JKN hakumpa SAS urais wa zanzibar kwa sababu sababu ipo wazi. wazanzibari walioshika madaraka wanamsema SAS kuwa amehusika na mauaji ya Karume mkubwa.

kinachoshangaza ni kuona hajapigiwa debe wakati wa nyerere baada ya nyerere kujiuzulu kushika madaraka ya Tanzania. that is badala ya Mkapa au Mwinyi.

udhaifu wa SAS is he is too diplomatic kwenye mambo yote.

which i think ni trend ya rais ambae hatumuhitaji tanzania kwa sasa.
 
joka kuu hebu kwanza kapekuwe utizame nani alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa serikali huru ya zanzibar chini ya utawala wa Sultani na alitoka chama kipi?
asilan si ASP
 
gaijin,
udhaifu wa SAS is he is too diplomatic kwenye mambo yote.

Mkuu mnaposema maneno haya nashindwa kabisa kuwaelewa...Hivi mtu anapokuwa doplomatic ni upungufu wa kiongozi ktk maswala ya ndani?

Je mnamtaka rais ambaye pia atakuwa jeuri,fisadi na dikteta ambaye atatumia mbinu chafu kama za hawa ili apate kukaa IKULU. Sidhani kama hii ni sifa nzuri kwetu wananchi kwa sababu mwisho ya yote tutaburuzwa...

Sasa tukirudi nyuma na kujiuliza kwa nini Salim hakupewa urais wakati ule wa Mwinyi hali tunafahamu Baraza la Mapinduzi Zanzibar lilimkataa na sababu hazikutolewa...Kumbukeni nchi huii ni ya Muungano na hakuna kitu ambacho Nyerere hakutaka kitokee wakati ule wa mabadiliko ni kuvunjika kwa Muungano.

Je, Nyerere angeweza kulazimisha baraza la Mapinduzi wamkubali Salim?.. sina hakika kwa sababu baraza la mapinbduzi sio majinga hivyo... Wanafahamu pengine kwa hofu zao za kudhulumu mapinduzi na haki ya kutawala Zanzibar chama cha UMMA, kwamba Salim akipata nafasi kama hiyo ndio wakati wa kulipa kisasi ama pengine ukweli wote kuwa wazi.

Hivi leo hata akiandika kitabu sidhani kama wapo watu watamsikiliza....labda kwa kuweka record sawa lakini sidhani kama itaweza kusaidia kitu..
Wamejaribu kina Jumbe leo hii wanaonekana wachawi tu...
 
mkuu mkandara, heshima mbele.
kwa jinsi nchi yetu ilivyomezwa na mafisadi kwa sasa, nahisi hatuhitaji rais aliyekuwa 'too diplomatic' kwenye mambo yote.
sio kama naunga mkono rais dictator, lakini mtu atakaeonyesha authority will be much preferable
 
SALIM ndugu yake (alitokea DENMARK) yuko ILFORD,LONDON na hana sehemu ya kulalasasa leo ataweza kweli kuwasaidia wapemba wakapata maisha bora?

 
GAME THEIRY,

Unapomsema Salim kutazama ndugu yake mkuu ebu kwanza rudi nyuma uzitazame mila za Mdanganyika.....
Tupo kibao ambao tuna ndugu zetu, wazazi wetu wanapuyanga mitaani utafikiria hawa jamaa hawana ndugu wanaojiweza.

Kumbuka tena kuwa viongozi wetu ni binadamu kama sisi wenye kufikiria kama wadanganyika wengine hivyo hawapo mbali na ukweli wa FMES kuwa wao ni reflection yetu sisi tofauti moja tu wameweza kushika madaraka na kuitwa waheshimiwa

Ni mila ya Mdanganyika kutojua kurithisha elimu wala mali zake, utasikia usia usiokwisha jinsi yeye alivyoweza kufanikiwa. Leo hii wapo wazee kibao wamefikia jua la magharibi kimaisha lakini bado wanaendesha biashara zao bila hata kuwahusisha ndugu wala watoto zao, kutokana na kikorosho cha maisha....Na ndio maana wazee wetu wakisha kufa huondoka na kila kheri kiasi kwamba majeshi huandaliwa siku msibani.. Mali itagawanywa, hata nyumba za marehemu zitauzwa kwa sababu sio mila yetu kurithiana elimu, mali, ujuzi ama biashara..sisi hugawana kilichopo na msiba ndio mwanzo wa hujuma za kuua undugu... Hua naelewa sana tunapolia sana kilioni sio kuondokea tu bali balaa linalofuata ni kubwa.. halibebeki.

Hata hivyo, ukitazama upande wa pili wa shilingi hii hii utawakuta ndugu wanaokaa wakitegemea uwashushie rehma. Hawapendi kujituma kikazi wala kutafuta maisha nje ya riziki za wazi kama vile ndugu aliyejaliwa..Kwa bahati mbaya hawa hawa ndugu hufuja mali na pengine hata kuharibu jina la mhusika wakitumia address yako... wao hutuita sisi kina CHUMA ULETE...
Kuna wakti hujiuliza ni mbinu gani haswa inayotakiwa kwetu sisi ku deal na ndugu, jamaa ama jamii hii ya wadanganyika.

Nitakupa mfano mdogo sana, rafiki yako akija na shida ya kukopa fedha basi ni afadhali umpe bure kwa sababu hawezi kuzirudisha atakutia ndani. Ukimwamini ndugu, rafiki na hata mzazi wako kwenye fedha atakuzika sii rahisi hata kidogo kumpata mwaminifu atakayekuwa na uchungu na mali yako ama wadhifa wako. Kwa hiyo yawezekana kutokana na kijimila kama hiki ndo tumepata utaratibu wa KILA MTU NA MZIGO WAKE.

Hivyo basi ni vizuri sana kama ukitafuta undani wa mtu huyo kwanza kabla hujamlalamikia Salim, yawezekana mazishi na mtu anayesubiri kuletewa..na sababu moja kubwa uloitaja wewe mwenyewe.

Kama yukokweli London (nchi yenye kila opportunity) na hana mahala pa kulala wakati sii mlemavu basi nadhni hiyo pekee imekueleza mengi kuhusu huyu jamaa.
 
SALIM ndugu yake (alitokea DENMARK) yuko ILFORD,LONDON na hana sehemu ya kulalasasa leo ataweza kweli kuwasaidia wapemba wakapata maisha bora?


Wakuu Mkandara na GT,
Nafikiri hii inaonyesha jinsi SAS asivyopenda kutumia madaraka yake kunufaisha ndugu zake kama walivyo viongozi wetu wengi. Hata vijana wake mwenyewe wamesomea Dar kama vile mwalimu alivyofanyia wa kwake. Tofauti ni kuwa aliwasimamia wa kwake wote wakafanikiwa kimasomo.

Unlike SAS, Mwandosya alipopata tu uwaziri, watoto wakapelekwa shule US masomoni. Huyu ni civil servant.
 
Wakuu Mkandara na GT,
Nafikiri hii inaonyesha jinsi SAS asivyopenda kutumia madaraka yake kunufaisha ndugu zake kama walivyo viongozi wetu wengi. Hata vijana wake mwenyewe wamesomea Dar kama vile mwalimu alivyofanyia wa kwake. Tofauti ni kuwa aliwasimamia wa kwake wote wakafanikiwa kimasomo.

Unlike SAS, Mwandosya alipopata tu uwaziri, watoto wakapelekwa shule US masomoni. Huyu ni civil servant.


Mwandosya Amekuwa consultant miaka mingi tu na watoto wake walienda nje wakati mwandosya hayuko serikalini na hakuwa civil servant.

Alikuwa mwalimu wa chuo na alikuwa na center yake ya mazingira wakati akiendelea kuwa consultant UN, Eritrea, SADC Namibia, Zimbabwe, siemens (Chairman Tirdo, KIbo paper, TPDC, Mkrugenzi Std Chartered, etc na alikuwa anaandika vitabu) kusema amepeleka watoto nje wakati amepata uwaziri ni uongo, alitoka serikalini 1993.
 
Hata vijana wake mwenyewe wamesomea Dar kama vile mwalimu alivyofanyia wa kwake. Tofauti ni kuwa aliwasimamia wa kwake wote wakafanikiwa kimasomo.

Marekebisho kidogo, watoto wake wamesoma US ambako hata alipoondoka walibaki na mama yao mdogo aliyeolewa na Councilman wa New York, Mr. Jackson.

Watoto wa Mkapa na Salim, wamesomea US walianzia Bunge, ambako sidhani kama watoto wa masikini walikuwa na access nako, unajua huu unazi ndo uliotuletea Mtandao! Sasa ungetegemea kuwa tutakuwa tumejifunza, lakini wapi!
 
Back
Top Bottom